Tetesi: Mabinti wanabakwa JKT

Tetesi: Mabinti wanabakwa JKT

Naunga mkono hoja. Kwa kuwa tayari hii habari imeshasambaa kwenye mitandao mbali mbali hapa nchini, kuna haja ya viongozi wa jeshi kufanya uchunguzi huru ili kubaini haya. Vinginevyo kwa kweli hii itakuwa ni hatari kubwa kwa watoto wetu na kwa kizazi chetu cha nchi hii.
Mkuu uchunguzi huru akufanyie nani nchi yetu hii. Kuna matukio mangapi mpaka sasa hatujaona majibu . Muombe Mungu tu kama una mtoto mwingine usimpeleke huko . Mpeleke vyuo vingine sio lazima wote wasome mlimani.
 
Mdogo wako alikuwa Omnipresent katika makambi yote?? Inawezekana vitendo hivi havikuwa vinafanyika katika kambi aliyokuwepo mdogo wako lakini vikawa vinafanyika katika kambi nyingine, so utakuwa ukosefu wa busara, mathalani, ku judge hali inayoendelea ktk kambi za Tanzania nzima kwa msingi wa maelezo/ madai ya mtu aliyeko kambi ya makutupora...na pia, inawezekana pia vilikuwa vinafanyika hata kambi aliyokuwepo lakini akawa hajui kwasababu victims wengine wana prefer ku baki kimya kwasababu wanaona aibu ku share taarifa hizo na wengine..au yeye anauwezo wa kuona sirini na hivyo akawa anajua siri zote za recruits wenzake na wakufunzi wao? Wewe ndio unaleta propaganda na mzaha kwa kujaribu kutuambia tuamini maneno ya mdogo wako na kupuuza madai haya ya msingi yanayopaswa kuchunguzwa. Uchunguzi huru ndio unapswa kututoa wasiwasi na sio maneno ya mdogo wako....
Mkuu nimekupata unajua sisi watz sijui tumelogwa na nani tu. Yaani tupo tayari kuita nyeusi nyeupe ili mradi watawala watuone tupo pamoja nao. Na hii tabia ndio inayorudisha nyuma mandeleo ya nchi yetu. Inashangaza kuona mtu anatetea eti hakuna ufirauni JKT wakati anaona wengi wanalalamikia hali hii. Ina maana hawa wote wanasema uongo?
 
Hii habari si ya kubeza hata kidogo! hata kama sheria na taratibu haziruhusu, lakini bado kuna uwezekano mkubwa wa haya mambo kutokea. Mfano: katika Tanzania hakuna utaratibu au sheria unaoruhusu kufanya ufisadi, kula/kutoa rushwa na kadhalika lakini bado watu wanafanya hayo mambo. Hili linaweza likawa ni sehemu ya uhalifu lazima serikali ifanye uchunguzi wa kutosha. Tunajua wanajeshi na maaskari wetu wanavyopenda vitu vya bwerere...yote yawezekana! EE Mungu tusaidie!

mkuu mkada umenena kweli.
Mi nina exprience na jkt na polisi, taratibu za majeshi haziruhusu hayo kutokea.
 
Hakuna kubakwa ila ni kujilegeza tu na kutaka unafuu,basi anajikuta anajilegeza kwa wakufunzi kisha mambo yanakuwa hivo.hakuna mtu anabakwa siku hiz.
 
mkuu mkada umenena kweli.
Mi nina exprience na jkt na polisi, taratibu za majeshi haziruhusu hayo kutokea.
Mkuu taratibu mbali,na hurka ya mtu binafsi mbali,taratibu za majeshi yetu haziruhusu majeshi kuhalifu lakini mwenyewe umeshuhudia wanajeshi(JWTZ na POLISI)Jinsi wanavyojihusisha na vitendo vya uhalifu hivi karibuni.Nilikuwa Masange JKT 1987 acha kabisa hawa dada zetu wana mitihani.
 
Pole sana Mkuu. Kama kuna namna ya kupata mawasiliano na binti yako basi fanya hivyo haraka sana na umuachie mama yake afuatilie kwa karibu kujua hali huko kambini. Kama itabidi kufanya maamuzi mazito basi msisite kufanya hivyo kabla hali haijawa mbaya zaidi.

Hapa ndiyo panaponiumiza sana. Nimesomesha kwa gharama kubwa, kabla hajaanza kujitegemea, naweza kujikuta naanza tena kuingia gharama ya kumuuguza. Oooh, shit. Naumia sana siyo siri. Hizi habari kwa hakika zinanitisha sana.
 
Hili swala sio kwamba ni la kutumia uzoefu wa JKT. Yanayotokea kule sio siri tena kwani mawasiliano yapo na vitendo hivyo vinajulikana. Cha muhimu ni viongozi kuangalia huu utaratibu kwa jicho la tatu.
 
wakati serikali inaanzisha mfumo wa kudahili wanachuo kwa njia ya mtandao nakumbuka humu jamii forum kulitokea wanaharakati wakatuambia kwamba walalahoi watakosa nafasi kwakuwa hawana access to internet. Cha ajabu ni kwamba hakutokea hata mmoja akakosa kutuma application labda kama ni mzembe na pia tumeshuhudia ambapo jamii wamefaidika na mfumo huo kwani unalipia once unapata access katika vyuo vyote.

Baadae vyuo vikapiga kelele wanaletewa watoto majuha kumbe wenyewe walikuwa wanafaidika na pesa za walalahoi za application. Chuo kina nafasi 500 application 12000. Wanataia kelele kutetea matumbo yao.

So hapa huenda kuna watoto wayai wanahofu kazi ya maisha plus ya jkt na sasa wanatafuta wanasiasa na wanaharakati uchwara wawaombee kuondolewa na kazi za makuzi.

Lazima watanzania tujifunze kubaini laghai ya majitu fulani.
 
kwa hali hii husipeleke mtoto wako.kwani hii hali hata mimi nilishaona huko kambini.Mtoto wa kike hawezi kumkatalia afande.akimwambia aende kufanya usafi nyumbani kwake.
 
Sina utaalamu na mambo ya jeshi lakini mimi ni mwalimu kitaaluma na nafundisha sekondari. Nachelea kusema kuwa jambo hili linatiwa chumvi sana na nahisi kuna ukweli watu wanauyumbisha ili kutia doa nia nzuri ya serikali ya kujenga uzalendo kwa vijana wetu. Kifo hutokea popote, tumuombee aliyetangulia.

Badala ya ushabiki watu tungejikita kutafakari mfumo mzima wa maadili ya vijana wetu. Msije kudhani wala kusingezia kuwa wanaoendesha mafunzo ya uzalendo (JKT) mi mabazazi kuliko mafataki wa mtaani na hata shuleni. Tuache kunyosha mikono, taifa lilishapotea.
 
Hivi kwani wanalazimishwa kwenda JKT?
sasa why mtu uchague ujinga kama huu?
wazazi na hawa wanafunzi wana akili kweli?
sielewi kabisa
 
Hivi hao madada wa tanzania kugawa kwao ni huko jkt tu? Mbona ya vyuoni hamyasemi? Gengeni na kwa machinga wanapotaka unafuu wa bidhaa? Kwenye siasa wanapotaka upendeleo? Msitie chumvi maneno kwa hila nyepesi, ubakaji haujawahi kuwa rahisi kwa kiwango hicho kinachozungumzwa sasa.
 
Ndugu zangu, najua siyo utaratibu kuleta mjadala hapa kwa msingi wa habari zilizopo facebook. Nakubali kabisa kwamba JF si ya viwango vya facebook. Lakini nimeiona hii habari facebook, na kwa kuwa nina binti yangu yupo kambi ya JKT Tabora, pressure imenipanda na nimekosa amani kabisa.

Hebu wenye uzoefu na mambo ya huko watuambie ukweli upoje.

Habari yenyewe ni kama ifuatavyo:


[/FONT][/COLOR][/COLOR][/h]
MY TAKE: Tusijekuwa tumepeleka watoto wetu jeshini kwa kisingizio cha kuwafunza uzalendo, halafu mwisho wa siku wakarudi na HIV, na hasira kali dhidi ya nchi yao. Kama hili lina ukweli basi hii ni hali ya hatari sana kwa watoto wetu. Tunaweza kujikuta miaka mtano ijayo, 80% ya graduates wa vyuo vikuu ni wagonjwa wa UKIMWI. Ikumbukwe kwamba waliokwenda JKT ni wenye division one hadi three. Kwa maana ya kwamba ni cream ya nchi ndiyo imekwenda huko. Tutabaki na mamburula nchi hii, if this is true.

Hakuna tofauti JKT na Taasisi zingine za elimu. Ni vigumu mtu kubakwa Jeshini JKT Kwani kuna sheria Ngumu mno na ikibainika aliyefanya hivyo kwake ni hatari sana. Hata hivyo, huwa kuna baadhi ya askari watovu wa nidhamu hutumia mbinu kama vile kutoa kazi ngumu hadi mtu aamue mwenyewe kutoa. Mazingira huweza sababisha ngono zembe Jeshini kwa maana ya kulazimisha kukubalika. La msingi ni ushauri kwa mabinti kuwa wavumilivu na kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni pamoja na kukubali kumaliza adhabu. Kuonewa pia hakupo kwani ni kosa kuonea. Vyuoni pia vijana wetu wanaweza toa ili wafaulu.
 
Kila lenye faida lina hasara zake pia. Kuna ambao wanakubali kuna ambao wanakataa kwamba JKT wasichana wanabakwa. Lakini ukweli utabaki pale pale kwamba mkufunzi akimtaka binti atamfanyia hila mpaka atafanikiwa kufanya nae mapenzi. Wanaopata shida hizi ni watoto wa mjini ambao wamelelewa maisha ya anasa, ambao hawajawahi kushika hata kisu, seuze jembe, panga n.k. watoto wenye mvuto wa sura huwa ndio hotcake kila mmoja anataka ampate yeye..!! Hakuna haja ya kukubali au kupinga, haya malalamiko yanasikiwa, tunaomba wahusika waichukue hii kama changamoto, wazidi kuboresha huduma, ili JKT iwe chombo bora, kwa maadili, ukakamavu na uzalendo wa wananchi wake.
 
Wanandugu kama una mtoto wa kike yuko mafunzoni ongea naye kabsa,,,,mambo ya kutafuta unafuu in exchange ya ngono aache,,,kwani watoto wa kike siku hizi hawaoni taabu yoyote kuuza mwili for a supid gain,tena mod huu uzi unaweza kuleta panic kubwa sana kwa wazazi, coz ukweli hakuna ubakaji wala nini,,ni uzushi wa hali ya juu sana.tena ukizushwa na watoto haohao wa shule ambao wana access na internet...pumbaf sana

wewe unaye mtoto wako huko? mimi nilipitia jeshini tena enzi hizo za Tanzania ya kweli. Enzi za zidumu fikra sahihi za mwenye kiti. Lakini, ubakaji ulikuwepo japo sisi tuliona ni kuonewa tu. Hivi leo, Piga tu! Imeruhusiwa, huyo afande atakaye poteza mda wa kutongoza ni wa wapi? Husikii yanayotokea huko Nt- wa- ra? Hata iwe nini, huko aende tu huyo binti lakini asinidanganye atakuwa salama. Hata akienda na salama box kumi. zitaisha tu.
 
wewe unaye mtoto wako huko? mimi nilipitia jeshini tena enzi hizo za Tanzania ya kweli. Enzi za zidumu fikra sahihi za mwenye kiti. Lakini, ubakaji ulikuwepo japo sisi tuliona ni kuonewa tu. Hivi leo, Piga tu! Imeruhusiwa, huyo afande atakaye poteza mda wa kutongoza ni wa wapi? Husikii yanayotokea huko Nt- wa- ra? Hata iwe nini, huko aende tu huyo binti lakini asinidanganye atakuwa salama. Hata akienda na salama box kumi. zitaisha tu.
Kama hali itakua mbaya zaidi ni bora mabinti zetu wakimaliza form 6 waolewe tu, watafanya kazi za kuuza maduka na mfano wa hayo, hizo ajira za serikali zinaelekea kupatikana ka ujira...
 
Hivi kwani wanalazimishwa kwenda JKT?
sasa why mtu uchague ujinga kama huu?
wazazi na hawa wanafunzi wana akili kweli?
sielewi kabisa
Yah, ni lazima boss, na suala la kwenda jeshini ni kwa mjibu wa sheria. Kutokana na taratibu walizoziweka, huwezi kuingia chuo kikuu bila ya kupitia jeshini. Majina ya waliohitimu JKT tu ndiyo yatakayofikiriwa kwenye udahili wa chuo kikuu. Hii ni kulingana na taarifa tulizopewa wakati huo.
 
Ndugu zangu, najua siyo utaratibu kuleta mjadala hapa kwa msingi wa habari zilizopo facebook. Nakubali kabisa kwamba JF si ya viwango vya facebook. Lakini nimeiona hii habari facebook, na kwa kuwa nina binti yangu yupo kambi ya JKT Tabora, pressure imenipanda na nimekosa amani kabisa.

Hebu wenye uzoefu na mambo ya huko watuambie ukweli upoje.

Habari yenyewe ni kama ifuatavyo:


[/FONT][/COLOR][/COLOR][/h]
MY TAKE: Tusijekuwa tumepeleka watoto wetu jeshini kwa kisingizio cha kuwafunza uzalendo, halafu mwisho wa siku wakarudi na HIV, na hasira kali dhidi ya nchi yao. Kama hili lina ukweli basi hii ni hali ya hatari sana kwa watoto wetu. Tunaweza kujikuta miaka mtano ijayo, 80% ya graduates wa vyuo vikuu ni wagonjwa wa UKIMWI. Ikumbukwe kwamba waliokwenda JKT ni wenye division one hadi three. Kwa maana ya kwamba ni cream ya nchi ndiyo imekwenda huko. Tutabaki na mamburula nchi hii, if this is true.

Mmm, nimetishika, na inawezakana ikawa kweli. Uchunguzi ufanyike, ngoja tuingie kazini, mimi naanzia Kambi ya Kimbiji,,kitaeleweka tu
 
Mmm, nimetishika, na inawezakana ikawa kweli. Uchunguzi ufanyike, ngoja tuingie kazini, mimi naanzia Kambi ya Kimbiji,,kitaeleweka tu
Thanks! Tafadhari usisahau kuja kutuletea report.
 
Back
Top Bottom