TFDA ichunguzeni dawa ya meno ya whitedent

TFDA ichunguzeni dawa ya meno ya whitedent

Kweli jamani Whitedent nimeisha nunua fake kama mara mbili hv!

Hii dawa ilisababisha nikawa nang'olewa meno kila mwaka, nikapoteza morals 4 ndipo mtu mmoja akaniambia nibadili dawa kwani huenda Whitedent inasababisha. Toka niachane nayo sijapata tatizo tena la meno leo miaka 5. TBS ndo wanaotuponza, tukiona nembo tunanunua kumbe hivyo tu.
 
Hii Dawa nikiitumia Fizi zinavimba. NAKUUNGA MKONO MKUU TFDA wafanye uchunguzi
 
Mkuu haujatishiwa wewe km haudhuriki ni bahati yako bt kiukweli hata bei tu zimetofautiana pakubwa mno,colgate ndogo ya sh 2500 ni sawa na whitedent kubwa moja.

Mkuu si sahihi kulinganisha bei na ubora wa kitu!mara nyingine huu ni ushamba tu!Colgate pia ipo fake sana sokoni na bei ni ile ile!Kinachofanya colgate iuzwe bei kubwa zaidi ni brand yake.Walitumia gharama kubwa kuitangaza kwa muda mrefu na hivyo jina linajiuza lenyewe.Haya mambo kama huyajui utakuwa unanunua vitu bei kubwa kubwa kwa vile tu una hela ya kununua ila suala la ubora ni kitu kingine

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Nilisha acha kuitumia miaka mingi sana iliyopita...... Niligundua Hiyo sio dawa nzuri kwangu kwasababu meno yalikuwa yakiuma na kuchimbika. Nilipo anza kutumia Colgate Herbal tatizo lili isha kabisa. Na dawa nyingine za kuchunguza ni hizi za kichina nina mashaka nazo.
 
Imesababisha watu wengi siku hizi wananuka midomo.ndio maana big G na PK soko lake linakua kwa kasi
 
amia colgate mkuu dawa ya dunia nzima achana na hao mwanafunzi mweupe made in mbagala

#Zitto
 
Kama vile nimefunguliwa macho kwa michango ya baadhi ya wadau humu ndani. Mimi nilianza kutumia White dent toka mwanzoni mwa miaka ya tisini wakati ule inawekwa kwenye paketi za aluminium, lakini kwa sasa naona kama kuna tofauti ya ubora ila kutokana na mazoea najikuta nashindwa kuiacha lakini kwa kweli kuna tofauti fulani ya ubora.

Hasa hizi zenye bei ya Tsh. 2500, kuna nyingine ukifungua mara mbili tu shingo yake inakatika, kwa hiyohuwezi tena kuifunga. Na ikikaa wazi inaganda basi tabu tupu hata ile ladha ya dawa ya meno mdomoni siyo ile tena.

Kwa kweli kama TFDA mnafuatilia uzi huu inabidi mfanye kitu na mimi kuanzia leo natangaza kuchukua maamuzi magumu kuhusu hii dawa.
 
nunueni ALOE au ANGOLA ni nzuri zinaondoa hadi matatizo ya mafindo findo na meno kuuma
 
Nyie pigeni kelelee,mwenzenu mwanzo nilikuwa natumia MAJIVUGATE,baada ya kupanda bei nikaona nitumie MKAAGATE.
Mkemia mkuu -ni Marehemu Bibi Yangu
Mkaguzi Mkuu-alikuwa mwalimu wa Zamu alipokuwa akinisifia meno yako masafi kweli
Muuzaji mkuu-Wapishi
Msambazaji mkuu-Akili kumkichwa
Expire date zake-Mpaka chakula kingine kipikwe
 
niliacha sikunyingi hiyo dawa maana meno yalikuwa yanatoboka sana. tangu nilivoanza kutumia Colgate tatizo liliisha mpaka leo
 
Mi natumia sana hii dawa, kuna kitu nimegundua zipo za aina mbili.
Kwa hii ya HERBAL, sanasana ile kubwa utakuta ina manufactured date in full (yaani ina tarehe,mwezi na mwaka ilipotengenezwa)
ukija expire date utakuta ina tarehe ya mwisho kutumika na mwezi ila mwaka hauonekani, hiyo ujue ni fake.
Hizi ambazo hazina mwaka wa ku-expire zinauzwa sana barabarani kwa wale wanaouza kwenye meza mida ya usiku kw baadhi ya maeneo.
Mara nyingi muhuri wake ni maandishi makubwa ukilinganisha na ile ambayo ni dawa ya kweli.
Nilivopita sehemu nyingi barabarani na kuona zote zinafanana nikaamua kuingia dukani na kuikuta hii ambayo ni nzuri muhuri wake upo clear kabisa unasomeka tarehe,mwezi na mwaka kwa sehemu zote mbili (manufactured date na expire date).
Tuwe makini ndugu zangu ni kweli dawa ya whitedent ipo ambayo ni fake.

Ngoja nianze kuzichunguza na mm maana ndio dawa yangu Ili niwe najua ipi fake
 
Hiyo itakuwa kweli kwani nimetumia moja ikaniumiza meno sana. Hili liserikali halijali watu wake kabisa. Inawezekana zinatengenezwa na akina madabida.
 
Hii sio dawa mimi naitumia kwenye kung'arishia taa za gari.
 
Back
Top Bottom