THT vs BSS

Hata ulimwengu uliumbwa kwa fikra ndugu. Na yawezekana hao wanaolalamikia muziki hawafikiri. Sasa, hao mapacha waliwabeba weusi kwa kipato kilichotokana na nini? Kama ni muziki mbona leo waanze kulia? Kama ni ishu zingine kwa nini leo walilie muziki? Sijui kama huwa unapata muda wa kujiuliza haya.

Kadhalika haimaanishi kuwa kila afanyaye kazi serikalini kipato chake kinamtosha. Hivyo haimaanishi kuwa kila afanyaye muziki basi aendeshe benzi, maana ndivyo unavyotaka tuamini.

Kingine ninachokiona hapa ni suala la kufuata mkumbo kwa hawa wasanii. Kisa tu fulani kaimba basi nami naweza. Ukiacha hilo kuna suala la kudhani muziki ni kimbilio baada ya kukosa kwingine, hasa kutokana na kukimbia umande. Bangi na malengo wapi na wapi?

nimekwambia Mapacha wamewapa fadhili Weusi,utake ustake ukweli ndio huo,na sio hao kuna wengine wengi...na nimekwambia jamaa ni Wajasiliamali,hawategemei muziki tena...

sasa ngoja nikupe faida ya wao kutoishi kutegemea muziki,kikubwa wao hawaishi kwa kutegemea muziki,ndio maana wapo huru kuzungumza ukweli bila kuwaogopa wadau...watu kama Weusi hawawezi kuzungumza malalamiko yao hadharani sababu wanaogopa kubaniwa nyimbo kupigwa,na airtime ndio inawapa maonyesho maana ata albam hawauzi siku izi...

Na siku zote usijidanganye kuwa kila anaeng'aa kwenye radio au tvs ni mkali...wengi wanatengenezwa tu...usifikiri unapomsikia sana Diamond,then Bele9 umskii ukadhani Bele hana kitu,au kazidiwa kipaji na Diamond..kuna mengi yanafanyika nyuma ya pazia na nyie walaji mnalishwa yalivyopikwa kama yalivyo...we unajua siri ya Diamond kushain?au umejikuta tu unamkubali bila kuelewa kwa nini...ivi siku izi unaskia nyimbo za dansi zinachezwa?unajua kwa nini azichezwi?

Natumai tunakwenda sawa...
 
Kumbe ndugu yangu mambo unajua kuwa maisha si muziki pekee? When one door is closed many more are open. Siri ya ku shine diamond siifaham. Tujuze hapa.

Na kama umefuatilia maongezi vyema kuna sehem tulikubaliana na Gwalu kuwa kuna ombwe la burudani kwani bongofleva ndio imeteka burudani kiasi cha kutufanya na sie tukose msimamo.

Kadhalika sijasema kuwa kila mwenye jina basi ana hela, sio. Kuna masuala mawili nimeyagusia mwishoni naona hujayaona. Hata hao THT walifika hapo kwa kubebwa na vipaji vyao ambavyo vilikuwa havina dira. Walikuwa watu wa kutanga na njia hadi THT ilipowaona na kuwatumia. Na Mawingu wanawatumia kwa kuwa wamewajenga wao. Hapo nazungumzia ukosefu wa elimu. Barnaba na 'nduguze' wanategemea sauti zao tu ambazo zimefikishwa hapo na Mawingu. Wana cha kusema?

Wako wengi pia wamekimbilia muziki kwa kuwa hawakuwa na kingine cha kufanya. Wanaimba, wanarap na mwisho wanachoka wanawekwa kando.

AY nimemjua tangu akiwa CBM crew miaka zaidi ya 10 iliyopita. Alikuwa na malengo na sasa yuko mbali kimaisha. Leo ni nani atamghasi? Huwezi ukamfananisha na hawa waliotengenezwa na THT. Utasema sieleweki. Ukikubali kutengenezwa kwa rehema kubali kulipa fadhila kwa rehema pia.

Wakati tunajadili maumivu wanayopata wasanii wa muziki tujadili pia na sababu za wao kufika hapo. Tusiangalie tu njia wanazopita. Ni rahisi kuzungumzia kuliko kutoa suluhu. Twende na yote mawili

NB: Hata muziki ni ujasiriamali. Au tuanze kozi ya ujasiriamali hapa?
 
ma2mbo nimekuachia kazi hiyo lol......

Kuna kitu lazima tukubaliane hapa......

"MAFANIKIO YA CLOUDS YA KIBIASHARA HAYAHUSIANI NA UKUAJI WA MUSIC....."

Japo wanawatumia sana wanamuziki na vijana wa bongofleva kwenye mafanikio yao.......

Sasa ndugu yangu Raia Fulani unataka kuaminisha au unachanganya kuwa mafanikio ya hao jamaa ni mafanikio ya music ndio kitu nakataa....
Sababu huwezi sema kuna mafanikio ya music katika mazingira hata taratibu za wasanii kutoa album zao hamna.....

Hivi mwaka jana zimetoka album ngapi? ya nani na nani??? Mauzo yake yapoje?? Hao wasanii wana hali gani??

Sasa katika namna kwamba hamna soko la music hao jamaa wako tuwasifu kwa lipi wakati wameshindwa pia.....

Wameshindwa sababu upande mwingine wanawaaminisha watu kama nyie kuwa "music is their business".........

 
Last edited by a moderator:
Hizo ni mbinu za watu kutunisha mifuko yao, bado zitakuja zingine nyingi tu za aina hiyo!
 
ma2mbo nimekuachia kazi hiyo lol......

Kuna kitu lazima tukubaliane hapa......

"MAFANIKIO YA CLOUDS YA KIBIASHARA HAYAHUSIANI NA UKUAJI WA MUSIC....."

Japo wanawatumia sana wanamuziki na vijana wa bongofleva kwenye mafanikio yao.......

Sasa ndugu yangu Raia Fulani unataka kuaminisha au unachanganya kuwa mafanikio ya hao jamaa ni mafanikio ya music ndio kitu nakataa....
Sababu huwezi sema kuna mafanikio ya music katika mazingira hata taratibu za wasanii kutoa album zao hamna.....

Hivi mwaka jana zimetoka album ngapi? ya nani na nani??? Mauzo yake yapoje?? Hao wasanii wana hali gani??

Sasa katika namna kwamba hamna soko la music hao jamaa wako tuwasifu kwa lipi wakati wameshindwa pia.....

Wameshindwa sababu upande mwingine wanawaaminisha watu kama nyie kuwa "music is their business".........


Naona hata hamtaki kunielewa sasa. Labda kwa kuwa hausomi ninachoandika, kaka. Ungekuwa unasoma wala usingetoa jibu hili. Hii mada tuipumzishe kwa sasa.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom