TFDA Failure isiwe kufunga viwanda

TFDA Failure isiwe kufunga viwanda

MVUMBUZI

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2011
Posts
5,182
Reaction score
2,330
Nimesikitishwa sana na kauli ya Mkurugenzi mkuu wa TFDA Hiiti Sillo kuwa amefunga kiwanda cha dawa kilichopo Njiro Arusha baada ya kubaini kuwa ndicho kilichojusika kusambaza dawa bandia za ARVs.

Ikumbukwe kuwa kilichoanza ni dawa bandia kugundulika katika soko na backward tracking ikafanyika kubaini ziliko toka na mchakato huu ukachukua muda huku sintofahamu na utata wa mhusika ukitawala hadi walipokuja kugundua very late na kuamua kufunga kiwanda.

Alichokifanya Mr. Sillo ni kujikosha kuwa hahusiki hata kidogo na uzembe wa dawa bandia kuuzwa na hatimaye kufanya kiini macho kwa kujibaraguza kuwa wako makini na wakali na hivyo kuchukua hatua za kukifungia kiwanda kiwanda cha dawa.

Kazi za TFDA ni kama ilivyoandikwa hapa " Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA) is a regulatory body under the Ministry of Health and Social Welfare which is responsible for regulating the quality and safety of food, drugs, cosmetics and medical devices.

Kwa ufupi TFDA walitakiwa wafanye monitoring ya uzalishaji wa madawa katika viwanda hivi regularly ili kuhakikisha dawa zinazozalishwa zinakidhi viwango. Swali je wao walikuwa wanafanya na walikuwa wapi nini hadi dawa zikazalishwa na kuingia sokoni? Ninaamini uzembe wa wao kutosimamia vema viwanda na hatimaye kuacha mianya ya uchakachuaji imepelekea dawa bandia kuzalishwa.
Hata hivyo najiuliza je viwanda vya dawa viko vingapi hata washindwe kuvifanyia proper monitoring?

Kama wangelijua hilo basi walitakiwa wao kwanza kuwajibika kwa kutofanya kazi yao sawa sawa na kuacha mianya ya na hivyo kusababisha uchakachuaji.

Kufunga kiwanda ni sawa na kutibu dalili badala ya kutibu chanzo cha ugonjwa. Pia kufunga kiwanda ambacho ni mojawapo ya viwanda vichache vya madawa nchini ni kuendeleza wimbi na kuruhusu mianya ya dawa feki kutoka nyje kuendelea kupenya TZ.
Siafiki na wazo la kufunga kiwanda ambacho kwa TZ viko vichache sana kwa sababu tu mtu mbinafsi anarusha mpira kwa mwenzake kujikosha bila kujali mamilioni ya waTZ watakaoathirika kwa kufungwa kiwanda si kwa kukosa ajira tu bali kutopata dawa za kutosha.

Kwa mtu makini kufunga kiwanda badala ya TFDA kuwajibika ni option suicidal kuliko zote na siamini kama viongozi wenye dhamana na uchungu na hii nchi watauona ni uamuzi wa busara.

Kuna kila sababu ya kuamini kuna chain ya events hapo zenye lengo la kutaka kunufaisha baadhi ya wanaoagiza dawa nje na si tusidanganyike kuwa lengo ni kuboresha mfumo wa utengenezaji dawa.

Namshauri Mkurugenzi wa TFDA akubali kuwa uzembe uko upande wao katika kusimamia viwanda vya kutengeneza madawa na cha kufanya ni kuwajibika na kuimarisha monitoring system yao. Alichokifanya ni sawa na ku eliminate ugonjwa kwa kumuua mgonjwa badala ya kupambana na chanzo cha ugonjwa. Kama bado utendaji wa TFDA hautaboreshwa ikiwamo monitoring system yao basi tutarajie viwanda vingi zaidi kufungwa!!!
Lazima tukubali hii ni failure ya TFDA na kosa liskwepwe kwa kufunga viwanda bali wahusika wawajibike.
 
Mkuu, hawa TFDA ndio walivyo.!
Kuna duka la uokaji mikate (bakery) moja hapa jijini watu walikula bidhaa zake na familia ikapoteza wapendwa wao kwa sumu ya bidhaa ile. Ila amini usiamini waliendelea na biashara na cheti chao cha uthabiti kutoka TFDA kiliendelea na kazi.
Hii ndio kazi ya mamlaka.....!
 
Nimesikitishwa sana na kauli ya Mkurugenzi mkuu wa TFDA Hiiti Sillo kuwa amefunga kiwanda cha dawa kilichopo Njiro Arusha baada ya kubaini kuwa ndicho kilichojusika kusambaza dawa bandia za ARVs.

Ikumbukwe kuwa kilichoanza ni dawa bandia kugundulika katika soko na backward tracking ikafanyika kubaini ziliko toka na mchakato huu ukachukua muda huku sintofahamu na utata wa mhusika ukitawala hadi walipokuja kugundua very late na kuamua kufunga kiwanda.

Alichokifanya Mr. Sillo ni kujikosha kuwa hahusiki hata kidogo na uzembe wa dawa bandia kuuzwa na hatimaye kufanya kiini macho kwa kujibaraguza kuwa wako makini na wakali na hivyo kuchukua hatua za kukifungia kiwanda kiwanda cha dawa.

Kazi za TFDA ni kama ilivyoandikwa hapa " Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA) is a regulatory body under the Ministry of Health and Social Welfare which is responsible for regulating the quality and safety of food, drugs, cosmetics and medical devices.

Kwa ufupi TFDA walitakiwa wafanye monitoring ya uzalishaji wa madawa katika viwanda hivi regularly ili kuhakikisha dawa zinazozalishwa zinakidhi viwango. Swali je wao walikuwa wanafanya na walikuwa wapi nini hadi dawa zikazalishwa na kuingia sokoni? Ninaamini uzembe wa wao kutosimamia vema viwanda na hatimaye kuacha mianya ya uchakachuaji imepelekea dawa bandia kuzalishwa.
Hata hivyo najiuliza je viwanda vya dawa viko vingapi hata washindwe kuvifanyia proper monitoring?

Kama wangelijua hilo basi walitakiwa wao kwanza kuwajibika kwa kutofanya kazi yao sawa sawa na kuacha mianya ya na hivyo kusababisha uchakachuaji.

Kufunga kiwanda ni sawa na kutibu dalili badala ya kutibu chanzo cha ugonjwa. Pia kufunga kiwanda ambacho ni mojawapo ya viwanda vichache vya madawa nchini ni kuendeleza wimbi na kuruhusu mianya ya dawa feki kutoka nyje kuendelea kupenya TZ.
Siafiki na wazo la kufunga kiwanda ambacho kwa TZ viko vichache sana kwa sababu tu mtu mbinafsi anarusha mpira kwa mwenzake kujikosha bila kujali mamilioni ya waTZ watakaoathirika kwa kufungwa kiwanda si kwa kukosa ajira tu bali kutopata dawa za kutosha.

Kwa mtu makini kufunga kiwanda badala ya TFDA kuwajibika ni option suicidal kuliko zote na siamini kama viongozi wenye dhamana na uchungu na hii nchi watauona ni uamuzi wa busara.

Kuna kila sababu ya kuamini kuna chain ya events hapo zenye lengo la kutaka kunufaisha baadhi ya wanaoagiza dawa nje na si tusidanganyike kuwa lengo ni kuboresha mfumo wa utengenezaji dawa.

Namshauri Mkurugenzi wa TFDA akubali kuwa uzembe uko upande wao katika kusimamia viwanda vya kutengeneza madawa na cha kufanya ni kuwajibika na kuimarisha monitoring system yao. Alichokifanya ni sawa na ku eliminate ugonjwa kwa kumuua mgonjwa badala ya kupambana na chanzo cha ugonjwa. Kama bado utendaji wa TFDA hautaboreshwa ikiwamo monitoring system yao basi tutarajie viwanda vingi zaidi kufungwa!!!
Lazima tukubali hii ni failure ya TFDA na kosa liskwepwe kwa kufunga viwanda bali wahusika wawajibike.
MVUMBUZI endelea na utafiti, uchunguzi na yanayofanana na hayo...hapo nilipobadilisha rangi katika maelezo yako ndipo penye tatizo kubwa katika sakata hili. Hakuna, narudia tena HAKUNA hata sehemu moja katika maelezo ya DG wa TFDA yaliyozungumzwa kuwa TPI walitengeneza dawa husika. Kusupply dawa na kutengeneza dawa ni vitu viwili tofauti. Unaweza kutengeneza na usi-supply, unaweza ukatengeneza na uka-supply, na unaweza usitengeneze na u-supply. Watanzania wanaambiwa, "Nyaraka tulizonazo zinaonyesha kuwa dawa husika zilikuwa supplied MSD na TPI". Hii statement haisemi kuwa hizi dawa zilitengenezwa TPI, wamiliki wa TPI walishalizungumza hili kuwa TPI haina teknolojia ya kuzalisha aina ya dawa husika
Watu wanapata wapi idea kuwa dawa hizi zilitengenezwa TPI beats me, yaani sielewi ni namna gani mtu anapata hiyo idea kutoka kwenye maelezo ya kuanzia naibu katibu mkuu, Naibu Waziri na Waziri (wa Wizara ya Afya). Hawa wote wameongelea uwepo wa nyaraka zinazoonyesha kuwa dawa hizo ziliingia mfumo wa MSD zikiingizwa na TPI. Sasa hapa si ndio sheria inachukua mkondo wake. [kuthibitisha kama ni kweli TPI wali-supply au hawaku-supply] Kuna mahakama basi na serikali iishtaki TPI kama ina uhakika na inalozungumza. Hivi MVUMBUZI kwa upeo wa haraka haraka tu, dawa ziwe zimetengenezwa TPI [ambako kuna ofisi ya kanda ya TFDA ikiongozwa na wataalamu waliobobea kuhusu sayansi ya madawa] halafu wataalamu wake wahusika wawe wameachwa tu wanadundika town?? Yaani wahusika wa udhibiti na uhakiki ubora wa MSD washughulikiwe halafu wale waliozitengeneza hizo dawa waachwe tu?? Dawa hazikutengenezwa TPI, zile dawa zinajulikana kampuni inayozitengeneza na supplier wake ndani ya nchi anajulikana. #KAVUMBUEZAIDIMKUU
 
TFDA ni regulator ambaye hana meno,anafanya kazi kimazoea pia anafanya kazi kisiasa.
 
MVUMBUZI endelea na utafiti, uchunguzi na yanayofanana na hayo...hapo nilipobadilisha rangi katika maelezo yako ndipo penye tatizo kubwa katika sakata hili. Hakuna, narudia tena HAKUNA hata sehemu moja katika maelezo ya DG wa TFDA yaliyozungumzwa kuwa TPI walitengeneza dawa husika. Kusupply dawa na kutengeneza dawa ni vitu viwili tofauti. Unaweza kutengeneza na usi-supply, unaweza ukatengeneza na uka-supply, na unaweza usitengeneze na u-supply. Watanzania wanaambiwa, "Nyaraka tulizonazo zinaonyesha kuwa dawa husika zilikuwa supplied MSD na TPI". Hii statement haisemi kuwa hizi dawa zilitengenezwa TPI, wamiliki wa TPI walishalizungumza hili kuwa TPI haina
teknolojia ya kuzalisha aina ya dawa husika
Watu wanapata wapi idea kuwa dawa hizi zilitengenezwa TPI beats me, yaani sielewi ni namna gani mtu anapata hiyo idea kutoka kwenye maelezo ya kuanzia naibu katibu mkuu, Naibu Waziri na Waziri (wa
ya Afya). Hawa wote wameongelea uwepo wa nyaraka zinazoonyesha kuwa dawa hizo ziliingia mfumo wa MSD zikiingizwa na TPI. Sasa hapa si ndio sheria inachukua mkondo wake. [kuthibitisha kama ni kweli TPI wali-supply au hawaku-supply] Kuna mahakama basi na serikali iishtaki TPI kama ina uhakika na inalozungumza. Hivi MVUMBUZI kwa upeo wa haraka haraka tu, dawa ziwe zimetengenezwa TPI [ambako kuna ofisi ya kanda ya
TFDA ikiongozwa na wataalamu waliobobea kuhusu sayansi ya madawa] halafu wataalamu wake wahusika wawe wameachwa tu wanadundika town?? Yaani wahusika wa udhibiti na uhakiki ubora wa MSD washughulikiwe halafu wale waliozitengeneza hizo dawa waachwe tu?? Dawa hazikutengenezwa TPI, zile dawa zinajulikana kampuni inayozitengeneza na supplier wake ndani ya nchi anajulikana. #KAVUMBUEZAIDIMKUU
TPI MANGEMENT has instead of manufacturing the said medicines counterfeit other manufactures medicines in a process that caused adulteration with a wrong drug.
 
Kuna kasoro kuanzia uingizaji wa materials pale bandari[Customs,TDFA,Mkemia Mkuu] kama kundi la kwanza,kundi la pili wanafuta wadau wengine katika mtiririko wa uingizaji bidhaa nchini.!!!
 
TFDA iwajibike kwa kuruhusu dawa ziingie sokoni ndipo iwaadhibu TPI. Hamjatuambia kwa nini hamkuzizuia. Hivi mkijua zimetengenezwa China mtaenda kufunga kiwanda huko?
 
TPI MANGEMENT has instead of manufacturing the said medicines counterfeit other manufactures medicines in a process that caused adulteration with a wrong drug.
Ongea ueleweke, wengine umombo tabu
 
Ongea ueleweke, wengine umombo tabu

Utawala wa TPI badala ya kutengeneza dawa husika kutoka kwenye maligafi walifungasha dawa za mtengenezaji mwingine na katika kufanya hivyo wakafunga dawa tofauti na jina lililo kwenye kifungashio
 
mcyawn usimlaumu , huyu kesha athirika na madawa bandia!
124ali ni suala la lugha ya kufundishia ndilo linalotoa nafasi ya kuchagua lugha ya kutumia...hayo ya dawa bandia kuniathiri umenifanya nicheke tu.
 
Utawala wa TPI badala ya kutengeneza dawa husika kutoka kwenye maligafi walifungasha dawa za mtengenezaji mwingine na katika kufanya hivyo wakafunga dawa tofauti na jina lililo kwenye kifungashio
Hayo maelezo ni uwongo kwa sababu:
1.) Utawala hauhusiki moja na kufungasha dawa, kuna wafanyakazi walioajiriwa kwa kazi ya kufungasha dawa.
2.) Hakuna kauli yeyote ya kuthibitisha uwepo wa ushahidi kuwa TPI waliingiza dawa nchini kwa nia ya kufungasha ili waiuzie MSD
3.)Kama kweli TPI waliingiza hizo dawa nchini na waliiuzia MSD, basi kungekuwa na mtiririko wa nyayo za nyaraka zinazothibitisha hilo, kwani utaratibu wa kuingiza dawa nchini una hatua nyingi (ikiwemo kuomba kibali MSD, kupata uthibitisho wa ubora wa dawa husika TFDA na uthibitisho wa kushindwa kuizalisha dawa hiyo kwa wakati) ambapo huwezi ukazikwepa.
4.) Kauli ya Serikali kupitia Wizara ya Afya inaeleza uwepo wa nyaraka ndani ya MSD unaoonyesha kuwa TPI ndio waliiuzia MSD, lakini hakuna maelezo kuhusu uwepo wa mtiririko wa nyayo za nyaraka zinazo thibitisha kuwa ni kweli TPI ndio walioiuzia MSD.
Nyaraka haziwezi zikaibuka tu bila nyingine kuwepo, kuna uwezekano mkubwa zikawa ni za kughushi hizo...hebu jiulize yafuatayo, yaani TPI watengeneze dawa March 2011, waiuzie MSD May 2011 (Hapa tu panatia shaka, haijawahi tokea mtengeneza ARV dunia hii akakaa na dawa alizokwisha zalisha zaidi ya wiki 2!!) Halafu MSD wakae nazo bohari mpaka August 2012 (muda ambao ni karibu na chaguzi ndani ya CCM) ndio waanze kuzisambaza. Zisambazwe koote, lakini zikakamatiwe Tarime (ambako ni home town ya mmoja wa wapinzani wa wamiliki wa TPI katika huo uchaguzi)...
 
Mkuu, hawa TFDA ndio walivyo.!
Kuna duka la uokaji mikate (bakery) moja hapa jijini watu walikula bidhaa zake na familia ikapoteza wapendwa wao kwa sumu ya bidhaa ile. Ila amini usiamini waliendelea na biashara na cheti chao cha uthabiti kutoka TFDA kiliendelea na kazi.
Hii ndio kazi ya mamlaka.....!

Hapana........walifungiwa kipindi kirefu mpaka uchunguzi ulipokamilika.....tena wapinzani wao kibiashara walikomalia sana wafungiwe kabisa.....wana product nzuri tu na ahao wapendwa walikula sumu kwingine kabisa
 
Hayo maelezo ni uwongo kwa sababu:
1.) Utawala hauhusiki moja na kufungasha dawa, kuna wafanyakazi walioajiriwa kwa kazi ya kufungasha dawa.
2.) Hakuna kauli yeyote ya kuthibitisha uwepo wa ushahidi kuwa TPI waliingiza dawa nchini kwa nia ya kufungasha ili waiuzie MSD
3.)Kama kweli TPI waliingiza hizo dawa nchini na waliiuzia MSD, basi kungekuwa na mtiririko wa nyayo za nyaraka zinazothibitisha hilo, kwani utaratibu wa kuingiza dawa nchini una hatua nyingi (ikiwemo kuomba kibali MSD, kupata uthibitisho wa ubora wa dawa husika TFDA na uthibitisho wa kushindwa kuizalisha dawa hiyo kwa wakati) ambapo huwezi ukazikwepa.
4.) Kauli ya Serikali kupitia Wizara ya Afya inaeleza uwepo wa nyaraka ndani ya MSD unaoonyesha kuwa TPI ndio waliiuzia MSD, lakini hakuna maelezo kuhusu uwepo wa mtiririko wa nyayo za nyaraka zinazo thibitisha kuwa ni kweli TPI ndio walioiuzia MSD.
Nyaraka haziwezi zikaibuka tu bila nyingine kuwepo, kuna uwezekano mkubwa zikawa ni za kughushi hizo...hebu jiulize yafuatayo, yaani TPI watengeneze dawa March 2011, waiuzie MSD May 2011 (Hapa tu panatia shaka, haijawahi tokea mtengeneza ARV dunia hii akakaa na dawa alizokwisha zalisha zaidi ya wiki 2!!) Halafu MSD wakae nazo bohari mpaka August 2012 (muda ambao ni karibu na chaguzi ndani ya CCM) ndio waanze kuzisambaza. Zisambazwe koote, lakini zikakamatiwe Tarime (ambako ni home town ya mmoja wa wapinzani wa wamiliki wa TPI katika huo uchaguzi)...
Mkuu si sahihi kuniita muongo kwa sababu pamoja na taarifa nyingi ulizonazo kuhusu sakata hili uelewe kwamba aliyelipwa na kupata faida kwa kuizuia MSD dawa hizo ni TPI. MSD kwa hali yeyote haina faida kwa kumlipa TPI halafu wafungashe dawa nyingine na sio aliyoipokea kutoka TPI. Dawa hizi hazikupatika na Tarime tu bali MSD ilizisambaza na kufika hadi vituo sehemu mbalimbali nchini mfano mkoani Ruvuma. Kwa kifupi sioni faida (motive) ya player yeyote katika suala hili isipokua kwa TPI Management. Kuhusu muda zilipopokelewa hadi kufika kwa mteja kama ulivyoeleza hayo yanasababu zake ambazo ni tofauti na ile ya kiwanda kuwauzia MSD dawa bandia. Utawala wa TPI kulingana na muongozo wa utengenezaji wa dawa wenye ubora(GMP) unahusika moja kwa moja katika kuhakisha Ubora (Quality assurance). Ndio maana ni utawala unaokaa na wakaguzi wanapotembelea kiwanda kujiridhisha kuhusu ubora. Usitumie nguvu sana kwenye hili kwani ukweli umeshaanza kuonekana kama ilivyo ada na karibuni utasikia atakayepanda kizimbani. Haitakua maofisa wa MSD.
 
cha kujifunza ni kwamba, kwa china wale waliotengeneza maziwa ya kadhuru watoto walinyongwa, kwa tz mtu anayetengeneza dawa feki etc na kusababisha vifo vya watu, anafungiwa tu, no more actions. hakuna kitu kibaya kama dawa bandia, kwasababu unajipinda kuinywa ukifikiri unakunywa dawa ili upone kumbe unakunywa makapi na sawa tu na haujanywa kitu. ugonjwa unaendela kula ndani kwa ndani matokeo yake watu wanakufa. kuna watu wengi sana wanakufa hata kwa malaria tu kwasababu ya dawa bandia....nilikuwa nategemea hatua moja zaidi ya hiyo ambayo TFDA imechukua.
 
Mkuu, hawa TFDA ndio walivyo.!
Kuna duka la uokaji mikate (bakery) moja hapa jijini watu walikula bidhaa zake na familia ikapoteza wapendwa wao kwa sumu ya bidhaa ile. Ila amini usiamini waliendelea na biashara na cheti chao cha uthabiti kutoka TFDA kiliendelea na kazi.
Hii ndio kazi ya mamlaka.....!

Royal Oven ya Mikocheni?
 
Mkuu si sahihi kuniita muongo kwa sababu pamoja na taarifa nyingi ulizonazo kuhusu sakata hili uelewe kwamba aliyelipwa na kupata faida kwa kuizuia MSD dawa hizo ni TPI. MSD kwa hali yeyote haina faida kwa kumlipa TPI halafu wafungashe dawa nyingine na sio aliyoipokea kutoka TPI. Dawa hizi hazikupatika na Tarime tu bali MSD ilizisambaza na kufika hadi vituo sehemu mbalimbali nchini mfano mkoani Ruvuma. Kwa kifupi sioni faida (motive) ya player yeyote katika suala hili isipokua kwa TPI Management. Kuhusu muda zilipopokelewa hadi kufika kwa mteja kama ulivyoeleza hayo yanasababu zake ambazo ni tofauti na ile ya kiwanda kuwauzia MSD dawa bandia. Utawala wa TPI kulingana na muongozo wa utengenezaji wa dawa wenye ubora(GMP) unahusika moja kwa moja katika kuhakisha Ubora (Quality assurance). Ndio maana ni utawala unaokaa na wakaguzi wanapotembelea kiwanda kujiridhisha kuhusu ubora. Usitumie nguvu sana kwenye hili kwani ukweli umeshaanza kuonekana kama ilivyo ada na karibuni utasikia atakayepanda kizimbani. Haitakua maofisa wa MSD.
Huja-address issue nilizozingumza hapo kukueleza kuwa huo ni uongo uliousema, unasema kukaa kwa muda mrefu kwa dawa katika bohari la MSD kuna maelezo yake, hebu nipe basi japo kwa kukisia, kutakuwa na nini?? Maana umekuwa bold mpaka kusema kwa uhakika kuwa TPI management ndio waliofaidika na hiyo biashara na kuwa pesa wamepokea wao ina maana maelezo madogo kama ya ni kwa nini kwa mwezi MSD wana-issue zaidi ya dozi laki tano (500,000) za dawa za ARV lakini wakaweza kukaa na dozi kama elfu kumi na mbili (12,000) kwa zaidi ya mwaka mmoja wakisubiri kuzisambaza?? Turudi kwenye suala la nani anafaidika kati ya MSD na TPI kwenye biashara ya dawa hizo; mkuu, thamani ya mauzo ya dawa aina hiyo ya TT-VIR 30 ambayo kwa uwezo wa kiwanda kwa mwezi ni zaidi ya bilioni za kitanzania 2.5, TPI kama kampuni haiwezi ikawa na akili ya kuzalisha dawa ili iziuze ambazo zinaweza kuzalishwa kwa siku 1 tu, ingetaka kufaidika ingezalisha dawa za zaidi ya miezi mitatu ili ipate pesa za kutosha, na thamani ya hizo dawa zilizouzwa hapo hazitoshi hata ku-attend overhead costs. Katika dawa ambazo zimezalishwa mwaka 2011 na kuuziwa MSD, hakuna hata batch 1 ambayo ilikutwa ina matatizo ya kiubora au kinyaraka, nyaraka zote zilikuwepo, isipokuwa hiyo OC.01.85 ambayo iliikosa nyaraka za kimaabara...hapa naona TPI inachinjiwa baharini, ila nimefurahi kuwa unalifahamu la umuhimu wa kuwepo mahakama ila nikukumbushe tu kuwa, kupandishwa mahakamani si kigezo cha kuonyesha kuwa TPI ndio wakosaji, ila ni watuhumiwa. Uthibitisho tutakuja kuusikia baada ya mahakama kujiridhisha na ushahidi wote utakaotolewa...
 
Huja-address issue nilizozingumza hapo kukueleza kuwa huo ni uongo uliousema, unasema kukaa kwa muda mrefu kwa dawa katika bohari la MSD kuna maelezo yake, hebu nipe basi japo kwa kukisia, kutakuwa na nini?? Maana umekuwa bold mpaka kusema kwa uhakika kuwa TPI management ndio waliofaidika na hiyo biashara na kuwa pesa wamepokea wao ina maana maelezo madogo kama ya ni kwa nini kwa mwezi MSD wana-issue zaidi ya dozi laki tano (500,000) za dawa za ARV lakini wakaweza kukaa na dozi kama elfu kumi na mbili (12,000) kwa zaidi ya mwaka mmoja wakisubiri kuzisambaza?? Turudi kwenye suala la nani anafaidika kati ya MSD na TPI kwenye biashara ya dawa hizo; mkuu, thamani ya mauzo ya dawa aina hiyo ya TT-VIR 30 ambayo kwa uwezo wa kiwanda kwa mwezi ni zaidi ya bilioni za kitanzania 2.5, TPI kama kampuni haiwezi ikawa na akili ya kuzalisha dawa ili iziuze ambazo zinaweza kuzalishwa kwa siku 1 tu, ingetaka kufaidika ingezalisha dawa za zaidi ya miezi mitatu ili ipate pesa za kutosha, na thamani ya hizo dawa zilizouzwa hapo hazitoshi hata ku-attend overhead costs. Katika dawa ambazo zimezalishwa mwaka 2011 na kuuziwa MSD, hakuna hata batch 1 ambayo ilikutwa ina matatizo ya kiubora au kinyaraka, nyaraka zote zilikuwepo, isipokuwa hiyo OC.01.85 ambayo iliikosa nyaraka za kimaabara...hapa naona TPI inachinjiwa baharini, ila nimefurahi kuwa unalifahamu la umuhimu wa kuwepo mahakama ila nikukumbushe tu kuwa, kupandishwa mahakamani si kigezo cha kuonyesha kuwa TPI ndio wakosaji, ila ni watuhumiwa. Uthibitisho tutakuja kuusikia baada ya mahakama kujiridhisha na ushahidi wote utakaotolewa...
Honestly I appreciate the level of details you are flashing here both on quantity supplied in the supply chain and value of medicines manufuctured by TPI. The money trail goes to TPI. What would be the better reason to counterfeirt a drug? About inefficiencies in supply chain to supply that particular brand that should be onother issue. I belive you are not suggesting as one of directors at TPI did that MSD manufuctured or adulterated TPI products/that batch. Am also impressed with the level of information on the documents that are available and you know clearly which document is missing at MSD which is related to receipt of that particular batch....anyway in investigation one should look for all information and never a particular document. A gate pass can tell a lot if you carefully scrutinise it under a 'microscope". I belive the investigative team will do that and come to the conclusion like the one I know and the one made in the parliament "Kiwanda cha TPI kimeiuzia bohari ya dawa MSD dawa bandia".
 
Honestly I appreciate the level of details you are flashing here both on quantity supplied in the supply chain and value of medicines manufuctured by TPI. The money trail goes to TPI. What would be the better reason to counterfeirt a drug? About inefficiencies in supply chain to supply that particular brand that should be onother issue. I belive you are not suggesting as one of directors at TPI did that MSD manufuctured or adulterated TPI products/that batch. Am also impressed with the level of information on the documents that are available and you know clearly which document is missing at MSD which is related to receipt of that particular batch....anyway in investigation one should look for all information and never a particular document. A gate pass can tell a lot if you carefully scrutinise it under a 'microscope". I belive the investigative team will do that and come to the conclusion like the one I know and the one made in the parliament "Kiwanda cha TPI kimeiuzia bohari ya dawa MSD dawa bandia".

Nimecheka kishenzi, serously!! Hiyo statement yako ya mwisho ni statement ambayo haina tatizo ndani yake, tatizo mlilonalo wabongo ni kuwa hiyo statement mnainyumbulisha into "TPI manufactured fake ARVs" kutengeneza na kuuza dawa ni vitu viwili tofauti, hizo dawa zilizokutwa ndani ya vifungashio vimetengenezwa kwa teknolojia ambayo haipo TPI, Tanzania wala Afrika ya Mashariki. Hizo dawa kampuni iliyozitengeneza inajulikana na mwenye vibali vya kuiingiza nchini anajulikana. Mbona hatajwi?? Itafute ripoti ya Naibu Waziri wa Afya ya kwanza kuhusu sakata hili, ilitajwa kampuni inayotengeneza dawa hizo na Brand name yake.
Kuna angle moja unaitumia kuituhumu TPI inanishangaza sana, yaani money trail kuonyesha dawa kuifaidisha TPI ndio kumei-restrict namna yako ya kulichambua hili jambo. Turudi hapo kwenye nani mwingine anaweza kufaidika kwa kuingiza dawa hizo TPI. Hivi sasa serikali inawapatia waathirika takriban laki tano dawa za kurefusha maisha (ARV) na kwa namna ambavyo wataalimu wa tiba husika walivyoutengeneza mfumo wa tiba za HIV/AIDS ni kuwa mgonjwa anachukua dozi ya mwezi 1 kwa mkupuo regardless ya tiba nyingine anazoendelea nazo (TB, URT, OI na vitu kama hivyo)...inamaanisha kuna dozi laki tano na ushee hivi zinatolewa kila mwezi. Kwa sasa, zote zinaagizwa kutoka nje, hasa India na China. Kuna kiwanda kipya kinajengwa na TPI cha kisasa ambacho hakuna kiwanda cha kisasa zaidi kwa miundo mbinu na teknolojia kama hicho kusini mwa jangwa la Sahara ukiondoa Afrika Kusini (ambao nao ndio wanakitengeneza mwaka huu), kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha dozi za ARV laki moja kwa mwezi. Hiki ni kiwanda ambacho kimombo ni "Pilot" kinaangaliwa ufanisi wake na nchi nyingi duniani ili kama kikifanikiwa kuendeshwa kwa ufanisi, viwanda zaidi kama hicho vitajengwa katika nchi zinazoendelea. Ina maana hapa Tanzania pekee vinaweza vikajengwa zaidi ya hicho, na ina maana hao wanaoagiza dawa watapoteza biashara yao. Hivi unadhani wao watakaa kimya tu waangalie wakinyang'anywa slesi zao za mkate??? Hii kitu imetengenezwa mkuu, imepikwa...mbona hao wataalamu wa uhakiki na udhibiti ubora wa TPI husikii kutajwa???Hakuna ushahidi wowote zaidi ya hizo nyaraka zilizokutwa hapo bohari ya MSD
 
Nimecheka kishenzi, serously!! Hiyo statement yako ya mwisho ni statement ambayo haina tatizo ndani yake, tatizo mlilonalo wabongo ni kuwa hiyo statement mnainyumbulisha into "TPI manufactured fake ARVs" kutengeneza na kuuza dawa ni vitu viwili tofauti, hizo dawa zilizokutwa ndani ya vifungashio vimetengenezwa kwa teknolojia ambayo haipo TPI, Tanzania wala Afrika ya Mashariki. Hizo dawa kampuni iliyozitengeneza inajulikana na mwenye vibali vya kuiingiza nchini anajulikana. Mbona hatajwi?? Itafute ripoti ya Naibu Waziri wa Afya ya kwanza kuhusu sakata hili, ilitajwa kampuni inayotengeneza dawa hizo na Brand name yake.
Kuna angle moja unaitumia kuituhumu TPI inanishangaza sana, yaani money trail kuonyesha dawa kuifaidisha TPI ndio kumei-restrict namna yako ya kulichambua hili jambo. Turudi hapo kwenye nani mwingine anaweza kufaidika kwa kuingiza dawa hizo TPI. Hivi sasa serikali inawapatia waathirika takriban laki tano dawa za kurefusha maisha (ARV) na kwa namna ambavyo wataalimu wa tiba husika walivyoutengeneza mfumo wa tiba za HIV/AIDS ni kuwa mgonjwa anachukua dozi ya mwezi 1 kwa mkupuo regardless ya tiba nyingine anazoendelea nazo (TB, URT, OI na vitu kama hivyo)...inamaanisha kuna dozi laki tano na ushee hivi zinatolewa kila mwezi. Kwa sasa, zote zinaagizwa kutoka nje, hasa India na China. Kuna kiwanda kipya kinajengwa na TPI cha kisasa ambacho hakuna kiwanda cha kisasa zaidi kwa miundo mbinu na teknolojia kama hicho kusini mwa jangwa la Sahara ukiondoa Afrika Kusini (ambao nao ndio wanakitengeneza mwaka huu), kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha dozi za ARV laki moja kwa mwezi. Hiki ni kiwanda ambacho kimombo ni "Pilot" kinaangaliwa ufanisi wake na nchi nyingi duniani ili kama kikifanikiwa kuendeshwa kwa ufanisi, viwanda zaidi kama hicho vitajengwa katika nchi zinazoendelea. Ina maana hapa Tanzania pekee vinaweza vikajengwa zaidi ya hicho, na ina maana hao wanaoagiza dawa watapoteza biashara yao. Hivi unadhani wao watakaa kimya tu waangalie wakinyang'anywa slesi zao za mkate??? Hii kitu imetengenezwa mkuu, imepikwa...mbona hao wataalamu wa uhakiki na udhibiti ubora wa TPI husikii kutajwa???Hakuna ushahidi wowote zaidi ya hizo nyaraka zilizokutwa hapo bohari ya MSD
Your level of imagination and your "devil's advocate attitued" makes you qualified to direct a quality "mafia" style movie not the Kanumba's class. The matter of the fact is that somebody pocketed money for selling those products to MSD and that they should be taken to account for that act. Your conspiracy theories has no place in this case.
 
Back
Top Bottom