MziziMkavu binafsi mdogo wangu amepona allerg kwa Mafuta ya Ubuyu,tangu amezaliwa mpaka sasa ana miaka 12 alikuwa yeye ni kukohoa,mafua na kuwashwa macho,amekunywa dawa mpaka utamuonea huruma.
Dada mmoja akatuambia kuhusu Mafuta ya Ubuyu, yeye mwenyewe alikuwa anayauza,na kwa kuwa tunamfahamu akatuambia tusimpe fedha kwanza ila tuchukue tukampe
huyu mdogo wangu na asipopona basi tusimlipe.
Sasa ni wiki ya tatu anaendelea na dozi hakuna cha kukohoa,mafua wala kuwashwa macho.
Nikaamini kweli karibu kila kitu kinachotuzunguka chaweza kuwa Dawa kwa binadamu.
Kwa hiyo mpungara hiyo ni dawa kweli.