"Hivi mnaona kile ambacho mimi nakiona?" Walker aliwauliza wenzake kwa kunong'ona lakini sauti yake ikionyesha kabisa taharuki ambayo alikuwa nayo.
Wote wakakodoa macho kutazama pale kwenye geti ili kung'amua kile ambacho Walker alikuwa anakiona.
"Mungu wangu, simani macho yangu.!!" Mzee Caleb akajishika mkono kifuani kwenye moyo kutokana na taharuki.
"Ndio Mzee… yule ni Vice President David Logan!!"
Walker aliongea huku wote wakiwa wamemkazia macho mwanaume wa kizungu ambaye alikuwa ameongozana na wale watu wengije watatu wakitoka ndani ya geti la lile Kasri.
"Tunafanyaje?" Moja ya makomando wale aliuliza.
"Yule ni Makamu wa Rais wa nchi yetu… ni lazima tuhakikishe kama yuko salama!" Walker aliongea huku bado akiwatazama wale watu ambao walikuwa wanatoka kwenye geti na David Logan.
"Lakini haonekani kama yuko kwenye hatari… anaonekana yuko hapa kwa hiari yake kabisa.!" Mzee Caleb akaongea.
"Ni jukumu langu kama afisa wa Ulinzi wa nchi yangu kuhakikisha yuko salama… lets go!" Walker ambaye ndiye alikuwa kamanda wa wenzake kwa sasa hakutaka kujadili zaidi… aliamuru wote wamfuate.
Walitembea kwa tahadhali kubwa kuwafuata wale watu pale getini.
"Kuweni tayari kwa lolote!" Walker aliwataahadhalisha wenzake kuwa macho ikitokea wakishambuliwa kwa ghafla.
Kadiri ambavyo walikuwa wanawasogelea kutoka msituni ndivyo ambavyo pia wale watu waliongozana na Logan na pamoja na Logan mwenyewe walisimama na kuanza kutazama msituni.
Yule mwanaume mmoja mweusi aliye pamoja na kina Logan alionekana kuwaonyeke ishara ya kidole mdomoni kwamba wanyamaze wasiongee kwa kuwa kuna kitu anakisikia msituni.
Ghafla… kufumba na kufumbua. Walker na wenzake waliruka kutoka msituni na kuwazunguka Logan na wenzake.
"Muweke salama Vice President!!" Walker aliamuru.
Mmoja ya mwanajeshi mwenzake alimnyakua David Logan kwa kasi na kumtenganisha na wale watu watatu ambao alikuwa nao.
Yule jamaa mweusi ambaye alikuwa na Logan aliruka kiustadi na kuanza kupambana na akina Walker. Alionekana dhahiri kuwa alikuwa ana uwezo mkubwa wa mapambano ya ngumi lakini kutokana na kuzidiwa wingi alidhibitiwa mara moja na wanajeshi wa Walker.
"Niko salama, niko salama… hawa ni watu wema waacheni… niko salama!" David Logan alisisitiza.
Aligundua kuwa hao walikuwa ni vijana kutoka kwenye moja ya vyombo vya Ulinzi nchini Marekani.
"Una hakika uko salama Mr. Vice President?" Walker aliuliza kwa msisitizo huku wanakukuruka kumdhibiti yule jamaa mweusi.
"Nimesema waacheni!" David Logan aliongea kwa mamlaka safari hii kwa kutoa amri.
Wakamuachia yule jamaa mweusi ambaye walimdhibiti kwa kumgandamiza chini kwenye mchanga.
Jamaa mweusi aliyeachiwa na akina Walker walikuwa bado wanaangaliana kwa hasira wote wakisubiri Logan aseme kitu kuweka mambo sawa.
"Uko salama Mr. Vice President?" Walker aliuliza tena kwa mara nyingine.
"Niko salama kabisa… mmefikaje hapa?" Logan akauliza kwa mshangao.
"Ni hadithi ndefu sana… labda utueleze wewe umefikaje hapa?" Walker alijibu swali kwa swali.
Wakiwa wanasuburi maelezo, macho ya Logan na Mzee Caleb yakagongana na Logan akamtambua.
"Mzee Caleb…! Ulisikia kiiichotokea Whitehouse?" Logan akauliza akikumbusha tukio lilitokea ambapo alivamiwa na mtu mwenye kufanana kabisa na Caleb.
"Nilisikia Muheshimiwa na nimewapa hawa maelezo ni nini kinaendelea… nitakueleza na wewe pia!" Mzee Caleb akaeleza kwa kifupi tu.
"Vipi mlifanikiwa kupata kile kitabu aaahh Book of… Book of…"
"BOOK OF CODES!" Mzee Caleb akamsadia David Logan kukumbuka.
Mara ya mwisho Logan na Mzee Caleb kukutana, ilikuwa ni pale ambapo Mzee Caleb alipelekwa Whitehouse na Mkurugenzi wa CIA Bw. James Rupert ili kueleza siri iliyomo ndani ya mchoro wa George Washington unaokaa Estern Room ya hapo Whitehouse. Kisha wakaondoka kwa pamoja mpaka Chuko Kikuu cha Stanford ambako walienda kutazama chupa ambayo iliokotwa huko Maldives na kufunguliwa na kuanzisha kizaa zaa cha miji kutwaliwa duniani. Japo waliikosa chupa hiyo kwa maelezo kwanba imeibiwa na mmoja wa wataalaku wa Idara ya Akiolojia ya chuo hicho ambaye amesafiri kwenda nchini Tanzania.
Kisha wakaondoka kutoka chuoni hapo kwa msafara wa pamoja ambao ulishambuliwa na watu wa ajabu ambao baadae walikuja kugundulika ni wapiganaji wa kikundi cha siri cha Sancta Cedes.
Ndipo hapa ambapo Mzee Caleb alitoa pendekezo la kwenda Maryland kwenye msitu wa Ox kwenye kaburi la babu yake ambako walifukia kitabu cha siri kinachoitwa BOOK OF CODES ili waweze kupambana na kikundi hicho cha siri cha Sancta Cedes.
Makamu wa Rais akatoa ruhusu mkurugenzi Mkuu wa CIA Bw. James Rupert ampatie Caleb na Naomi kikosi cha siri cha kijeshi cha CIA kinachoongozwa na Ethan kiongozana na Caleb na Naomi kwenye msitu wa Ox huko Marylanda.
"Ethan na Naomi wako wapi?" Logan akamuuliza Mzee Caleb baada ya kuunganisha nukta kwamba wanajeshi hao walio pamoja na Caleb watakuwa ni vijana wa Ethan.
"Walirudi Washington baada ya kupata taarifa kuwa umevamiwa Whitehouse!" Walker akajibu.
"Kwa hiyo mnamaanisha kwamba walienda Whitehouse?" Logan aliuliza kwa taharuki kiasi.
"Ndio Mr. Vice President." Walker akajibu.
"Damnt it! Lazima yule mwanamke atakuwa amewatia nguvuni!" David Logan aliongea kwa hasira huku amejishika kichwa.
"Mwanamke gani?" Wakajikuta wote wote wameuliza kwa pamoja.
"Madam President Laura Keith.!" Logan akajibu.
Wote wakashikwa na mshangao ghafla. Hawakuwa wanajua kile ambacho kilikuwa kinaendelea nyumbani Marekani.
"Nitawaeleza.!" David Logan akajibu tena kwa kifupi tu.
"Sawa Mr. Vice President… lakini hatujui tuko mahala gani hapa na ni muhimu tukijua nini kimetokea mpaka umefika hapa..!" Walker akauliza tena.
"Tupo Rabat, Morocco!" Cindy akajibu
"Samahani sikuwatambulisha… huyu ni Dr. Cindy Wheaton… Mzee Caleb yule mtaalamu wa Akiolojia ambaye tukiambiwa pale Stanford ameondoka na chupa ya Maldives na kwenda nayo Tanzania ndiye huyu… huyu hapa anaitwa Magdalena ni mtaalamu wa Biolojia kutoka Kenyatta University na huyu hapa ni Salim, Afisa ya Idara ya Usalama nchini Tanzania.!" Logan alifanya utambulisho wa haraka haraka.
Mzee Caleb, Walker na wenzake walibakia wametumbua macho tu kama wamechanganyikiwa. Walikuwa wanajiuliza ni namna gani Makamu wa Rais David Logan siku kama moja au mbili nyuma alikuwa Whitehouse amevamiwa na watu wasiojulikana kwa mujibu wa taarifa waliyoipata na sasa hivi yuko hapa na watu kutoka Tanzania na Kenya. Ulikuwa ni mkanganyiko mkubwa vichwani mwao.
"Mr. Vice President nadhani unaweza kuhisi ni namna gani tumechanganyikiwa vichwani mwetu!" Walker akaongea tena.
"Nafahamu… lakini hatuna muda wa kupoteza! Tunapaswa kufika sehemu haraka sana!"
"Sehemu gani?"
"Tunapswa kutafuta Hekalu la Mungu Zeus lilipo hapa Rabat!" Logan aliongea huku anaanza kutembea.
Sio Mzee Caleb, Walker na wanajeshi wenzake pekee ambao walishtuka bali pia hata Cindy, Magdalena na Salim. Walipotoka ndani ambako walimkuta kama amechanganyikiwa na baadae akili zake kukaa sawa baada ya kipigo kutoka kwa Salim, hakuwaeleza wanaenda wapi bali aliwaambia tu wamfuate. Sasa hivi ndio walijua kuwa wanatakiwa kwenda kwenye hekalu la Mungu Zeus. Kwa mtaalamu wa akiolojia kama Cindy alishituka zaidi kwa maana alifahamu fika ni namna gani suala hilo haliwezekani. Kwa sababu moja Hekalu la Zeus lilikuwepo yapata miaka elfu thalathini iliyopita na pili kwa mujibu wa historia hakuna binadamu ambaye amewahi kukanyaga mguu ndani ya hekalu hilo zaidi ya miungi kumi na mbili ya Kigiriki.
"Hekalu la Zeus!" Cindy alirudia kichwani huku akiongozana na wenzake kumfuata David Logan.
Itaendelea…
*The Bold*
To Infinity and Beyond
Sent using
Jamii Forums mobile app