TFDA ichunguzeni dawa ya meno ya whitedent

TFDA ichunguzeni dawa ya meno ya whitedent

PRINCE CROWN

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
5,210
Reaction score
4,178
Mamlaka ya chakula na dawa tunaomba muichunguze dawa ya whitedent, imekua na athari ya kuunguza mdomo,kupasuka na kuufanya mdomo kupoteza test unapo itumia, nadhani kemikali wanayoitumia siyo nzuri kwa kutumia inaathari,
 
Utakuwa na tatizo wewe..pengine una ugonjwa wa UMAKI-upungufu wa mate kinywani.
 
Tanzania Foods and Drugs Authority fanyieni hili kazi achaneni na Carolight. Hata lamba lamba na maji ya matunda ya mzee wetu hapo mmeyafungia macho wakati mnajua yana madhara kibao.
 
Wadau ni kweli mara nyingi mimi hali hiyo imenitoke sana hadi nikajihisi labd ni mimi tu, ila kwa sasa nimebadilish aina ya dawa na hainidhuru, dawa ya whitedent ina matatizo.
 
Mimi ile nyeupe ilinishindaga kitambo nikahamia whitedent herbal ikawa afadhali kidoogo
 
acheni kutisha watu me hiyo ndio dawa ninayotumia so unanishauri nikatupilie mbali?duuuh na jana tu ndio nimenunua ile kubwa kubwa!!!!!!!!
 
Hizo dawa si salama ingawa tunapuuzia,mi pia ilishanitokea nkaacha kutumia,na sasa natumia colgate basi.
 
acheni kutisha watu me hiyo ndio dawa ninayotumia so unanishauri nikatupilie mbali?duuuh na jana tu ndio nimenunua ile kubwa kubwa!!!!!!!!

Mkuu haujatishiwa wewe km haudhuriki ni bahati yako bt kiukweli hata bei tu zimetofautiana pakubwa mno,colgate ndogo ya sh 2500 ni sawa na whitedent kubwa moja.
 
Mamlaka ya chakula na dawa tunaomba muichunguze dawa ya whitedent, imekua na athari ya kuunguza mdomo,kupasuka na kuufanya mdomo kupoteza test unapo itumia, nadhani kemikali wanayoitumia siyo nzuri kwa kutumia inaathari,

kama chokaa vile
 
hiyo dawa ni rahisi ila ina madhara makubwa mi nilikuwa naitumia fizi zikawa zinavimba nikatibiwa fizi
na baadae nikahamia colget na tena nilijua madhara yake
baada ya kupitia uzi hapa jf.
uliokuwa unachambua hiyo dawa ilivyotengenezwa
 
Mwenyewe ilinishinda kitambo Sana hii dawa aisee,
Yaani ilikuwa kila nikiitumia ulimi unachanikachanika vidonda vidogovidogo hadi kula inakuwa shida hasa hot meals mpaka nilihisi nimekanyaga miwaya!!

Halafu hawa jamaa wanavyo-iindiketi exp date yao ni utata mtupu tena kwa vile vi-tube vidogo ni shida kusomeka aisee.

Haki za walaji hazizingatiwi kabisa na hawa jamaa.

MBAYA ZAIDI:Hii ni dawa kama dawa zingine lakini utakuta zinauzwa kwenye magulio/minadani tena kwa kuwekwa juani siku nzima zisipouzika zinarudishwa madukani tena hapo matching guys nao wanashinda nazo juani PIA.

TFDA wameng'ang'ana na vipodozi tu.
W.T.F
 
TFDA is a toothless dog. wanawakomalia wajasiriamali wadogo wadogo wa vipodozi wakati viwanda vya Mohd enterp vinatengeneza bidhaa ambazo hazina viwango na zimetapakaa mujini
 
Mi natumia sana hii dawa, kuna kitu nimegundua zipo za aina mbili.
Kwa hii ya HERBAL, sanasana ile kubwa utakuta ina manufactured date in full (yaani ina tarehe,mwezi na mwaka ilipotengenezwa)
ukija expire date utakuta ina tarehe ya mwisho kutumika na mwezi ila mwaka hauonekani, hiyo ujue ni fake.
Hizi ambazo hazina mwaka wa ku-expire zinauzwa sana barabarani kwa wale wanaouza kwenye meza mida ya usiku kw baadhi ya maeneo.
Mara nyingi muhuri wake ni maandishi makubwa ukilinganisha na ile ambayo ni dawa ya kweli.
Nilivopita sehemu nyingi barabarani na kuona zote zinafanana nikaamua kuingia dukani na kuikuta hii ambayo ni nzuri muhuri wake upo clear kabisa unasomeka tarehe,mwezi na mwaka kwa sehemu zote mbili (manufactured date na expire date).
Tuwe makini ndugu zangu ni kweli dawa ya whitedent ipo ambayo ni fake.
 
Tanzania kila kitu feki, tusubiri tu kupata rais feki,
 
Mamlaka ya chakula na dawa tunaomba muichunguze dawa ya whitedent, imekua na athari ya kuunguza mdomo,kupasuka na kuufanya mdomo kupoteza test unapo itumia, nadhani kemikali wanayoitumia siyo nzuri kwa kutumia inaathari,

Ni kweli. Hiyo dawa ina hitilafu. Mimi na familia yangu tuliacha kitambo sana kuitumia. Binafsi niliharibika kabisa ulimi. Toka niachane nayo niko poa.
 
Ile wanaita whitedent herbel unaweza ukala na mkate ina sukari balaa.
 
Back
Top Bottom