britanicca
JF-Expert Member
- May 20, 2015
- 18,029
- 46,326
RUSHWA HUANZAJE KWENYE SYSTEM?
1.Unaachiwa maziwa au unamuachia mtoto wako mkubwa chakula cha mdogo anakula chote,
2.Monitor darasani anawapanga wengine ratiba za usafi lakin rafiki yake hampangi kwenye ratiba ya usafi
3.Mwalimu wa stard za kazi au sanaa anawatuma mayai nyumbani anawapa marks za kutosha wakati waliyochonga sanaa za mwiko wanapata 10 au 20, huu ujinga huleta rushwa
Haya yote ndo yamepekea watotot hao kukua na kuwa viongozi wakubwa wakatuibia kwenye RICHMOND au KAGODA , MIGODI au kujimilikisha Lunch, ufisadi uanza hivyo
Usishangae yule wa RICHMOND alikuwa nakunywa maziwa ya mdogo wake, au aliiba sana penseli za wenzake hapo shule Tabia ikakua haikukemewa kabisa ikaleta madhara kwa taifa,