PreGE2025 The Chanzo yaondoa Maudhui ya Askofu Gwajima YouTube Kufuatia wito wa TCRA

PreGE2025 The Chanzo yaondoa Maudhui ya Askofu Gwajima YouTube Kufuatia wito wa TCRA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Leo Mei 27, 2025, The Chanzo imepokea wito kutoka kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuhusu maudhui ya video tuliyochapisha katika chaneli yetu ya Youtube, ambayo ni mkutano na waandishi wa habari mazungumzo aliyoyafanya Askofu Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe (Chama cha Mapinduzi - CCM), mnamo Mei 24, 2025.

Kutokana na mazungumzo hayo kuendelea kufuatiliwa, ili kuboresha uwazi, na imani ya wafuatiliaji wetu, The Chanzo inapenda kuwajulisha wasomaji na wadau wake wengine kuwa imetubidi kuyaondoa maudhui hayo kutokana na wito huo.

Sehemu ya taarifa tuliyopokea kutoka TCRA inaeleza:

"Maudhui hayo yaliyopakiwa na Chanzo Online TV yalikuwa ni maelezo ya mtu aliyejitambulisha kwa jina la Josephat Gwajima, hayakufuata Sheria, Kanuni, Maadili wala Misingi ya Uandishi na Utangazaji wa Habari kutokana na kukosa mizania/kuwa na taarifa za upande mmoja tu bila ya kuwapa nafasi upande wa Serikali au Mamlaka husika kutolea ufafanuzi shutuma au taarifa kuhusu idadi ya watu waliodaiwa kutekwa kama ilivyodaiwa katika taarifa husika. Kitendo cha Chanzo Online TV kupakia taarifa zenye kuegemea upande mmoja kinaweza kuhamasisha au kuchochea chuki dhidi ya Serikali kutoka kwa wananchi wake."

Wakati ni nadra wito wa namna hii kutokea, kutokana na wito huu kutoka TCRA, leseni ya maudhui inatutaka kuyaondoa maudhui hayo; jambo ambalo tumelifanya leo Mei 27, 2025, 10:09 asubuhi.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

1748330422028.png

 
Leo Mei 27, 2025, The Chanzo imepomea wito kutoka kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuhusu maudhui ya video tuliyochapisha katika chaneli yetu ya Youtube, ambayo ni mkutano na waandishi wa habari mazungumzo aliyoyafanya Askofu Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe (Chama cha Mapinduzi - CCM), mnamo Mei 24, 2025.

Kutokana na mazungumzo hayo kuendelea kufuatiliwa, ili kuboresha uwazi, na imani ya wafuatiliaji wetu, The Chanzo inapenda kuwajulisha wasomaji na wadau wake wengine kuwa imetubidi kuyaondoa maudhui hayo kutokana na wito huo.

Sehemu ya taarifa tuliyopokea kutoka TCRA inaeleza:

"Maudhui hayo yaliyopakiwa na Chanzo Online TV yalikuwa ni maelezo ya mtu aliyejitambulisha kwa jina la Josephat Gwajima, hayakufuata Sheria, Kanuni, Maadili wala Misingi ya Uandishi na Utangazaji wa Habari kutokana na kukosa mizania/kuwa na taarifa za upande mmoja tu bila ya kuwapa nafasi upande wa Serikali au Mamlaka husika kutolea ufafanuzi shutuma au taarifa kuhusu idadi ya watu waliodaiwa kutekwa kama ilivyodaiwa katika taarifa husika. Kitendo cha Chanzo Online TV kupakia taarifa zenye kuegemea upande mmoja kinaweza kuhamasisha au kuchochea chuki dhidi ya Serikali kutoka kwa wananchi wake."

Wakati ni nadra wito wa namna hii kutokea, kutokana na wito huu kutoka TCRA, leseni ya maudhui inatutaka kuyaondoa maudhui hayo; jambo ambalo tumelifanya leo Mei 27, 2025, 10:09 asubuhi.

20250527_101402.jpg
 
Leo Mei 27, 2025, The Chanzo imepokea wito kutoka kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuhusu maudhui ya video tuliyochapisha katika chaneli yetu ya Youtube, ambayo ni mkutano na waandishi wa habari mazungumzo aliyoyafanya Askofu Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe (Chama cha Mapinduzi - CCM), mnamo Mei 24, 2025.

Kutokana na mazungumzo hayo kuendelea kufuatiliwa, ili kuboresha uwazi, na imani ya wafuatiliaji wetu, The Chanzo inapenda kuwajulisha wasomaji na wadau wake wengine kuwa imetubidi kuyaondoa maudhui hayo kutokana na wito huo.

Sehemu ya taarifa tuliyopokea kutoka TCRA inaeleza:

"Maudhui hayo yaliyopakiwa na Chanzo Online TV yalikuwa ni maelezo ya mtu aliyejitambulisha kwa jina la Josephat Gwajima, hayakufuata Sheria, Kanuni, Maadili wala Misingi ya Uandishi na Utangazaji wa Habari kutokana na kukosa mizania/kuwa na taarifa za upande mmoja tu bila ya kuwapa nafasi upande wa Serikali au Mamlaka husika kutolea ufafanuzi shutuma au taarifa kuhusu idadi ya watu waliodaiwa kutekwa kama ilivyodaiwa katika taarifa husika. Kitendo cha Chanzo Online TV kupakia taarifa zenye kuegemea upande mmoja kinaweza kuhamasisha au kuchochea chuki dhidi ya Serikali kutoka kwa wananchi wake."

Wakati ni nadra wito wa namna hii kutokea, kutokana na wito huu kutoka TCRA, leseni ya maudhui inatutaka kuyaondoa maudhui hayo; jambo ambalo tumelifanya leo Mei 27, 2025, 10:09 asubuhi.

View attachment 3347334
Samia amekuwa muoga kupindukia........Huyu mtu anaajenda ovu sana na Tanganyika yetu
 
Tumeisave hiyo press kwenye simu zetu tutatumiana WhatsApp😆😆,mwaka huu analo tutaenda nae Saco to Baco
 
Babeki zao wote hao, kodi zetu ndiyo wanakula mishahara minono. Mnajua wananchi wa Tz tunachezewa kama kitenesi. Huku tuitwe kenge wa ndani, anayetuita hivyo, anakula na kulala kwa kodi zetu.

Huku tunazuiwa kupata habari, kisa viongozi hawataki wao kusikia hayo maudhui. Kwani hii nchi ni ya viongozi peke yao? Wasituletee usengerema wao, hiyo press imesambaa karibu kwa kila mtu, wamezoea kuuwa haya muueni na Gwajima sasa.

Hamna haya, mko hapo kwa hisani ya wananchi, kodi zetu badala ya kufanya kilichowapeleka mnajifanya Serikali kama ya familia zenu. Hakuna mtu mjinga miaka yote, huyo unayemuona mjinga leo, siku akijanjaruka hakuna rangi mtaacha kuziona. Nimekwazika haki...
 
Ninayo kwenye simu yangu sasa nafanyeje, nisiisikilize tena, maudhui yake kwani yanatatizo gani au mshono umeanza kuaachia na maumivu yameanza kuwa makali
 
Back
Top Bottom