Mr Acky
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 234
- 313
MTUNZI : AKIDA S. RAMBAO
Contact : 0658328596
email: akidasiri@gmail.com
SEHEMU 1 (A) : JINAMIZI LA SIKITIKO.
Kijiji cha kishanje, Makaburini, Bukoba-Kagera.
Dodoso:
Ni maumivu yanayo ukoroga moyo wake na kuutibua tibua, moyo unatibuka
unachafukwa anajikuta akilia kwa uchungu anatamani abadilishe ukweli uwe uongo
lakini yameshakuwa. Nini kimemkuta, atafanya nini na ataamua nini? Ni ukweli upi huo? Yeye ni nani?
Alibaki kasimama akitazama makaburi manne ya thamani kubwa, yaliyojengwa kwa kufanana na kufatana, akafumba
macho huku akikunja sura kama mtu anayejitahidi kupingana na hali inayomkabili. Punde machozi yakaanza kumtoka aliyaacha yamwagike kwa mfatano huku sauti ya kilio cha chini chini iliyobanwa isitoke ikisikika ikiomboleza kichwa kikinesa nesa kwa uchungu. Mwisho kitambaa kikapita kati ya macho yake na kuyakaushia mbali. Akavuta kamasi lililokuwa likizengea zengea kuchungulia katika tundu ya pua likitaka
kutoka na kukirudisha kitambaa mfukoni.
“Uuuuuuhuu…”
alizishusha pumzi “Nimewamisi sana…baba, mama, dada na kaka Pater…niko mpweke sana” aliongea kwa kuachia achia maneno akijishika kichwa mara kiuno na tena kichwa kana kwamba ni mtu asiyeamini au kuchanganyikiwa.
Mara alijikuta akiishiwa nguvu akayakita magoti ardhini na kuanza kulia kwa sauti kama mtoto. Alilia bwana huyo kwa kupiga nduru kadri alivyoweza huku akitweta jasho likimtoka.
“Kiongozi inatosha utaumwa kichwa unajua, alafu jua ni kali…” ilikuwa ni sauti ya kiume nyuma ya mgongo na mkono ukagusa bega lake kumaanisha, akageuza shingo na kumtazama hasira ikijidhihirisha machoni pake “Lau kama
Ungeliniacha ungelikuwa bora kuliko kuniingilia” aliongea huku sura ikiwa imekunjamana haswa kiasi cha
kumuogopesha aliyemuongelesha mara moja mkono ukatolewa begani mwake na kurudi alipokuwa. “…nakumbuka
mengi sana yaliyopita tukiwa pamoja, zaidi ninachoweza kuwaambia nimekuja kwa kuwa nahitaji Baraka zenu juu ya
kazi ambayo naenda kuifanya naamini itawapa amani huko mlipo na nafsi zenu zitatulia” aliongea kisha akasimama
“Majaliwa nipatie maua yangu tafadhari” aliongea tena, Majaliwa akampatia, huyo akasogea hadi katika kaburi la kwanza “Julius Ebariki Emmanuel Mkwasi” aliyasoma kwa sauti ndogo maneno yaliyoandikwa katika jiwe kubwalililojengwa kichwani mwa kaburi lililonakshiwa kwa Granite muundo huo hujulikana kama Memorial Granite tombstone na kisha akaweka moja ya maua aliyoyakumbatia. Alifanya hivyo
kwa makaburi yaliyosalia akageuka na kuondoka zake.
“Nipatie simu yangu nataka kupiga” aliongea akapandisha mguu baada ya kufunguliwa mlango wa gari kwa heshima.
Baada ya kupatiwa akabonyeza namba zenye usajili wa nchi ya kigeni “Hallow what’s news…will please give him his cash in cash and transport him by Private plane to Tanzania without being denied and make sure he does not escape” aliongea kisha akatabasamu “Majaliwa tuondoke” Gari ikawashwa na kuondoka
Kijiji cha Kyakailabwa, Bukoba-Kagera
“Sijaja hapa kwa ajili ya kupoteza muda Mzee Ishengoma nipo serious nipatie majibu ya maswali yangu tafadhari laa sivyo…” kabla hajamaliza Mzee Ishengoma akadakia “Fanuel mwanangu kwanza umekuja bila taarifa na ukapitiliza katika
makaburi na sasa usiku huu mzito unanishambulia kwa
maneno nikueleze ukweli!? ni ukweli upi kijana wangu unaniweka katika wakati mgumu mbona…” Mzee Ishengoma
alijikuta akishindwa kumalizia kauli yake nakujiinamia akisikitika kwa kichwa “…nimekulea na nimekusomesha na
sasa una wadhifa mkubwa mwanangu hebu tulia achana na
hayo mambo ni mambo makubwa mwanangu” Mzee
Ishengoma aliongea tena, “Mzee hujajibu maswali yangu” aliongea Fanuel Emmanuel sasa sura yake ikiwa imekunjamana kwa hasira akimkodolea kwa macho yaliyotumbuka, “Kijana sikia sitakuwa tayari kwa hilo nilipokusaidia panatosha” aliongea Mzee Ishengoma huku akinyanyuka toka sofani “ooh sawa watu kama nyinyi dawa yenu ndogo sana” aliongea Fanuel na kutoa bunduki ndogo
nyuma ya kiuno aina ya Girsan M1911SC akaifunga kiwambo wakati huo Mzee Ishengoma macho yakiwa yamemtoka
akishuhudia bunduki ikimtazama haraka akanyanyua mikono wasiwasi ukimzidi “Hapana mwa…mwanangu” aliongea Mzee Ishengoma akitetemeka, lakini hakuwa na bahati teyari risasi
ilisharuhusiwa na kukutana na paji la uso wa mzee huyo akiwa kwenye Taharuki mwili ukisikilizia maumivu alifyatuliwa risasi nyingine ya kifua iliyomyumbisha hadi katika sofa alilokuwa amekalia wakati wa mazungumzo, masikini akaacha Mkono.
Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu-Dar es Salam.
Yowe la furaha lilisikika pindi tu Mheshimiwa Jaji bwanaCharles Pascal Kunambi alipoipiga nyundo yake ya haki juu ya meza kusisitiza kile alichokisema awali kisha akanyanyuka
katika kiti chake akiliacha joho pana lililo mzidi kwa wembamba likienda huku na kule akilizuia kwa kulishika
akiwaacha watu wakiwa wamesimama toka kwenye kitiwakitia gumzo za hapa na pale wakishikana mikono wengine
wakitoka kimya kimya huyo. “Hongera sana Richardwasamehe bure ni roho mbaya na wivu wa maendeleo ndio
umetutawala watu wengi na tunakosa ubinadamu” Mzee mmoja aliyekakamaa kwa utuuzima aliongea huku akiwa
kashikilia kiganja cha mkono wa Mheshimiwa Richard
“Asante sana Mzee Boni namshukuru Mungu kwa huruma zake na kumuongoza wakili wangu rafiki yangu bwana
Ferdric Shaka Dodo ambaye alikuwa nami bega kwa bega katika kesi hii” aliongea Richard huku akimshika bega mtu
aliyevalia joho jeusi pembeni yake akitabasamu mkononi akiwa ameshikilia lundo la nyaraka “Ooh vizuri sana kijana
kazi nzuri sana huo ndio urafiki wa kweli haya naondoka” Mzee Boni akauachia mkono huyo akashika njia akipishana na
watu walioendelea kuja kumpa hongera.
“Mheshimiwa… mheshimiwaaa” ilisikika sauti ya kike ikiwa inakuja na kupotea Richard akaacha matembezi ya taratibu aliyoyaanza akiwa karibu kabisa kutoka nje akiongea na Wanahabari
akatulia kidogo akionekana kutegesha masikio “Kuna sauti naisikia kwa mbali” alijisemea “Baada ya madai ya ufujaji wa
mali za Young Trader Company unalipi la kuwaambia wananchi?” hatimaye sauti ilisikika vema na kumfanya Richard kukutanisha macho na mwanahabari akiwa kashikilia kinasa sauti chake akiminyana na watu, akatabasamu
“Naomba utulivu tafadhari” aliongea Mheshimiwa Richard kwa sauti yake ya besi na watu wakatulia “Naomba mumpishe huyo dada asogee karibu ana swali muhimu sana…binti rudia
swali lako tafadhari” aliongea Mheshimiwa Richard na binti akarudia na Mheshimiwa Richard akaanza kujibu huku
akiwaacha wanahabari wakiendelea na jukumu la kuchukua kila kinachowafaa “Kila mtu anapitia changamoto mbalimbali katika maisha yake lakini zote zipo kwa ajili ya kumfanya mtu
akue, nashukuru Mungu nimeshinda kama ilivyo kawaida lazima atokee mshindi na mshindwa, na ninacho weza
kukisema ni kuwa sita rudi nyuma japo biashara zangu zimeathirika kwa kiwango kikubwa na siwezi kuwakasirikia
na nimewasamehe washindani wangu, zaidi ya yote ni kuwa hakuna sehemu iliyoandikwa kuwa ni dhambi kujitafutia cha kwako isitoshe kufanikiwa au kufeli ni jitihada zako, asanteni”
alimaliza Richard na kutoka katika mkusanyiko akifatwa na jamaa zake huku waandishi wa habari wakimfata na maswali lukuki hakujishughulisha nayo akaingia kwenye gari hao wakatimka.
“Unajua mpaka sasa sielewi imekuwaje Richard akashinda hiikesi kwa kishindo jamani tena akiwa na vidhibiti vya kutosha
mbona nashindwa kuelewa hapa” ilisikika Sauti ndani ya chumba cha ofisi mlangoni kukiwa na kibao chenye maandishi
makubwa meusi Ofisi ya Wakili binafsi “Ndugu yangu hata mimi nilibaki mdomo wazi sikutegemea kabisa, wakili hata wewe ulishindwa kuligundua hili? hela zetu zimepotea, alikuwa kila kitu kwetu msimamizi wa kila jambo unajua, akajitoa na mara from no where anakuwa mfanya biashara mkubwa kutuzidi akituacha na madeni na mikopo isiyoeleweka na
bidhaa zilizopitwa na wakati inawezekanaje hili?” “Ndugu
sikia ngoja yameshatokea wacha tujipange upya hakuna atakae skia kilio chetu hapa tumezidiwa kete tumeshajifunza
japo inaumaa” mara mlango ukafunguliwa na wanaume watatu wakatoka wakiwa na nyuso zilizo sawajika,wanahabari waliwaona wakawakimbilia lakini
hawakusikilizwa wakaingia kwenye gari na kuondoka.
Julius K. Nyerere Road, Dar es Salam.
Kimya kilikuwa kimetanda ndani ya gari kila mtu akiwa na lake “Mzee ilikuwaje nikashinda hii kesi kirahisi hivi mihuri
nyaraka kibao, hati miliki, barua sijawahi ziona, taarifa nyingi mpya nimezisikia pale kizimbani zilinishtua ila nilijikaza tu
kama ulivyoniambia, nini kinaendelea hapa?” Richard aliongea “We ni mtu mkubwa bwana, Mheshimiwa Rais
bwana Meza anahitaji kukutana na wewe hayo ndiyo maagizo niliyopewa kwa kweli, maana hata mimi vithibiti nilivyovitoa
mahakamani nililetewa jana home tena na watu nisiowafahamu nikabaki mdomo wazi nani ameziandaa na kwanini ukiniuliza sijui…nakuomba uwe makini naona kuna kitu hakipo sawa mahali au wewe kuna kitu umenificha si
bure au unatakiwa kurudi kazini wanakutafutia sababu”
aliongea Ferdrick huku akiuma meno yake macho yakiwa na wasiwasi Richard akabaki kumtazama akiyapima maneno
aliyoyasikia,Ferdrickakaendelea
“Kingine naonelea uwatafutie pesa kidogo uwape kama shukrani kwa Mungu
maana tulikuwa tunakupoteza ungeshikwa na ndoto zako za biashara na Siasa zingekufa leo kwa kifungo cha miaka ishirini au pesa taslimu, ungezitoa wapi...hata kama tulikuona
ukipambana mengine ni siri yako jaribu kuwapoza na msameheane tu maisha yaendelee pesa zinatafutwa ndugu
yangu” Richard alibaki kumtazama “Na nina wasiwasi na kuvuja kwa siri kuhusu umiliki wa Mzalendo web”
“Inawezekanaje hilo! ni mimi, wewe na Swai tunaojua kuhusu Mzalendo web nani mwingine anaweza kujua bila kuambiwa
na sisi” Richard aliongea kwa wasiwasi “Aah mi nimesema tu haya hayo tuyaache Je, nambie nani unaenda kumuoa kati ya
wale wasichana wawili? Inabidi ufanye maamuzi na tukio mapema” aliongea tena Ferdrick na kumfanya Richardajiinamie huku akiibana midomo yake akalitoa tabasamu la kujilazimisha “Sipo tayari kuingia katika matatizo tenanitatangaza ndoa soon…” Richard akaanza kujisikitikia
akishika kichwa chake machozi yakimlenga lenga. “Maamuzi
mazuri, we ni mwanaume na una bahati hivyo hupaswi kulia utajitia nuksi bure jikaze na usimame kila mmoja akuone,
ujenge na kuziboresha imani za watu upya hilo ndilo jambo la msingi” alidakia Ferdrick
Itaendeleaaaa...wakati ujao
Mijadara inaruhusiwa
Contact : 0658328596
email: akidasiri@gmail.com
SEHEMU 1 (A) : JINAMIZI LA SIKITIKO.
Kijiji cha kishanje, Makaburini, Bukoba-Kagera.
Dodoso:
Ni maumivu yanayo ukoroga moyo wake na kuutibua tibua, moyo unatibuka
unachafukwa anajikuta akilia kwa uchungu anatamani abadilishe ukweli uwe uongo
lakini yameshakuwa. Nini kimemkuta, atafanya nini na ataamua nini? Ni ukweli upi huo? Yeye ni nani?
Alibaki kasimama akitazama makaburi manne ya thamani kubwa, yaliyojengwa kwa kufanana na kufatana, akafumba
macho huku akikunja sura kama mtu anayejitahidi kupingana na hali inayomkabili. Punde machozi yakaanza kumtoka aliyaacha yamwagike kwa mfatano huku sauti ya kilio cha chini chini iliyobanwa isitoke ikisikika ikiomboleza kichwa kikinesa nesa kwa uchungu. Mwisho kitambaa kikapita kati ya macho yake na kuyakaushia mbali. Akavuta kamasi lililokuwa likizengea zengea kuchungulia katika tundu ya pua likitaka
kutoka na kukirudisha kitambaa mfukoni.
“Uuuuuuhuu…”
alizishusha pumzi “Nimewamisi sana…baba, mama, dada na kaka Pater…niko mpweke sana” aliongea kwa kuachia achia maneno akijishika kichwa mara kiuno na tena kichwa kana kwamba ni mtu asiyeamini au kuchanganyikiwa.
Mara alijikuta akiishiwa nguvu akayakita magoti ardhini na kuanza kulia kwa sauti kama mtoto. Alilia bwana huyo kwa kupiga nduru kadri alivyoweza huku akitweta jasho likimtoka.
“Kiongozi inatosha utaumwa kichwa unajua, alafu jua ni kali…” ilikuwa ni sauti ya kiume nyuma ya mgongo na mkono ukagusa bega lake kumaanisha, akageuza shingo na kumtazama hasira ikijidhihirisha machoni pake “Lau kama
Ungeliniacha ungelikuwa bora kuliko kuniingilia” aliongea huku sura ikiwa imekunjamana haswa kiasi cha
kumuogopesha aliyemuongelesha mara moja mkono ukatolewa begani mwake na kurudi alipokuwa. “…nakumbuka
mengi sana yaliyopita tukiwa pamoja, zaidi ninachoweza kuwaambia nimekuja kwa kuwa nahitaji Baraka zenu juu ya
kazi ambayo naenda kuifanya naamini itawapa amani huko mlipo na nafsi zenu zitatulia” aliongea kisha akasimama
“Majaliwa nipatie maua yangu tafadhari” aliongea tena, Majaliwa akampatia, huyo akasogea hadi katika kaburi la kwanza “Julius Ebariki Emmanuel Mkwasi” aliyasoma kwa sauti ndogo maneno yaliyoandikwa katika jiwe kubwalililojengwa kichwani mwa kaburi lililonakshiwa kwa Granite muundo huo hujulikana kama Memorial Granite tombstone na kisha akaweka moja ya maua aliyoyakumbatia. Alifanya hivyo
kwa makaburi yaliyosalia akageuka na kuondoka zake.
“Nipatie simu yangu nataka kupiga” aliongea akapandisha mguu baada ya kufunguliwa mlango wa gari kwa heshima.
Baada ya kupatiwa akabonyeza namba zenye usajili wa nchi ya kigeni “Hallow what’s news…will please give him his cash in cash and transport him by Private plane to Tanzania without being denied and make sure he does not escape” aliongea kisha akatabasamu “Majaliwa tuondoke” Gari ikawashwa na kuondoka
Kijiji cha Kyakailabwa, Bukoba-Kagera
“Sijaja hapa kwa ajili ya kupoteza muda Mzee Ishengoma nipo serious nipatie majibu ya maswali yangu tafadhari laa sivyo…” kabla hajamaliza Mzee Ishengoma akadakia “Fanuel mwanangu kwanza umekuja bila taarifa na ukapitiliza katika
makaburi na sasa usiku huu mzito unanishambulia kwa
maneno nikueleze ukweli!? ni ukweli upi kijana wangu unaniweka katika wakati mgumu mbona…” Mzee Ishengoma
alijikuta akishindwa kumalizia kauli yake nakujiinamia akisikitika kwa kichwa “…nimekulea na nimekusomesha na
sasa una wadhifa mkubwa mwanangu hebu tulia achana na
hayo mambo ni mambo makubwa mwanangu” Mzee
Ishengoma aliongea tena, “Mzee hujajibu maswali yangu” aliongea Fanuel Emmanuel sasa sura yake ikiwa imekunjamana kwa hasira akimkodolea kwa macho yaliyotumbuka, “Kijana sikia sitakuwa tayari kwa hilo nilipokusaidia panatosha” aliongea Mzee Ishengoma huku akinyanyuka toka sofani “ooh sawa watu kama nyinyi dawa yenu ndogo sana” aliongea Fanuel na kutoa bunduki ndogo
nyuma ya kiuno aina ya Girsan M1911SC akaifunga kiwambo wakati huo Mzee Ishengoma macho yakiwa yamemtoka
akishuhudia bunduki ikimtazama haraka akanyanyua mikono wasiwasi ukimzidi “Hapana mwa…mwanangu” aliongea Mzee Ishengoma akitetemeka, lakini hakuwa na bahati teyari risasi
ilisharuhusiwa na kukutana na paji la uso wa mzee huyo akiwa kwenye Taharuki mwili ukisikilizia maumivu alifyatuliwa risasi nyingine ya kifua iliyomyumbisha hadi katika sofa alilokuwa amekalia wakati wa mazungumzo, masikini akaacha Mkono.
Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu-Dar es Salam.
Yowe la furaha lilisikika pindi tu Mheshimiwa Jaji bwanaCharles Pascal Kunambi alipoipiga nyundo yake ya haki juu ya meza kusisitiza kile alichokisema awali kisha akanyanyuka
katika kiti chake akiliacha joho pana lililo mzidi kwa wembamba likienda huku na kule akilizuia kwa kulishika
akiwaacha watu wakiwa wamesimama toka kwenye kitiwakitia gumzo za hapa na pale wakishikana mikono wengine
wakitoka kimya kimya huyo. “Hongera sana Richardwasamehe bure ni roho mbaya na wivu wa maendeleo ndio
umetutawala watu wengi na tunakosa ubinadamu” Mzee mmoja aliyekakamaa kwa utuuzima aliongea huku akiwa
kashikilia kiganja cha mkono wa Mheshimiwa Richard
“Asante sana Mzee Boni namshukuru Mungu kwa huruma zake na kumuongoza wakili wangu rafiki yangu bwana
Ferdric Shaka Dodo ambaye alikuwa nami bega kwa bega katika kesi hii” aliongea Richard huku akimshika bega mtu
aliyevalia joho jeusi pembeni yake akitabasamu mkononi akiwa ameshikilia lundo la nyaraka “Ooh vizuri sana kijana
kazi nzuri sana huo ndio urafiki wa kweli haya naondoka” Mzee Boni akauachia mkono huyo akashika njia akipishana na
watu walioendelea kuja kumpa hongera.
“Mheshimiwa… mheshimiwaaa” ilisikika sauti ya kike ikiwa inakuja na kupotea Richard akaacha matembezi ya taratibu aliyoyaanza akiwa karibu kabisa kutoka nje akiongea na Wanahabari
akatulia kidogo akionekana kutegesha masikio “Kuna sauti naisikia kwa mbali” alijisemea “Baada ya madai ya ufujaji wa
mali za Young Trader Company unalipi la kuwaambia wananchi?” hatimaye sauti ilisikika vema na kumfanya Richard kukutanisha macho na mwanahabari akiwa kashikilia kinasa sauti chake akiminyana na watu, akatabasamu
“Naomba utulivu tafadhari” aliongea Mheshimiwa Richard kwa sauti yake ya besi na watu wakatulia “Naomba mumpishe huyo dada asogee karibu ana swali muhimu sana…binti rudia
swali lako tafadhari” aliongea Mheshimiwa Richard na binti akarudia na Mheshimiwa Richard akaanza kujibu huku
akiwaacha wanahabari wakiendelea na jukumu la kuchukua kila kinachowafaa “Kila mtu anapitia changamoto mbalimbali katika maisha yake lakini zote zipo kwa ajili ya kumfanya mtu
akue, nashukuru Mungu nimeshinda kama ilivyo kawaida lazima atokee mshindi na mshindwa, na ninacho weza
kukisema ni kuwa sita rudi nyuma japo biashara zangu zimeathirika kwa kiwango kikubwa na siwezi kuwakasirikia
na nimewasamehe washindani wangu, zaidi ya yote ni kuwa hakuna sehemu iliyoandikwa kuwa ni dhambi kujitafutia cha kwako isitoshe kufanikiwa au kufeli ni jitihada zako, asanteni”
alimaliza Richard na kutoka katika mkusanyiko akifatwa na jamaa zake huku waandishi wa habari wakimfata na maswali lukuki hakujishughulisha nayo akaingia kwenye gari hao wakatimka.
“Unajua mpaka sasa sielewi imekuwaje Richard akashinda hiikesi kwa kishindo jamani tena akiwa na vidhibiti vya kutosha
mbona nashindwa kuelewa hapa” ilisikika Sauti ndani ya chumba cha ofisi mlangoni kukiwa na kibao chenye maandishi
makubwa meusi Ofisi ya Wakili binafsi “Ndugu yangu hata mimi nilibaki mdomo wazi sikutegemea kabisa, wakili hata wewe ulishindwa kuligundua hili? hela zetu zimepotea, alikuwa kila kitu kwetu msimamizi wa kila jambo unajua, akajitoa na mara from no where anakuwa mfanya biashara mkubwa kutuzidi akituacha na madeni na mikopo isiyoeleweka na
bidhaa zilizopitwa na wakati inawezekanaje hili?” “Ndugu
sikia ngoja yameshatokea wacha tujipange upya hakuna atakae skia kilio chetu hapa tumezidiwa kete tumeshajifunza
japo inaumaa” mara mlango ukafunguliwa na wanaume watatu wakatoka wakiwa na nyuso zilizo sawajika,wanahabari waliwaona wakawakimbilia lakini
hawakusikilizwa wakaingia kwenye gari na kuondoka.
Julius K. Nyerere Road, Dar es Salam.
Kimya kilikuwa kimetanda ndani ya gari kila mtu akiwa na lake “Mzee ilikuwaje nikashinda hii kesi kirahisi hivi mihuri
nyaraka kibao, hati miliki, barua sijawahi ziona, taarifa nyingi mpya nimezisikia pale kizimbani zilinishtua ila nilijikaza tu
kama ulivyoniambia, nini kinaendelea hapa?” Richard aliongea “We ni mtu mkubwa bwana, Mheshimiwa Rais
bwana Meza anahitaji kukutana na wewe hayo ndiyo maagizo niliyopewa kwa kweli, maana hata mimi vithibiti nilivyovitoa
mahakamani nililetewa jana home tena na watu nisiowafahamu nikabaki mdomo wazi nani ameziandaa na kwanini ukiniuliza sijui…nakuomba uwe makini naona kuna kitu hakipo sawa mahali au wewe kuna kitu umenificha si
bure au unatakiwa kurudi kazini wanakutafutia sababu”
aliongea Ferdrick huku akiuma meno yake macho yakiwa na wasiwasi Richard akabaki kumtazama akiyapima maneno
aliyoyasikia,Ferdrickakaendelea
“Kingine naonelea uwatafutie pesa kidogo uwape kama shukrani kwa Mungu
maana tulikuwa tunakupoteza ungeshikwa na ndoto zako za biashara na Siasa zingekufa leo kwa kifungo cha miaka ishirini au pesa taslimu, ungezitoa wapi...hata kama tulikuona
ukipambana mengine ni siri yako jaribu kuwapoza na msameheane tu maisha yaendelee pesa zinatafutwa ndugu
yangu” Richard alibaki kumtazama “Na nina wasiwasi na kuvuja kwa siri kuhusu umiliki wa Mzalendo web”
“Inawezekanaje hilo! ni mimi, wewe na Swai tunaojua kuhusu Mzalendo web nani mwingine anaweza kujua bila kuambiwa
na sisi” Richard aliongea kwa wasiwasi “Aah mi nimesema tu haya hayo tuyaache Je, nambie nani unaenda kumuoa kati ya
wale wasichana wawili? Inabidi ufanye maamuzi na tukio mapema” aliongea tena Ferdrick na kumfanya Richardajiinamie huku akiibana midomo yake akalitoa tabasamu la kujilazimisha “Sipo tayari kuingia katika matatizo tenanitatangaza ndoa soon…” Richard akaanza kujisikitikia
akishika kichwa chake machozi yakimlenga lenga. “Maamuzi
mazuri, we ni mwanaume na una bahati hivyo hupaswi kulia utajitia nuksi bure jikaze na usimame kila mmoja akuone,
ujenge na kuziboresha imani za watu upya hilo ndilo jambo la msingi” alidakia Ferdrick
Itaendeleaaaa...wakati ujao
Mijadara inaruhusiwa