Tetesi madaktari kuzimua mgomo wao

Nchi masikini ya pili kutoka chini na bado tunamuda kibao wa kugoma huku tunataka tuendelee, Labda mbingu zishuke ndo bongo itaendelea.
ni kweli kabisa ndugu Bufa..., migomo haina tija na inarudisha maendeleo nyuma. ila si kwa nchi kama tanzania. iweje uendelee kuumia na kazi wakati kinachopatikana hakifanyi kazi iliyokusudiwa????. kinaishia mikononi mwa wachache wanaojilimbikizia mali. tunalipwa kidogo n bado tunakatwa kodi kubwa ambayo hatuoni inachikifanya. UKITEKA MAJI MBALI NA KUYAMWAGA KWENYE PIPA LINALOVUJA, NA BADO UKAENDELEA TU, HAKIKA UTAKUWA MWENDAWAZIMU. ziba matundu kwanza ndo uendelee kuweka maji. Migomo inaweza saidia kidogo kwa hilo.

Bufa jiangalie sana, na jitathmini juu ya uwezo wako wa kufikiri........, otherwise great thinkers hapakufai.
 
Kipindi cha mfungo si ndicho ambacho DHAIFU huwa anaanguka!, akisikia hivyo lazi asalimu ardhi. yangu macho.
Jana nilimuona kwenye gazeti moja la kila siku akiwa anaongea na mama mmoja huku akiwa amelala sakafuni........sikuelewa maana yake ni nini, au ndo anajihami kutokana na sababu ulizozitoa hapo juu?
 
hakuna nchi maskini labda wewe mwenyewe watu wana fedha nje ya nchi zaidi ya bajeti ya serikali ya mwaka usema nchi maskini ,ungesema nchi yenye watu waroho na wabinafsi ningekuelewa.
Tanzania si maskini hata kidogo

Ndugu yangu siujui umasikini ni nini nasikia tu watu wakilalamika ila kwangu mm maisha na safi san. Pili, watu kua na jela zaidi ya bajeti ya serikali nje ya nchi haimaanishi kwamba basi nchi ni tajiri hizo ni pesa zao, ulivyompambe kama watu wengine utaanza kusema ooh tuna mbuga, madini, sijui ardhi na maji hivyo pekee havitoshi nchi kua tajiri dunia ya leo, singapore, tswana, swiss hawana yote hayo na wako mbelea yenu saaana sijui mtawaambia nini. TZ masikini sana sana na mbingu zishuke ndo itaendelea.
 
Sikubaliani na migomo hata kidogo kwani bado kuna njia mbadala za kutafuta suluhu. Watanzania wenzangu ni lazima tuangalie faida na hasara za migomo katika jamii yetu. Daktari anapogoma nani anapata hasara/matatizo?.

Kudai malipo makubwa na kuboreshewa mazingira ya kufanyia kazi ni madai ya msingi kabisa, lakini pia tuangalie hali na uwezo uliopo wa serikali. Tusipende kulaumu na kudai kisichowezekana, huo ni uendawazimu wa hali ya juu.

Kwa upande wangu sioni sababu ya kuwa na migomo pamoja na maandamano yasiyo na tija.

Labda kwa sababu walisema watafanya kila liwezekanalo nchi isitawalike.
 
Kama hali ndiyo hiyo kuna raha kweli ya kutawala, au ndiyo dalili za nchi kutotawalika.
 
Busara zinahitajika hapo, waanze kupunguza kujilimbikizia mali wanasiasa kwanza ndipo hiyo migomo itakwisha, vinginevyo sahau.
 
Ili kupunguza hizi stress dr feki itabid asafiri nje ya nchi kodogo
Roho za mabalaa zinamwandama kwa kuwa ulinzi wa majeshi aliyoahidiwa na Sheikh Yahya umeyeyuka!! Asipotubu na kumrudia muumba wake, huo ndio mwisho wake!!
 
naibu spika akihutubia watanzania waishiio Korea ya kusini siku moja alituasa tusitembelee jf kwani kuna upotoshwaji mkubwa. So wanalijua jukwaa hili na wanapitia hapa
 
Dhaifu ni Schizophrenia,
Kuhudhuria Harusi na kuhudhuria Msiba kwake hakuna tofauti.

Sasa watumishi wa serikali wakigoma,
anashindwa kuelewa yeye anahusika vipi,

Madakatari hawafanyi kazi Ikulu!
Walimu hawafanyi kazi Ikulu!

Migomo ya watu hawa inamhusu nini??

Ndiyo asii ya Dhaifu kutabasamu kila mahali,
brain yake haina uwezo wa kujitune na reality.


Tumbo la kuhara laingia Magogoni
 
Raisi wetu ana tatizo la "hubris"
Which means extreme pride or arrogance. Hubris often indicates a loss of contact with reality and an overestimation of one's own competence or capabilities, especially when the person exhibiting it is in a position of power.(Wikipedia)
 
Jamiiforum ni jukwaa tosha. Na usidanganyike hao watendaji wakuu wa serikali wanatembelea humu kwenye hili jukwaa kwa sana kusikia kinachoongelewa.

Natumia mobile mkuu, ningekupiga na bonge la LIKE. Hivi kuna wachovu bado hawaamini nguvu ya JF! Kwa hakika ni source ya habari nyeti hata kwny ofisi nyeti serikalini. Tunayaona haya...
 
Madaktari mgomo wanini tena wakati wameshaambiwa asiyetaka aache?au wanakuja na madai mengine tofauti na yale ya kwanza?
 
Nchi masikini ya pili kutoka chini na bado tunamuda kibao wa kugoma huku tunataka tuendelee, Labda mbingu zishuke ndo bongo itaendelea.

Wewe vipi? Nani alikuambia kuwa nchi yetu maskini? Wewe ni magamba?
 
Madaktari mgomo wanini tena wakati wameshaambiwa asiyetaka aache?au wanakuja na madai mengine tofauti na yale ya kwanza?

WanaJF!

Kuna post nilichangia sometimes back, I remember to have told you thinking loudly that "Mgomo wa Madaktari" ulikuwa batili simply because ulivunja sharia za Kazi za Mwaka 2004.

Before rushing to open and post new posts on the subject matter Nyie vijana just let it go . Kasomeni sheria inasemaje and then come back.

Dhaifu alikwisha sema his hopeless govt of the day is no in position to offer more than fifteen percentum (15%)increase who ever is not willing to accept that offer should peacefully look for an employer of his choice. This was spoken openly and he didn't want to mince words pronto!

Sasa hizo ngonjera za kufufua mgomo wa Madaktari zinatoka wapi vijana . The train has gone and the President aliwaonea huruma kwani mlivunja sheria halali . Mimi tu nikemee hii Tabia mbaya ya Rais kuwa raisi na kuwasamehe watu hata kabla ya kuwapeleka mahakamani kumjibu tuhuma. If he had sober washauri sio hao akina Salva angengojea wakishahukumiwa then waende jela angojee siku ya siku kuu ya Uhuru awasamehe. Aliwasamehe akina Rostam and the Chenges,Msabaha, Ngeleja and the whole pack historian will judge him come 2016 dead or alive.

Msiote kugoma ila endeleeni na huo Mgomo baridi anyway hakuna sheria inayozuia mgomo baridi. But ushauri wangu why don't you simply pack and go anywhere except hell of course my dear Doctors!!!!
 
Ni kweli kuwa mishahara ya wafanyakazi walio wengi ni midogo sana kumudu mahitaji muhimu ya binadamu. Lakini tuangalie chanzo ni nini? how can we move forward? je kulalamika kwenye mitandao is a solution? kwa nini tusiombe jukwaa tukayazungumza wakiwepo watendaji wakuu wa serikali? tujaribu kuangalia njia mbadala ya kurekebisha hali. Mawazo yetu yatasaidia. Lakini kwa halli ya sasa ilivyo ya uchumi mishahara mikubwa haitawezekana na huo ndio ukweli. Ingawaje vitu vinaweza kufanyika mambo yakawa mazuri. PIa tusipende ku generalize issues. Sio wote walioko CCM ni wabaya na sio wote walioko upinzani ni wazuri huo ndio ukweli. Watanzania bado tuna ubinafsi mkubwa na hiyo inachangiwa na sera za nchi yetu.
Ulichosema ni kweli kabisa,ninacho kiona mimi tatizo lipo kwa watunga SERA! kwanini? WANABAGUA WATUMISHI. idara ya kilimo mishahara yao ni mizuri sana lengo lilikuwa ni kuwashawishi waweze kukaa vijijini ambako ndio kwenye mashamba na wakulima pia. lakini wakasahau kuwa huko vijijini kuna walimu wengi tu ambao nao wanahitaji motisha.Jambo hili linaleta manung'uniko miongoni mwa watumishi wa umma.haiwezekani mwalimu alipwe tshs 300,000 mtu wa ugani akaanza na tshs 700,000/= na wote wanaishi kijiji kilekile na wote wana shahada za fani zao.
Tunaweza tukawa tumeweza kuwashawishi watu wa ugani kukaa vijijini lakini kwa upande mwingine tumewakatisha tamaa walimu.watu wa ngazi fulani ya elimu bila kujali fani zao basi tofauti ya mshahara isiwe kubwa kihivyo.kuwe na tofauti ya 100,000 hadi 200,000 lakini sivyo ilivyo sasa.mathalani katika sakata hili la walimu na serikali hata walimu wote walio goma wakifukuzwa tuna uhakika gani watakao kuja watakubali hiyo mishahara isiyo kidhi mahitaji?
ushauri wangu,NCHI hii ni yetu sote,tusibaguane,yatupasa kuona UAMZI WOWOTE UNAO HUSU WATU NA USTAWI WAO UNAZINGATIA MASLAHI mapana ya NCHI.UDUMISHE UPENDO,UMOJA WETU na MSHIKAMANO.
 
Wewe vipi? Nani alikuambia kuwa nchi yetu maskini? Wewe ni magamba?
We sijui ndo wa wapi unataka kusema bongo ni tajiri? acheni kujidanganya wabongo kwamba nchi yenu ni tajiri, mbuga na milima pekee havifanyi nchi kua tajiri.
 
Back
Top Bottom