The Way Forward - UKAWA

Magehema

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
428
27
Nadhani baada ya Katiba pendekezwa kupitishwa katika Bunge la Katiba umefika wakati sasa kwa UKAWA kutumia busara na hekima za kutosha ili kuipata Katiba ya Wananchi kama ilivyopendekezwa na Jaji Warioba. Kwa mtazamo wangu sioni sababu ya hawa ndugu zetu wa Ukawa kutumia nguvu nyingi kutaka kupambana na mamlaka kwa jambo ambalo tayari limeshapitishwa kisheria ingawa halina uhalali wa kisiasa.

Cha kufanya:
Ukawa watulizane, wajifungie mahali na wafanye kazi ya kuipitia Katiba pendekezwa kwa jicho la kisiasa, kisheria na kisha warudi kwa wanachi kupitia majukwaa halali na kuwaeleza ni nini tofauti ya Katiba pendekezwa vs Rasimu ya Tume. Wawe wa kweli, naamini Katiba pendekezwa ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu ya kutosha, vivyo hivyo Rasimu ya Tume ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu.

Wawaeleze wananchi ni marekebisho yapi ambayo Rasimu ya Tume ilihitaji kufanyiwa ili ikidhi mahitaji ya sasa na ya baadae ya nchi yetu.

Na mwisho wa siku waibebe Rasimu ya Tume yenye marekebisho yao kama agenda ya uchaguzi mwaka ujao.

Nawasilisha
 
Hicho ndo kilichowaponza wachangiaji wengi wa kipima joto cha jana ITV (kwa walioangalia). Wachangiaji wengi hawakuweza kuwa na point za muhimu za utofauti wa katiba pendekezwa, rasimu ya pili na ukizi wa mahitaji ya sasa. Ni wakati wa kutafakali nini cha kufanya.....
 
UKAWA wameonyesha njia sahihi kabisa na wala hawana haja ya kusikiliza matangazo ya michepuo ,kilichobakia ni kwa wananchi wenyewe aidha wasijitokeze kupiga kura kama waliogomea sensa au kama wakienda basi wajue wanaenda kuandika HAPANA au NDIO ili wasije wakawalaumu wanasiasa wa UKAWA pale Katiba itakaposhindwa kuwatia hatiani wahujumu uchumi mapapa.
 
UKAWA wameonyesha njia sahihi kabisa na wala hawana haja ya kusikiliza matangazo ya michepuo ,kilichobakia ni kwa wananchi wenyewe aidha wasijitokeze kupiga kura kama waliogomea sensa au kama wakienda basi wajue wanaenda kuandika HAPANA au NDIO ili wasije wakawalaumu wanasiasa wa UKAWA pale Katiba itakaposhindwa kuwatia hatiani wahujumu uchumi mapapa.

Ukiangalia Katiba ya pendekezwa kwa mrengo wa UKAWA unaiona kama ina mapungufu lakini ukiitazama kwa mrengo wa maslahi ya wananchi , iko fiti kinoma, hakuna sababu yoyote ile ya wananchi kuhofia kuipigia kura ya ndiyo.
 
Hicho ndo kilichowaponza wachangiaji wengi wa kipima joto cha jana ITV (kwa walioangalia). Wachangiaji wengi hawakuweza kuwa na point za muhimu za utofauti wa katiba pendekezwa, rasimu ya pili na ukizi wa mahitaji ya sasa. Ni wakati wa kutafakali nini cha kufanya.....

kile kinaitwa kipima joto cha MENGI siyo cha ITV. Ni Mengi ndiyo anawaelekeza maswali ya kuwauliza wananchi tena wananchi wenyewe wanaoulizwa utakuta wengi wanaitwa Masawe, Tarimo, Ngoli, Elisante n.k Majina ya huko huko. Sijawahi kusikia Marwa, Robi, Chacha au Bhoke, wakiulizwa hayo maswali ya kipimajoto cha MENGI
 
Hicho ndo kilichowaponza wachangiaji wengi wa kipima joto cha jana ITV (kwa walioangalia). Wachangiaji wengi hawakuweza kuwa na point za muhimu za utofauti wa katiba pendekezwa, rasimu ya pili na ukizi wa mahitaji ya sasa. Ni wakati wa kutafakali nini cha kufanya.....
Jana kulikuwa na kina mama wengi na mahitaji yao ya usawa (NGO) tu wamebaki pongeza. Sikuona watu waliweza kuchambua vipengele vya rasimu zote 2.
 
ukawa jeneza.jpg
 
kile kinaitwa kipima joto cha MENGI siyo cha ITV. Ni Mengi ndiyo anawaelekeza maswali ya kuwauliza wananchi tena wananchi wenyewe wanaoulizwa utakuta wengi wanaitwa Masawe, Tarimo, Ngoli, Elisante n.k Majina ya huko huko. Sijawahi kusikia Marwa, Robi, Chacha au Bhoke, wakiulizwa hayo maswali ya kipimajoto cha MENGI
Mtu asiye na hoja marazote hukimbilia kwenye mambo ya kipuuzi. Tumia akili vizuri kwa manufaa ya Taifa.
 
Nadhani baada ya Katiba pendekezwa kupitishwa katika Bunge la Katiba umefika wakati sasa kwa UKAWA kutumia busara na hekima za kutosha ili kuipata Katiba ya Wananchi kama ilivyopendekezwa na Jaji Warioba. Kwa mtazamo wangu sioni sababu ya hawa ndugu zetu wa Ukawa kutumia nguvu nyingi kutaka kupambana na mamlaka kwa jambo ambalo tayari limeshapitishwa kisheria ingawa halina uhalali wa kisiasa.

Cha kufanya:
Ukawa watulizane, wajifungie mahali na wafanye kazi ya kuipitia Katiba pendekezwa kwa jicho la kisiasa, kisheria na kisha warudi kwa wanachi kupitia majukwaa halali na kuwaeleza ni nini tofauti ya Katiba pendekezwa vs Rasimu ya Tume. Wawe wa kweli, naamini Katiba pendekezwa ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu ya kutosha, vivyo hivyo Rasimu ya Tume ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu.

Wawaeleze wananchi ni marekebisho yapi ambayo Rasimu ya Tume ilihitaji kufanyiwa ili ikidhi mahitaji ya sasa na ya baadae ya nchi yetu.

Na mwisho wa siku waibebe Rasimu ya Tume yenye marekebisho yao kama agenda ya uchaguzi mwaka ujao.

Nawasilisha


Uhalali wa katiba ni mmoja tu, "SHARTI MAWAZO YA WANANCHI KUZINGATIWA" Full stop?
Hayo mengine ya kusema Ukawa wajifungie, sijui waitazame rasimu kwa jicho la kisiasa na kisheria. Ni bora ukayaweke hayo maneno yako kwenye kanga maana unaweza ukawauzia kina Makonda na Anakilango m.
 
well said ila wasikimbie bunge tena

Hayo marekebisho wangeweza kuyafanya walipokuwa bungeni ila sijui ni wazimu gani uliwapanda wakaamua kutoka nje.

Katiba pendekezwa ni nzuri 100%

Ukiangalia Katiba ya pendekezwa kwa mrengo wa UKAWA unaiona kama ina mapungufu lakini ukiitazama kwa mrengo wa maslahi ya wananchi , iko fiti kinoma, hakuna sababu yoyote ile ya wananchi kuhofia kuipigia kura ya ndiyo.

 
hilo neno....yaani umewashauri haswaa...lakini jamaa zangu hawa ni sikio la kufa...wao uchu wao ni madaraka tu na ndio maana wanan'gan'gania serikali tatu....Sisi wenzao tumeijadili ile rasimu tukapitisha karibu asilimia sabini na tano ya maoni yake na tukaongeza yale ambayo jaji wenu aliyaacha kwa makusudi na tukaondoa yale yote yanayotishia umoja wetu na amani yetu....Jamaa zako wa Ukawa wakajichimbie na waje na rasimu mbadala watakayoibeba kama agenda yao uchaguzini lakini kwa hii katiba mpya....tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele..
Nadhani baada ya Katiba pendekezwa kupitishwa katika Bunge la Katiba umefika wakati sasa kwa UKAWA kutumia busara na hekima za kutosha ili kuipata Katiba ya Wananchi kama ilivyopendekezwa na Jaji Warioba. Kwa mtazamo wangu sioni sababu ya hawa ndugu zetu wa Ukawa kutumia nguvu nyingi kutaka kupambana na mamlaka kwa jambo ambalo tayari limeshapitishwa kisheria ingawa halina uhalali wa kisiasa.

Cha kufanya:
Ukawa watulizane, wajifungie mahali na wafanye kazi ya kuipitia Katiba pendekezwa kwa jicho la kisiasa, kisheria na kisha warudi kwa wanachi kupitia majukwaa halali na kuwaeleza ni nini tofauti ya Katiba pendekezwa vs Rasimu ya Tume. Wawe wa kweli, naamini Katiba pendekezwa ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu ya kutosha, vivyo hivyo Rasimu ya Tume ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu.

Wawaeleze wananchi ni marekebisho yapi ambayo Rasimu ya Tume ilihitaji kufanyiwa ili ikidhi mahitaji ya sasa na ya baadae ya nchi yetu.

Na mwisho wa siku waibebe Rasimu ya Tume yenye marekebisho yao kama agenda ya uchaguzi mwaka ujao.

Nawasilisha
 
Ati sharti mawazo ya wananchi kuzingatiwa....kama ni kuzingatia basi wale wengi ambao hawakutaka kabisa hoja ya serikali tatu ndio wangekuwa wamepewa kipaumbele....HAKUNA SHARTI MAWAZO YA WANANCHI HAPA KWANI TUTAKWENDA KWA HAO WANANCHI UNAOWASEMEA SASA ili wao waamue kama kweli UKAWA wako sahihi au wale waliobaki bungeni na kujadili hadi kupata katiba pendekezwa katika hali ya utulivu na maelewano..acheni ushabiki na uroho wa madaraka .....walipoondoka bungeni walidai wanatukanwa...mara wakaja na hoja ati lazima serikali tatu...mara wakasema ahirisha bunge....sasa sijui watasemaje maana sisi wazalendo wa nchi hii tumethubutu, tuemweza na tunasonga mbele.....karibuni mshuhudie makabidhiano dodoma
Uhalali wa katiba ni mmoja tu, "SHARTI MAWAZO YA WANANCHI KUZINGATIWA" Full stop?
Hayo mengine ya kusema Ukawa wajifungie, sijui waitazame rasimu kwa jicho la kisiasa na kisheria. Ni bora ukayaweke hayo maneno yako kwenye kanga maana unaweza ukawauzia kina Makonda na Anakilango m.
 
well said ila wasikimbie bunge tena

Maamuzi ya UKAWA bado yanasimama na yatasimama siku zote....kususia bunge la katiba yalikua maamuzi bora kabisa...Hata upitishwaji wa rasimu yenyewe umefanywa kwa udanganyifu...Kura Mbili za maruhani....Hao wajumbe hawatajwi...wamefanywa siri........Ni kina nani? haijulikani

UKAWA wako sahihi kwa sababu hata wangeshiriki usitarajie la tofauti lingetokea kutokana na bunge lenyewe lilivyoundwa(Tangu mwanzo uteuzi wa wajumbe uliofanywa na JK uliangalia makada wa CCM kupitia makundi yao).

Kwa sababu hizo UKAWA waliona mbali kwamba product ya bunge hilo itakuwa "Bora katiba" na sio katiba bora.

Ulitaka UKAWA wabaki ili waendelee kubezwa na kutukanwa na CCM ilihali hata katiba yenyewe isingekuwa bora.?

Tuwashukuru UKAWA kwa sababu wamekuwa wazalendo vya kutosha kuweza kuacha pesa na kuokoa zaidi ya Sh bilioni 3 ambazo zingetumika kuleta bora katiba.

UKAWA wameweza kusimamia lile wanaloliamini....wameepuka ulafi wa posho ...

UKAWA wameepuka kuwa rubber stamp kwa katiba ambayo haitadumu asilani.

UKAWA wameweza kutusaidia kuona sura halisi ya CCM na mawakala zake...Uzomeaji...utukanaji...kufanya fujo na vurugu bungeni..Watanzania wameona kabisa nani ni tatizo.

UKAWA wameweza kutusaidia watanzania kuthibitisha jinsi CCM wanavyoiba kura kila mara...Kitendo cha kura za zanzibar ku fluctuate kutokana na mahitaji kimethibitisha hili......

Mwisho wa Siku.....Katiba ni document inayotakiwa kuliweka pamoja taifa....ni product ya maridhiano na sio mashindano....

Katiba inatakiwa kuwa mkataba kati ya watawala na watawalwa..........Katika "Bora Katiba" watawala wamejiweka katika nafasi ya kutohojiwa wala kubanwa na watawalwa......

UKAWA bado wataendelea kudai katiba MPYA...Na hii ajenda itasimamiwa katika Coallition ya Vyama vya UKAWA katika chaguzi zote zijazo.

Watanzania tusikate tamaa....Tuendelee kupambana...Tutaipata katiba iliyo centred kwa wananchi.....
 
Nadhani baada ya Katiba pendekezwa kupitishwa katika Bunge la Katiba umefika wakati sasa kwa UKAWA kutumia busara na hekima za kutosha ili kuipata Katiba ya Wananchi kama ilivyopendekezwa na Jaji Warioba. Kwa mtazamo wangu sioni sababu ya hawa ndugu zetu wa Ukawa kutumia nguvu nyingi kutaka kupambana na mamlaka kwa jambo ambalo tayari limeshapitishwa kisheria ingawa halina uhalali wa kisiasa.

Cha kufanya:
Ukawa watulizane, wajifungie mahali na wafanye kazi ya kuipitia Katiba pendekezwa kwa jicho la kisiasa, kisheria na kisha warudi kwa wanachi kupitia majukwaa halali na kuwaeleza ni nini tofauti ya Katiba pendekezwa vs Rasimu ya Tume. Wawe wa kweli, naamini Katiba pendekezwa ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu ya kutosha, vivyo hivyo Rasimu ya Tume ina mazuri yake ingawa pia ina mapungufu.

Wawaeleze wananchi ni marekebisho yapi ambayo Rasimu ya Tume ilihitaji kufanyiwa ili ikidhi mahitaji ya sasa na ya baadae ya nchi yetu.

Na mwisho wa siku waibebe Rasimu ya Tume yenye marekebisho yao kama agenda ya uchaguzi mwaka ujao.

Nawasilisha

Ukawa wapo sahihi kabisa mpaka wakati huu na vizazi vijavyo vitaikuta historia hiyo,msingi mkuu au sababu za raisi Jakaya kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya alikuwa akitafuta uhalali hasa kwa nchi inayojipambanua kuendeshwa kwa demokrasia.Sababu za hitaji la katiba mpya ni kuwa hii iliyokuwapo haikutokana na wananchi wa Tanzania ila ilitungwa na kikundi cha watu wachache na ndio sababu ya kuundwa kwa tume ya katiba iweze kuyachukua maoni ya wananchi.Hoja ya kuwa UKAWA walikosea sio sahihi UKAWA wana hoja za msingi hata kama ni wachache.Tunajua italazimishwa na itapita katika upigaji wa kura lakini bado wananchi watadai katiba mpya kwa sababu zile zile(uhalali) zilizopelekea hii ya sasa 1977 kuonekana kukosa uhalali wa moj kwa moja.Tunajenga taifa taifa moja ni vizuri kuwa wamoja,swali kidogo kwako kama katiba ni jambo la maridhiano je hii rasimu ya Sitta iliyopitishwa Bungeni imezingatia maridhiano?
 
Uhalali wa katiba ni mmoja tu, "SHARTI MAWAZO YA WANANCHI KUZINGATIWA" Full stop?
Hayo mengine ya kusema Ukawa wajifungie, sijui waitazame rasimu kwa jicho la kisiasa na kisheria. Ni bora ukayaweke hayo maneno yako kwenye kanga maana unaweza ukawauzia kina Makonda na Anakilango m.
Very well said, chukua big like.
 
Back
Top Bottom