The Engineers tafadhali msaada wa haraka

Kama unakiwanja anza kujenga, hiyo pesa itakapoishia utapumzika uvute nguvu kidogo uanze tena. Lakini ukitaka ushauri wa watu wengi mwishowe watakukatisha tamaa, watakupigia mahesabu ya juu mpaka hiyo pesa utaitumia, uchungu wa kujenga utauhisi unapoanza, na raha yake ni pale inapokua imenyanyuka kidogo, hata pesa ikiisha utafanya juu chini ili umalizie. Kila la kheri mkuu nijambo jema sana umeamua.
 
 
acha kumpotosha mwenzako wewe,,, ni dhambi ya mauti

Mkuu Architect I kno its ur pro lkn kwa sis waswazi kum-hire akitect ni ngumu labda mafisadi,mkuu tembelea morogoro/mbeya uone m2 anajenga nyumba nzuri kwa mil 3.5 Kiwanja sehemu nzuri iliyochangamka unaweza ukapata kwa laki 2,simpotoshi hata kidogo:::Hyo mil 5 akinipa niisimamie namuingizia hadi umeme,yeye ni kuamia tu.Me mwenyewe najenga so I kno everythin kibongo bongo
 

Aseee......
 

Huwezi kuwa siriaz mkuu....5m? Hadi umeme????
Ufundi wote 400k???
Matofali 5000???
Sementi mifuko 25???
Labda usaidiane na kina mwingira waweke na miujiza yao.....
 
Kwa mtindo huu na mahesabu haya, kila mtu lazima atajenga wallah!
 


Mkuu,
Mtu anapoomba ushauri anahitaji msaada. Usimpotoshe. Its better you tell him/her the truth halafu aamue. Wewe unamdanganya mwenzio. Na ki ukweli ni bora ungekaa kimya. I'm an Engineer who have been ni this industry for more than six yrs. Nakubaliana kabisa na Architect. Hiyo hela ni ndogo sana kwa aina ya nyumba anaxotaka. Hata msingi sidhani kama utamalizika. Bei ya tofali, cement, mchanga, kokoto, ufundi for 3bedroom self containing housi, nakuhakikishia hata msingi haumaliziki!
 
Habar zenyu wana jf nakuombeni msaada wa haraka tafadhalini! Ninataka kuanza ujenzi wa nyumba ya kawaida self ya room 3 nina shilingi mil.5 tofali nitatumia za kuchoma! Nawasilisha

5 M hardly unaweza kuishia kwenye Msingi tu
 

in red, nina jamaa yangu huwa ananiambiaga huwezi kufikiria kujenga wakati huna kiwanja...
nakuunga mkono umeweka ushauri mzuri, kibongo bongo ni wachache mno wanaoanza ujenzi na kumaliza bila kusimama...
wengi wetu tunakwenda kwa hatua, hivyo basi ukiwa na kiwanja inakuwa rahisi kwako kujenga koz kila pesa utakayoingiza utakuwa unafikiria ufanye nini kwenye kiwanja chako!
mkuu naomba ufanyie kazi wazo lako, anza ujenzi taratibu utafanikiwa...
 

mkuu nakubaliana na wewe hapo kwenye red...
lakini kwa pesa hiyo, kama ana kiwanja anaweza kufanya kitu ambacho atakapoishia atakuja kuendeleza atakaposhika pesa nyingine...
kwa gharama za ujenzi jinsi zilivyo ukianza kuzipigia hesabu huwezi jenga, koz kukamata l/s ya kukamilisha ujenzi wengi wetu ni ishu...
hivyo tumshauri aanze, hata akiishia kwenye msingi atakuja aendeleze ujenzi pindi atakaposhika pesa tena na mwisho wa siku atajikuta amemaliza ujenzi huo...(wangu mtazamo)
 
Simple calculation
450,000/- per square metre of building
3 bedroom house is approx. 120 sqm
thats give 54,000,000/
Including evrything unaingia tu
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…