naa
JF-Expert Member
- May 5, 2013
- 1,766
- 3,797
Anakuja Mzungu anasema anahitaji Ngedere, ananunua mmoja kwa bei ya 20,000/=, basi wanakijiji wanahaha kusaka ngedere, wanawaleta Mzungu ananunua wote anasepa nao.
Anarudi tena anasema vipi, naona wameadimika, sasa ntanunua kwa bei ya 35,000 ngedere mmoja, wanakijiji wanaenda deep zaidi msituni, kamata ngedere, leta kwa mzungu, mzungu anasepa nao.
Alafu wiki mnayofuatia Mzungu anasema bado anataka ngedere, saivi atanunua kwa Laki. Wanakijiji macho yamewatoka, hawana tena Ngedere.
Mzungu anasema basi ntaftieni kwa Laki na Nusu. Kesho yake inasikika kuwa kuna Mchagga anauza Ngedere kijiji cha pili, anauza kwa 100,000/=, wanakijiji wanawahi fasta wanaenda nunua Ngedere wote wa kijiji cha pili. Wanarudi kijijini hawana pesa ila wana ngedere wakijua watamuuzia mzungu fasta kwa laki na nusu, Mzungu hatokei Ng'oooo!!!!
Infact, yule mzungu alikuwa anawakusanya tu na kuwahifadhi kule kijiji cha pili akijua ataja wauza kwa 100,000/= kwa hawa hawa wa kijiji hiki.
Mwenye macho na aone, mwenye masikio na asikie. Muwe na usiku mwema wakuu.
Anarudi tena anasema vipi, naona wameadimika, sasa ntanunua kwa bei ya 35,000 ngedere mmoja, wanakijiji wanaenda deep zaidi msituni, kamata ngedere, leta kwa mzungu, mzungu anasepa nao.
Alafu wiki mnayofuatia Mzungu anasema bado anataka ngedere, saivi atanunua kwa Laki. Wanakijiji macho yamewatoka, hawana tena Ngedere.
Mzungu anasema basi ntaftieni kwa Laki na Nusu. Kesho yake inasikika kuwa kuna Mchagga anauza Ngedere kijiji cha pili, anauza kwa 100,000/=, wanakijiji wanawahi fasta wanaenda nunua Ngedere wote wa kijiji cha pili. Wanarudi kijijini hawana pesa ila wana ngedere wakijua watamuuzia mzungu fasta kwa laki na nusu, Mzungu hatokei Ng'oooo!!!!
Infact, yule mzungu alikuwa anawakusanya tu na kuwahifadhi kule kijiji cha pili akijua ataja wauza kwa 100,000/= kwa hawa hawa wa kijiji hiki.
Mwenye macho na aone, mwenye masikio na asikie. Muwe na usiku mwema wakuu.