Serikali moja inawezekana endapo mfumo wa wenye dunia yao yaani mataifa yenye nguvu yatakubaliana nao.
Changamoto kubwa ni wanasiasa, je watakubali kunyang'anywa ulaji na ile pride ya mimi ndiye rais au mfalme wa nchi hii then wakubali kuwa sawa na magavana?
Wananchi siku zote hawanaga noma maana utawaliwa na hawa wanaowazid akili yaani wanasiasa so hata likija hili la serikali moja ya dunia propaganda sikishaenezwa, wananchi watapangwa na wataeleweka.
Swali ni je, uwepo wa serikali ya namna hii ni strength na suluhisho la matatizo tuliyonayo au ni majanga matupu bora na tulivyo sasa.
1. Je, serikali hiyo itaweza kumaintain amani ya dunia kuliko ilivyo sasa?
2. Je, serikali hiyo itaweza kufutilia mbali kabisa umasikini nakuondosha matabaka?
3. Je, serikali hiyo itadumisha usawa kati ya nchi zote pasipo kupendelea upande wowote kati ya mataifa yale tajiri zaidi na maskini?
4. Je, serikali hiyo itaweza hakikisha inathibiti uzalishaji wa silaha za maangamizi na kuwajibika kikamilifu kwa dosari zake?
5. Je, serikali hiyo itawajibishwa na chombo kipi endapo ikienda ndivyo sivyo?
6. Je, itatumia muundo upi kuongoza watu ambao hauna dosari?
7. Ikiwa sasa hivi chanjo ya corona tunalazimishana, viwanda vimekuwa kero kwenye athari za kimazingira na tabia ya nchi au waamiaji toka Afrika na Asia wanawekewa vizuizi wasiingie Europe, je siku wakitawala wao kwa asilimia 100% maamuzi yao yataiathiri vipi dunia?
8. Kwa miaka yote dunia imeendelea sababu ya ushindani, sasa tukiondoa nchi tukazibadilisha kuwa na cheo cha mikoa/states, je uhakika wa maendeleo upo au yale yale tu kama tulivyo sasa?
9. Je, usalama, uhuru, usawa, haki, maamuzi ya haraka,kuheshimu imani za watu wote na tamaduni zao utadumishwa kwenye nyanja zote za kijamii na kiuchumi ikiwemo biashara?
Mfano; Leo wewe ni mfanyabiashara umekuja bongo tumezingua unaondoka na kutafuta eneo lingine kuwekeza, pata picha ni serikali hiyo hiyo hata kama imekuminya hapa hamna pa kuchomokea hata uende wapi.
10. Je, serikali hiyo itaruhusu upinzani? Vp ikitokea waliopo madarakani wakagoma kutoka nani atawaondoa? Na kama ni jeshi la dunia limepindua uongozi wa dunia nani atawachomoa?
11. Je, serikali hiyo ikiamua kuingilia uhuru wetu wa maamuzi,afya,faragha,imani,n.k au kutuongoza kidikteta au ukatokea mpasuko wa kisiasa ndani ya serikali hiyo moja nini hatima yake?
12. Je, utawala huo utatofautiana vipi na tawala zakishenzi zilizopita kama ajemi,mesopotamia,rumi na nyinginezo ambazo licha ya kutawala dunia ziliishia kulipisha kodi kubwa, kuishi luxury, kupendelea mabara yao na kudumisha ubaguzi wa rangi,utamaduni mpaka imani?
Kiufupi kuna maswali mengi nahisi yanapaswa kujibiwa kabla ya kuunga sera ya serikali moja ambayo badala ya kuwa na faida inaweza ishia kuwa jehanamu kwa dunia yetu.