The vatican changing tone on homesexuality?!

The vatican changing tone on homesexuality?!

Status
Not open for further replies.
Kanisa linapotoa reference kwenye ripoti na utafiti nashindwa kuwaelewa sijui ni nini cha kujadili kuhusu hili suala wakati

Bible imepinga vikali kabisa na iko wazi na wasipotoa msimamo wao kwa kunukuu Bible sijui wanahubiri nini??
 
Huo mkutano haujadili kubadilisha Doctrine yoyote ya Kanisa na pamoja na habari hizi kuandikwa kwa uzuri kufurahisha wale ndugu zetu pamoja na maadui wa kanisa bado wasiojua mifumo ya Kanisa Katoliki kesho wataandika kabisa "Kanisa Katoliki lakubali ushoga" .....kwa anayetaka kuelewa nini kilijadiliwa aingie kwenye official site za Kikatoliki ili usome ujumbe halisi na si hizi tafsiri zenye lengo la kuonesha sasa Kanisa linatambua mashoga ...... Kwa mnaosubiri Kanisa kutangaza kuwatambua rasmi mashoga mtangoja MILELE ......miaka zaidi ya 2000 kanisa ni moja na halijawahi kuyumba kimafundisho ......nani aliyumbishe sasa? Hao activist wenye media kubwa kubwa na ambao watu wetu wengi wanachota habari zenye tafsiri zao?
 
141005195936_pope_synod_512x288_getty.jpg


Makasisi wanaoshiriki katika mkutano wa maaskofu wanaangazia masuala ya mafunzo ya kanisa katoliki kwa familia ,wametoa mwito kwa kanisa hilo duniani kuwachukulia watu wenye mapenzi ya jinsia moja kwa usawa

Kauli hii inakuja baada ya Maaskofu kuandika ripoti wakati wa mkutano wa synodi ukiendelea huko Vatican na kusema kuwa wapenzi wa jinsia moja wana zawadi na viwango vya kutoa kwenye jumuiya za kikristo hii ikiwa ni ripoti iliyotolewa mapema wiki hii.

Ripoti hiyo haitoi changamoto yoyote kwa msimamo wa muda mrefu wa kanisa hilo juu ya kupinga ndoa za jinsia moja,lakini baadhi ya vikundi vya kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja wanachukulia kauli hiyo kuwa ya mafanikio makubwa kwa jamii zao.

Na moja ya makundi yenye kushikilia msimamo mkali kikanisa wametupilia mbali ripoti hiyo na kuuita ya kisaliti.

Zaidi ya maaskofu 200 wa kanisa katoliki wanakutana kwenye mkutano wa synodi tangu mapema mwezi huu,katika mkutano huo ni papa Francis aliyetoa mwito wa kujadili masuala ya utoaji wa mimba,vidonge vya uzazi wa mpango,mapenzi ya jinsia moja na talaka.

Papa Francis amewataka viongozi wa juu wa kanisa hilo kuzingatia Zaidi suala la wapenzi wa jinsia moja chanya kuliko kuwa kinza na amefanikiwa kuwateka maaskofu wanaohudhuria mkutano huo wa sinodi.

Mwaka uliopita katika ripoti aliyo itoa papa Francis kuhusiana na mwenendo wa kanisa katoliki kuwa waumini walio wengi waliliacha mkono kanisa hilo kutokana na mafunzo yahusianayo na ngono na dawa za uzazi wa mpango.

Papa huyo anazichukulia ndoa hizo za jinsia moja kama zisizo na utaratibu akiinukuu ripoti ya kanisa katoliki iliyochapishwa mwaka 1986,wakati Papa Francis alipokua mshauri mkuu wa masuala ya teolojia ya kanisa katoliki wa hayati papa John Paul wa pili.

Nguvu kubwa ya vikundi vya kutetea haki za watu wenye mapenzi ya jinsia moja ni juu ya kauli ya papa Francia aliyoitoa mwishoni mwa mwaka wa jana alipokuwa kwenye kambi ya vijana wa kanisa hilo huko Rio de Jeneiro alitoa kauli kua kama mtu anamtafuta Mungu na ana nia njema ,yeye ni nani wa kuhoji?

Papa Francis anaingia katika historia ya kanisa katoliki ulimwenguni kutumia jina (hasha kum si matusi) ------- hadharani kuliko kutumia neno wapenzi wa jinsia moja.

CHANZO: BBC
 
Jamani ulimwengu unakwenda wapi? tujifiche wapi na hasira ya Mungu?

karibuni wadau mtoe mawazo yenu...
 
Hii habari inapotoshwa na mashoga kwa maslahi yao wenyewe.

Kanisa Katoliki halitaweza kuukubali ushoga miaka yote.
 
Kwa kuogopa hasira za mungu BMK hata kujadili hawakutaka,tusubiri ya kanisa ukizingatia kesi za kulawiti zililitingisha kanisa.
 
Kwa kuogopa hasira za mungu BMK hata kujadili hawakutaka,tusubiri ya kanisa ukizingatia kesi za kulawiti zililitingisha kanisa.


Hali inatisha mkuu

Mungu aturehemu maana machukizo yameingia nyumbani pake
 
Umesoma source? BBC ni ya mashoga?

Aliyekwambia BBC hakuna "makanjanja" ni nani? Au kitu kikiwa cha "mweupe" ndo kinakuwa perfect kwa asilimia 100?

Waziri mkuu wa nchi iliyo makao makuu ya hiyo BBC si ndiyo alikuwa anatuhimiza tuukubali ushoga?
 
Aliyekwambia BBC hakuna "makanjanja" ni nani? Au kitu kikiwa cha "mweupe" ndo kinakuwa perfect kwa asilimia 100?

Waziri mkuu wa nchi iliyo makao makuu ya hiyo BBC si ndiyo alikuwa anatuhimiza tuukubali ushoga?


Mkuu habari ndiyo hiyo kwakweli inatisha kanisa kukubali hili
 
Hii habari inapotoshwa na mashoga kwa maslahi yao wenyewe.

Kanisa Katoliki halitaweza kuukubali ushoga miaka yote.

Nilitegemea watu kama nyie mngejitokeza kwa kujifarij . Badala ya kujibu hoja mnaleta blabla. Hebu fafanua upotoshaji ni upi na ukweli pia ni upi ili tukuelewe..
 
Kwa mtu asiyekuwa na akili atakwenda na maji. Ila ushoga haupo na hautakuwepo roman catholic. Kama umesoma vizuri utaelewatu. Ila ukikurupuka utaenda na maji.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom