Tetesi za kununua wabunge na Madiwani: CCM inatafuta nini tena wakati wana majority Bungeni?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,516
Katika mfumo wa kidola tulionao, Bunge ni kila kitu. Pamoja na uwepo wa Serikali, Bunge na Mahakama kama mihimili ya kidola, Bunge ni mhimili muhimu kuliko yote katika kufanya siasa, kuisimamia Serikali, kutunga sheria na hata kupitisha bajeti. Mwenye wingi wa wabunge ndiye 'anayekula bata' kwakuwa alitakalo ndilo linalofanyika na kuwa Bungeni.

Kwa wingi wa Wabunge walionao CCM katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, CCM inalimiliki itakavyo Bunge. Wana haja gani ya kuwanunua Wabunge wa upinzani? Vyama vyenye Wabunge Bungeni ni CCM, CHADEMA,CUF,NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo. Kati ya vyama hivyo, CCM ina wabunge wengi kuzidi jumla ya wabunge wa vyama vya upinzani. Kuna haja gani ya kununua Wabunge wa upinzani?

Kuhusu Madiwani, CCM inaongoza zaidi ya asilimia 80 ya Majiji, Manispaa, Miji na Miji Midogo nchini kutokana na kuwa na wingi wa Madiwani. Wana Mameya, Manaibu Meya, Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa kutosha katika kuongoza Halmashauri hizo.Ndiyo kusema, Ilani ya CCM inatekelezwa bila kikwazo. Madiwani wa upinzani wa nini kununuliwa?

Katika sura hiyo ya kisiasa Bungeni na kwenye Halmashauri, tuamini kuwa Wabunge na Madiwani wa upinzani wanaojiunga na CCM wanajiunga kweli kwa utayari wao binafsi katika kumuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake (kama ni kweli)? Au, tuamini kuwa kinachofanyika (kama ni kweli) ni jitihada za kuua upinzani na kuturejesha katika mfumo wa chama kimoja? CCM inafaidikaje ikiwa tayari ina wingi wa aina hiyo?
 
Katika sura hiyo ya kisiasa Bungeni na kwenye Halmashauri, tuamini kuwa Wabunge na Madiwani wa upinzani wanaojiunga na CCM wanajiunga kweli kwa utayari wao binafsi katika kumuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake (kama ni kweli)? Au, tuamini kuwa kinachofanyika (kama ni kweli) ni jitihada za kuua upinzani na kuturejesha katika mfumo wa chama kimoja? CCM inafaidikaje ikiwa tayari ina wingi wa aina hiyo?

Nadhani ndiyo lengo!.
Lakini tujiulize je Dunia ya leo Chama kimoja Mambo ya Kidumu fikra za mwenyekiti zitatufikisha kwenye Nchi ya Viwanda???
 
Katika mfumo wa kidola tulionao, Bunge ni kila kitu. Pamoja na uwepo wa Serikali, Bunge na Mahakama kama mihimili ya kidola, Bunge ni mhimili muhimu kuliko yote katika kufanya siasa, kuisimamia Serikali, kutunga sheria na hata kupitisha bajeti. Mwenye wingi wa wabunge ndiye 'anayekula bata' kwakuwa alitakalo ndilo linalofanyika na kuwa Bungeni.

Kwa wingi wa Wabunge walionao CCM katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, CCM inalimiliki itakavyo Bunge. Wana haja gani ya kuwanunua Wabunge wa upinzani? Vyama vyenye Wabunge Bungeni ni CCM, CHADEMA,CUF,NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo. Kati ya vyama hivyo, CCM ina wabunge wengi kuzidi jumla ya wabunge wa vyama vya upinzani. Kuna haja gani ya kununua Wabunge wa upinzani?

Kuhusu Madiwani, CCM inaongoza zaidi ya asilimia 80 ya Majiji, Manispaa, Miji na Miji Midogo nchini kutokana na kuwa na wingi wa Madiwani. Wana Mameya, Manaibu Meya, Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa kutosha katika kuongoza Halmashauri hizo.Ndiyo kusema, Ilani ya CCM inatekelezwa bila kikwazo. Madiwani wa upinzani wa nini kununuliwa?

Katika sura hiyo ya kisiasa Bungeni na kwenye Halmashauri, tuamini kuwa Wabunge na Madiwani wa upinzani wanaojiunga na CCM wanajiunga kweli kwa utayari wao binafsi katika kumuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake (kama ni kweli)? Au, tuamini kuwa kinachofanyika (kama ni kweli) ni jitihada za kuua upinzani na kuturejesha katika mfumo wa chama kimoja? CCM inafaidikaje ikiwa tayari ina wingi wa aina hiyo?
Kwan Nyalandu alinunuliwa?. Mwanasheria unapoamini habar zisizokuwa na ushaidi taaluma yako huitendei haki. Wasiokuwa wabobez katika masuala ya sheria wanaionaje taaluma hii.
 
Kwan Nyalandu alinunuliwa?. Mwanasheria unapoamini habar zisizokuwa na ushaidi taaluma yako huitendei haki. Wasiokuwa wabobez katika masuala ya sheria wanaionaje taaluma hii.
Nyarandu amekuwa Mbunge zaidi ya Miaka 15 bado alikuwa Waziri mtu wa namna hii niwazi kilicho mtoa CCM sio pesa kutakuwa na kitu kingine ambacho sisi hatukijui,lakini yule maulidi aliyanza ubunge Juzi pamoja na masilahi lufufu yaliopo kwenye ubunge eti aache kwa ajili ya kuuunga mkono Juhudi za Magufuli kweli kabisa wewe na utu uzima wako inakuingia akilini? hata mtoto wa darasa la 7 hawezi kukubaliana na hoja kama hiyo
 
Mimi sidhani kama wananunuliwa
Hudhani lakini ni kweli hata kama si cash ni ktk mazingira ya kazi/biashara.
Mfano kati ya wale madiwani watano kule Arusha, mmoja alikuwa anamiliki shule, na shule ilifungiwa kisa udiwani wake cdm. Na sharti ilikuwa a defect kutoka cdm ndio shule iruhusiwe kufanya kazi!! Angalia Wema alivyotangaza tu kwenda cdm lipsticks zake zilipigwa marufuku imebidi ajisalimishe. Angalia yaliyompata Mbowe ktk biashara zake?! Je ni wangapi walivunjiwa mikataba yao na NHC, mashamba yake yameharibiwa lakini mkuu alipofika mto Kagera anasema limeni !!!

Hata kama si cash lakini mazingira yanafanywa magumu kwenye shughuli zao.
HII NI AFRICA
 
Katika mfumo wa kidola tulionao, Bunge ni kila kitu. Pamoja na uwepo wa Serikali, Bunge na Mahakama kama mihimili ya kidola, Bunge ni mhimili muhimu kuliko yote katika kufanya siasa, kuisimamia Serikali, kutunga sheria na hata kupitisha bajeti. Mwenye wingi wa wabunge ndiye 'anayekula bata' kwakuwa alitakalo ndilo linalofanyika na kuwa Bungeni.

Kwa wingi wa Wabunge walionao CCM katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, CCM inalimiliki itakavyo Bunge. Wana haja gani ya kuwanunua Wabunge wa upinzani? Vyama vyenye Wabunge Bungeni ni CCM, CHADEMA,CUF,NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo. Kati ya vyama hivyo, CCM ina wabunge wengi kuzidi jumla ya wabunge wa vyama vya upinzani. Kuna haja gani ya kununua Wabunge wa upinzani?

Kuhusu Madiwani, CCM inaongoza zaidi ya asilimia 80 ya Majiji, Manispaa, Miji na Miji Midogo nchini kutokana na kuwa na wingi wa Madiwani. Wana Mameya, Manaibu Meya, Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa kutosha katika kuongoza Halmashauri hizo.Ndiyo kusema, Ilani ya CCM inatekelezwa bila kikwazo. Madiwani wa upinzani wa nini kununuliwa?

Katika sura hiyo ya kisiasa Bungeni na kwenye Halmashauri, tuamini kuwa Wabunge na Madiwani wa upinzani wanaojiunga na CCM wanajiunga kweli kwa utayari wao binafsi katika kumuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake (kama ni kweli)? Au, tuamini kuwa kinachofanyika (kama ni kweli) ni jitihada za kuua upinzani na kuturejesha katika mfumo wa chama kimoja? CCM inafaidikaje ikiwa tayari ina wingi wa aina hiyo?
Ukizoea kufanya biashara haramu, huwezi kuiacha kamwe. Ukimaliza kuwanunua wote utaishia kuwauza hata watoto wako kisha unawanunua tena.

Vv
 
Nimeamua kutoka kwenye familia yetu na kuhamia kwa jirani baada kuona anamafanikio ambayo wazazi wangu wamekuwa wakiyatafuta kwa muda mrefu, naenda kum support jirani kwani anayaishi tuliyokuwa tunayatafuta
 
Kuna kijana aliyekuwa Mgombea wa Jimbo la Bumbuli ameomba radhi wapiga kura wake akisema amevumilia kunyang'anywa Mali zake za halali zikiwemo mashamba na kadispensari na bado wakamuundia na zengwe la TRA akainua mikono juu.

Issue ya ununuzi na vitisho ipo kwa asilimi 100.Waansheria mtusaidie watanzania.Wanachofanyiwa hasa vijana ni kuwanyima any source of income ili waweze kuwabeba kwa urahisi tu maana hata milino 2 zitakuchuka.Haki ya kuamua kuamini ITIKADI lazima tuitafute hakuna njia
 
Hivi wewe Mtu kachaguliwa ubunge Mwaka Juzi hajawahi kuwa Mbunge leo hii anasema anaacha eti kwa kuridhishwa na utendaji wa JPM alafu famila yake inakula nyasi au? mtu aache mshahara wa M 10+ kwa mwezi bado pension ya M 200+ baada ya miaka 5.Inakuingia akilini kweli?
Ushahidi ndio hakuna.
 
Hakuna mbunge wala wabunge wanaonunuliwa ni mtu anaposoma nyakati kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020
 
Mkuu, kwa heshima kubwa kwako, nathubutu kusema kuwa hujaelewa mada yangu. Tafadhali isome tena na uchangie.
Kuna tatizo linalowakumba watu wengi hapa JF ambayo ilitakiwa kuwa GT, na hilo tatizo ni kutoelewa mada. Mtu anaisoma mada kama ilivyo na moja kwa moja anaingiza unazi wa chama. Kama angekusoma vizuri ulikua na maana gani kwa namna moja ama nyingine hata huo mchango wake wewe aliouandika wewe umeuweka lakini haupo wazi upo katikati ya mistari.
 
Back
Top Bottom