MWANAHARAMU
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 4,826
- 12,470
Fikra duni na analyst wa Tanu ndio aliwaweka.Rejea historia
Simba ni timu ya wakoloni walianzishwa kupinga Yanga waliokuwa wanafanya harakati za ukombozi
Zamani Simba iliitwa Queens đź‘‘ stars baadae ikaitwa Sunderland ndo likaja jina la Simba au mbumbumbu
Historia inaonyesha Simba na Yanga zilizaliwa kutoka timu iliyoitwa New Young.
Mwaka 1935 na 1936 baada ya mgawanyiko ndio ikaundwa Young African na Queens zikiwa ndio timu za wazawa.
Ila tofauti yake Simba ikawa ni waafrika waliopata elimu, wafanyakazi wa bandari na watoto wa kata ya Mchafukoge.
Wakati Young Africa ndio timu iliyoundwa na makabwela kutoka bonde la Mto msimbazi , wasio na mbele Wala nyuma na ugmfahamu hafifu.
Hizi timu zote zilishiriki Ligi ya waafrika watupu na kuongeza hamasa ya Ligi.
Hapa hakukuwa na jina la kiafrika Wala kiswahili ila zote zilitumia lugha ya kiingereza tu.
Baadae Simba ikaungana na Arabs football club Ili kuboresha zaidi. Na kuitwa Sunderland
Huku Yanga ikibakia na wahamiaji haramu na wakimbizi kutoka Malawi huko na Burundi.
Baadae Sunderland ikaitwa Eagle F.c
Na kusaidia uhuru wa Tanzania na mwanachama wake Sykes alimpa nauli Nyerere Ili aende Uingereza kudai uhuru.
Young Africa ikabakia timu ya wabaguzi, wasio na elimu, kipato na upeo finyu.
Baada ya uhuru Raisi wa Zanzibar akaomba hizi timu azitumie majina ya kiafrika hivyo Eagle f.c ikajiita Simba s.c ila Young Africa ikabakia na majina ya kikoloni mpaka leo.
Ila wanachama kwa sababu ya upeo mdogo, elimu ndogo wakashindwa kutamka ndio ikaitwa Yanga ambayo haipo popote kwenye katiba yao.
Mazingira: Simba ipo Town ila Young Africa ipo bondeni kule jangwani kwenye mafuriko.
Mpaka leo, hali haijabadilika kabisa
Wanachama wao wanasapoti uongozi wao kwa kugomea mechi wakati wanaijua kitakacho wakuta.
Simba ni Taifa kubwa
Simba nguvu moja
Ubaya Ubwela