TICTS waendeleza Mgomo- 2.

The Fixer

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
1,365
583
Wafanyakazi wa Kitengo cha kupakua makontena Bandarini TICTS wameendeleza mgomo wao wa kutokufanya kazi mpaka kile ambacho walikiita "Kujua hatima yao " kama serikali ikiifungia kufanya kazi pale Bandarini nini itakuwa hatima yao kimafao kwani katika mkataba wao na TICTS hakuna mahala ambapo kumeelezea kuwa kama TICTS wakiiachishwa kutoa huduma na Serikali wao watalipwa nini ?
Sasa hivi mkutan kati ya DOUTA ambacho ni chama cha Wafanyakazi wa Bandari na Uongozi wa TICTS wapo katika mazungumzo ili kuweka mambo sawa kwani hali inavyoonekana TICTS inaanza kupata hasara tayari Wafanyakazi wanafanya kazi kwa speed ndogo sana... Badala ya kupakua Contena 20 kwa saa sasa wanapakua Contena 3 kwa saa na Meli zinazidi kukaa Bandarini kitu ambacho Principally itatakiwa TICTS kulipa gharama hizo za kukaa pale Ukingoni mwa Bandari bila kupakua mizigo ndani ya meli.

TICTS kumekucha mshika dau KARAMAGI naye yupo ndani ya nyumba na jamaa wala hawaonekani kujali kuwepo kwake ni kufanya kazi kwa speed ya konokono.........!!

More updates baadae........Stay Tuned !
 
Lazima...wajue nini hatma yao....ingawa mwajiri hawezi kujua......atawafanyia nini maana na yeye atakuwa ame data wakati huo......
 
Back
Top Bottom