TID akanusha kushindwa kulipa bili Kitambaa Cheupe

TID akanusha kushindwa kulipa bili Kitambaa Cheupe

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2012
Posts
25,438
Reaction score
46,187
Mwanamuziki TID amekanusha vikali madai ya kushindwa kulipa bili ya takribani Sh500,000 katika bar ya Kitambaa Cheupe, Tabata.

Amedai sakata hilo lilopelekea kukamatwa na Polisi, ulikuwa mpango wa kumchafua.

TID ameeleza kama kweli alikuwa anadaiwa, basi wangekata deni lao katika fedha aliyokuwa akiwadai ya show ambayo walimpa.

Vilevile amesisitiza kuwa hakunywa vinywaji vingi kiasi hicho hadi kufikia Sh500,000, na atawachukulia hatua za kisheria kwa kumchafua.

Pia soma:Mwanamuziki TID akamatwa kwa kushindwa kulipa bili Bar
 
Mtu wa hapa kitambaa cheupe alisema Top In Dar(TID) alikuwa na company,
Hakuwa peke yake 😀

Kiufupi ningekuwa mimi TID ningekataa hizi kashfa pia
 
Mwanamuziki TID amekanusha vikali madai ya kushindwa kulipa bili ya takribani Sh500,000 katika bar ya Kitambaa Cheupe, Tabata.

Amedai sakata hilo lilopelekea kukamatwa na Polisi, ulikuwa mpango wa kumchafua.

TID ameeleza kama kweli alikuwa anadaiwa, basi wangekata deni lao katika fedha aliyokuwa akiwadai ya show ambayo walimpa.

Vilevile amesisitiza kuwa hakunywa vinywaji vingi kiasi hicho hadi kufikia Sh500,000, na atawachukulia hatua za kisheria kwa kumchafua.
Kazi sanaaa muda ni mwalim mzuri sanaa tena mwalim mkuu
 
Mtu wa hapa kitambaa cheupe alisema Top In Dar(TID) alikuwa na company,
Hakuwa peke yake 😀

Kiufupi ningekuwa mimi TID ningekataa hizi kashfa pia
Si umeona hapo anakiri kuwa alikunywa na hakulipa lakini anadai bili sio sahihi.
 
Back
Top Bottom