Thanx God....17 yrs...Still getting stronger

We Gaga usinifundishe tabia mbaya mke wa mtu hapana tupendane kwenye keyboard sweety lol! Nawavulia kofia we na mumeo mi nimejaribu mara mbili na kuachana na wote niko sokoni lol!
Kweli kabisa mke wa mtu sumu, sasa swt mara mbili zote hizo jamani?? ilikuwaje? ni wewe mgomvi au hao wakezo?
 
Kweli kabisa mke wa mtu sumu, sasa swt mara mbili zote hizo jamani?? ilikuwaje? ni wewe mgomvi au hao wakezo?
Yaani we acha tu,wote mambo yangu yalipokuwa ovyo wakanikimbia,mmoja baada ya mambo kurudi kwenye mstari eti alitaka kurudi nikamwambia hapana,wakina Gaga ni nadra mujini kuwapata.
 
hongera sana dada....May God strengthen u n help u to kip him as ur first priority......God bless ur marriage...amen
 
Incredible! Hongera sana Gaga. Tokea mwaka 1994 ni mbali sana. Mara nyingi tumekuwa tukisoma vilio vya walio kwenye mahusiano hapa MMU, lakini anniversary yako itakuwa inspirational kwa watu wengi. Ni sawa na kusema, pamoja na misukosuko ya hapa na pale, YES WE CAN. Kwa kawaida zawadi ya anniversary ya kutimiza miaka 17 ya ndoa ni funiture. Ngoja basi tumalizie kutengeneza hii funiture kwa jina "Madame Dakar" toka Senegal fast fasta tutaishusha hapo home within minutes. Hongereni sana and God bless you all.

the-making-of-madame-dakar-by-bibi-seck-and-ayse-birse.jpg
 
Hi marafiki, wanajamii wenzangu, siwezi amini miaka inavokatika, nikiangalia naona kama ni juzijuzi tu, sijui wakati umeenda wapi, all in all namshukuru Mwenyezi Mungu sana sana kwani leo ni anniversary yetu na my hubby, namshukuru Mume wangu pia kwa kunichagua mimi kuwa mke wake, nawashukuru pia watoto wangu kwa kunipa sababu nyingine ya kuishi, nawapenda sana hawa watu walio katika maisha yangu. Our anniversary is a time to look back at the good times and to look ahead to live our dream...below is my story.. Nikirudi nyuma kabisa nakumbuka nikiwa msichana mdogo na kabegi kangu ka shule nakutana na huyu mkaka aliyehamia mtaani kwetu, na kupanga chumba nyumba ya jirani baada ya kumaliza masomo ya chuo, utani uleeee wa kizamani ukaanza, oooh mchumba, oooh hakuna shule hapo, oooh sijui nini badae nikaja kugundua huyu jamaa ananizimia, mwisho wa siku akaniambia ukweli wake, niliogopa sana...ukizingatia alikuwa mkubwa kuliko mimi. Moyoni nilikuwa na mawazo sana hasa wasichana wengi wanajua kipindi ambapo wanafanya maamuzi ya kuwa na BF wa kwanza kabisa, nikammwaga,nilihisi bado wakati na siwezi kuwa na uhusiano na mkaka mkubwa,miezi ikaendelea, mara tunakutana dukani, mara kwenye chips mtaani.....miezi inaendelea...hatimae mwaka....jamaa kawa stable kidogo kazini anataka kuhamia chumba kingine eneo lingine kabisa, hapo ndio kimbembe kilianza Jioni moja kaniita kanambia anahama keshapata chumba mahala pengine, na alipohama ndipo nilianza ku mmiss mpaka nikaumwa kabisa, kumbuka kipindi cha miaka ya tisini na hivi simu ilikuwa ni ishu, mawasiliano ni mpaka umtafute mtu, na wakunitafuta ni yeye coz mie alipohama nilijifanya sitaki kujua anahamia wapi,muda ukapita ila jamaa hakukata tamaa, akarudi siku moja mtaani nilipomwona mpaka machozi yalinitoka....... hapa ndio ule msemo wa "huwezi jua thamani ya kitu mpaka ukipoteze ndipo ulifika mahala pake"........kiss ya kwanza bonde la mchicha loooooooooo.....jamaa hakuamini... baada ya muda mfupi uhusiano ukaanza... "Love for me is to trust yourself that your in love....thats what happened to me, pamoja nilikuwa mdogo ila nilijua kabisa huyu mwanaume nimempenda kwa dhati,love is trusting your partner enough to tell them everything about yourself,ukijumlisha na yale yooote you might be ashamed of, Love is feeling comfortable and safe with someone........thats what i felt when im around him Basi rafiki zangu, maisha yakaenda nikamaliza shule yaaani O level nikaolewa mwenzenu loooo.... yaliyofata kutokea hapo ni rahaaaaaaaaaa, uchungu ......rahaaaaaaaaaaaaa uchungu....... na sasa ndio raha kamili kila mahali....ndoa zina changamoto nyingi sana ni namna unavoichukulia wewe ndio itakuwa hivohivo, ndoa ni tamu asikwambie mtu, hata kama ni ndoano, ila ndoano yake ni ya aina ya pekee...Nampenda sana Mume wangu mpenzi, Naendelea kuomba Mungu atupe afya mie na familia yangu, kwa maisha yetu yote, atulinde na mabaya yote, azidi kutupa nguvu na amani ndani ya ndoa yetu.......Ndoa yetu na iheshimiwe na watu wote,,,,AMIN
Gaga unanipa hamu ya kuoa
 
Yaani we acha tu,wote mambo yangu yalipokuwa ovyo wakanikimbia,mmoja baada ya mambo kurudi kwenye mstari eti alitaka kurudi nikamwambia hapana,wakina Gaga ni nadra mujini kuwapata.
duh pole sana, hawajui mwanaume ukimvumilia kwenye shida akija kupata anakufanya kama malkia vile, anakumbuka mlipotoka, mie nakumbuka kuna u ethiopia ulitupitia huwezi amini hadi pesa ya kula ilikuwa ni taabu..lakini sikukata tamaa na kumpa moyo mpaka mambo yalipokuwa mazur...kwa kweli uvumilivu huwa una play part kubwa sana kwenye ndoa...ila usikate tamaa inawezekana Mungu hakukuandikia hao watu uwe nao, ila ulilazimishia,utapata tu mke wako atakaekuvumilia kwenye shida na raha
 
Incredible! Hongera sana Gaga. Tokea mwaka 1994 ni mbali sana. Mara nyingi tumekuwa tukisoma vilio vya walio kwenye mahusiano hapa MMU, lakini anniversary yako itakuwa inspirational kwa watu wengi. Ni sawa na kusema, pamoja na misukosuko ya hapa na pale, YES WE CAN. Kwa kawaida zawadi ya anniversary ya kutimiza miaka 17 ya ndoa ni funiture. Ngoja basi tumalizie kutengeneza hii funiture kwa jina "Madame Dakar" toka Senegal fast fasta tutaishusha hapo home within minutes. Hongereni sana and God bless you all.

the-making-of-madame-dakar-by-bibi-seck-and-ayse-birse.jpg
Hahahahahaaahaha, EMT thanx for the furniture, yaani naisubiria kwahamu, kwa kweli miaka imekatika bila hata kujua, machungu yapo tu ila nashukuru Mungu unakuwa unajua namna ya kuya handle..... hakuna ndoa inayoenda tu smooothly, mara nyingi lazima yanatokea kutokubaliana na mabishano ya hapa na pale, ila yakiisha mnasahau na kuendelea na maisha..ahsante sana EMT naisubiria zawadi yangu
 
Aaaaaaaa gagaaaaaa, nazidi kukupenda my sis, kwa kweli mapenzi ya dhati ni kuvumiliana, umemvumilia. Mapenzi ya dhati ni kujua kila kitu kuhusu mtu fulani na kutaka kuwa nae hivohivo alvo kutoka moyoni, umefanya pia. Mapenzi ya kweli ni kumwamini sana mtu na kumkabidhi kila kitu chako akishikilie mkononi bil kuwaza kama atakuumiza au vipi, Umefanya pi. Heshima kwa mwenzako pia ni jambo labusara sana sio kutoheshimiana na kuadhiriana mbele ya jamii nzima....Mungu awazidishie upendo wenu, uwe kama ule ulioandikwa kwenye vitabu vya dini, mpendane kwa dhati nawaombea maisha marefu yenye kila aina ya raha na mafanikio,mbarikiwe sana, ahsante kwa ku shea na sisi
 
Duh! Yaani hii sredi imenifanya ni-log in ili nikupe ma-congrats wewe na my husband wako! Halafu umenitia moyo kweli... Kumbe yule bidada nayefukuzia niongeze bidii, au nikiona vipi nahama mtaa ili animiss!! Ha ha haaa!! Hongereni sana na kila la heri.
 
18 + 17= 35..........Being 35 and having 17 yrs in marriage sio mchezo aisee, yaani nahisi bado una miaka mingi tu inakuja, maana kwa umri wako mdogo na uzoefu ulio nao kwa kweli una hitaji pongezi Gaga, ndio maana una mabusara sana Mungu akupe nguvu na akuzidishie upendo juu ya mme wako na familia kwa ujumla, wako wasichana wenye umri kama wako na bado wameshikilia mchuma wanasubiria kiti wakae.....duh sikutegemea aisee nashukuru sana kwa story nzuri gaga ila nina maswali nitakuuliza PM....umri ulioanza kunanihii
 
Aaaaaaaa gagaaaaaa, nazidi kukupenda my sis, kwa kweli mapenzi ya dhati ni kuvumiliana, umemvumilia. Mapenzi ya dhati ni kujua kila kitu kuhusu mtu fulani na kutaka kuwa nae hivohivo alvo kutoka moyoni, umefanya pia. Mapenzi ya kweli ni kumwamini sana mtu na kumkabidhi kila kitu chako akishikilie mkononi bil kuwaza kama atakuumiza au vipi, Umefanya pi. Heshima kwa mwenzako pia ni jambo labusara sana sio kutoheshimiana na kuadhiriana mbele ya jamii nzima....Mungu awazidishie upendo wenu, uwe kama ule ulioandikwa kwenye vitabu vya dini, mpendane kwa dhati nawaombea maisha marefu yenye kila aina ya raha na mafanikio,mbarikiwe sana, ahsante kwa ku shea na sisi
Daaa umenifanya nifurahi sana, umenipa maneno matamu sana nashukuru sana rafiki yangu

18 + 17= 35..........Being 35 and having 17 yrs in marriage sio mchezo aisee, yaani nahisi bado una miaka mingi tu inakuja, maana kwa umri wako mdogo na uzoefu ulio nao kwa kweli una hitaji pongezi Gaga, ndio maana una mabusara sana Mungu akupe nguvu na akuzidishie upendo juu ya mme wako na familia kwa ujumla, wako wasichana wenye umri kama wako na bado wameshikilia mchuma wanasubiria kiti wakae.....duh sikutegemea aisee nashukuru sana kwa story nzuri gaga ila nina maswali nitakuuliza PM....umri ulioanza kunanihii
Hahahaha kwa kweli mautundu niliyaanza mdogo sana, loooo ila hayakuniadhiri yamelipa eeee au sio, cha muhimu namshukuru mpenzi mume wangu kwa kugundua udogo wangu na kuwa mkali wakati mwingine ili niwe kwenye mstari, raha nyingine ya kuolewa mdogo ni muda wote unaonekana wewe ni mtoto tu mpaka wakati mwingine unakuwa mkali ili akuchukulie kama mtu mzima, aaaich kwa kweli raha sana
 
.Ndoa yetu na iheshimiwe na watu wote,,,,AMIN

Muendelee kuiheshimu ninyi wenyewe wengine watafuata mkumbo mkiteteleka mjue ya kuwa fisi wapo mtaani wakisubir..to pick the pieces...................best of luck.........just keep CHRIST in the first place He is going to take you places you never imagine ever existed 4 u.............................I know this because I am one of its living testimony
 
Duh! Yaani hii sredi imenifanya ni-log in ili nikupe ma-congrats wewe na my husband wako! Halafu umenitia moyo kweli... Kumbe yule bidada nayefukuzia niongeze bidii, au nikiona vipi nahama mtaa ili animiss!! Ha ha haaa!! Hongereni sana na kila la heri.
Fukuzia mwanawane ikiwezekana hama hata mtaa msichana ataanza kukumiss kama kweli umemuingia moyoni, kuna wakati mwingine huw a tunajidanganya kwamba hatuwapendi watu kumbe deep inside kabisa mahaba yamejaa tele
 
Muendelee kuiheshimu ninyi wenyewe wengine watafuata mkumbo mkiteteleka mjue ya kuwa fisi wapo mtaani wakisubir..to pick the pieces...................best of luck.........just keep CHRIST in the first place He is going to take you places you never imagine ever existed 4 u.............................I know this because I am one of its living testimony
Kwa kweli nimefurahi umenipa moyo , na Mungu najua ndiye aliyenifikisha hapa nilipo, pia nina shuhuda nyingi tu za kushuhudia, ahsante sana
 
Back
Top Bottom