Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 78
WAKATI Chama cha Wananchi (CUF) kimepanga kufanya maandamano makubwa kuanzia Buguruni Sheli hadi kwenye Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, msajili huyo amepiga marufuku maandamano kufika katika maeneo ya ofisi hizo.
Taarifa za kupingana kwa taasisi hizo mbili zilitolewa jana kwa nyakati tofaiti na kila moja ikitoa sababu zake za kuchukua hatua husika.
Mapema asubuhi, Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ibrahim Lipumba alisema msimamo wao ni kumtaka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Jaji Lewis Makame ajiuzulu kutokana na kushindwa kuzuia na kuhakikisha uwajibikaji na uwazi kwenye taratibu za uchaguzi na kutaka tume hiyo ivunjwe na kuweka watu safi wenye kuijua demokrasia.
"Tutaendelea na maandamano hayo bila kuchoka na yatafanyika nchi nzima kwani tume imeshindwa kuunda asasi za kuhakikisha usalama na uwazi katika vipindi kadhaa vya uchaguzi hapa nchini." alisema Prof. Lipumba.
lakini ilipofika mchana, Msajili wa vyama vya siasa nchini, Bw. John Tendwa naye aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kueleza kuwa yupo tayari kupokea ujumbe wao katika maandamano yanayofanyika leo lakini wapange maeneo tofauti na viwanja vya eneo la ofisi yake.
Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa iko katika Barabara ya Mirambo, ikiwa takriban mita 300 kutoka kwenye geti la Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete, Ofisi ndogo ya Bunge na maeneo mengine nyeti ya serikali.
"Nimekubali kuwapokea lakini niliwataarifu kuwa eneo letu ni dogo na hapa tupo karibu na ofisi mbalimbali ikiwa ni Benk Kuu, Ofisi ndogo ya bunge, Shule ya Msingi, Wizara ya Fedha pamoja na Magereza, tunahitaji kulinda usalama," alisema Bw. Tendwa.
Alisema kuwa katika maandamano hayo si kila mmoja ana nia ya kufikisha ujumbe kama ulivyokusudiwa bali miongoni mwao wapo watu wanaoweza kufanya vurugu na kuvunja amani iliyopo.
"Katika msafara wa mamba hata kenge wamo, sisi tunaangalia usalama, pia kesho ni siku ya kazi, niliwashauri na pia ninaweka msisitizo kuwa tupo tayari kuwapokea mahali popote," alisema Bw. Tendwa
Alifafanua kwamba baada ya kupata taarifa kuwa wanataka kuandamana, aliamua kuwapa taarifa kuwa yupo tayari kukutana katika maeneo mbalimbali ya wazi ikiwa ni pamoja na eneo la Mnazi Mmoja, Kidongo chekundu pamoja na Jangwani lakini hakupata majibu yoyote.
"Tatizo la CUF ni kuwa namba wanazoziweka katika paper (nakala za machapisho) yao ukizipiga huwapati, mpaka umpigie mtu binafsi," alisema.
Wakati hayo yakiendelea, CUF kwa upande wake ilikuwa ikiendelea na maandalizi ya maandamano na Profesa Lipumba alipoulizwa msimamo wa Tendwa alisema hakuwa na taarifa nao lakini kijana wake alikuwa polisi akizungumzia suala hilo.
Imeandikwa na Prosper Mosha, Yusuph Katimba na Husna Ridhiwan
Taarifa za kupingana kwa taasisi hizo mbili zilitolewa jana kwa nyakati tofaiti na kila moja ikitoa sababu zake za kuchukua hatua husika.
Mapema asubuhi, Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ibrahim Lipumba alisema msimamo wao ni kumtaka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Jaji Lewis Makame ajiuzulu kutokana na kushindwa kuzuia na kuhakikisha uwajibikaji na uwazi kwenye taratibu za uchaguzi na kutaka tume hiyo ivunjwe na kuweka watu safi wenye kuijua demokrasia.
"Tutaendelea na maandamano hayo bila kuchoka na yatafanyika nchi nzima kwani tume imeshindwa kuunda asasi za kuhakikisha usalama na uwazi katika vipindi kadhaa vya uchaguzi hapa nchini." alisema Prof. Lipumba.
lakini ilipofika mchana, Msajili wa vyama vya siasa nchini, Bw. John Tendwa naye aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kueleza kuwa yupo tayari kupokea ujumbe wao katika maandamano yanayofanyika leo lakini wapange maeneo tofauti na viwanja vya eneo la ofisi yake.
Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa iko katika Barabara ya Mirambo, ikiwa takriban mita 300 kutoka kwenye geti la Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete, Ofisi ndogo ya Bunge na maeneo mengine nyeti ya serikali.
"Nimekubali kuwapokea lakini niliwataarifu kuwa eneo letu ni dogo na hapa tupo karibu na ofisi mbalimbali ikiwa ni Benk Kuu, Ofisi ndogo ya bunge, Shule ya Msingi, Wizara ya Fedha pamoja na Magereza, tunahitaji kulinda usalama," alisema Bw. Tendwa.
Alisema kuwa katika maandamano hayo si kila mmoja ana nia ya kufikisha ujumbe kama ulivyokusudiwa bali miongoni mwao wapo watu wanaoweza kufanya vurugu na kuvunja amani iliyopo.
"Katika msafara wa mamba hata kenge wamo, sisi tunaangalia usalama, pia kesho ni siku ya kazi, niliwashauri na pia ninaweka msisitizo kuwa tupo tayari kuwapokea mahali popote," alisema Bw. Tendwa
Alifafanua kwamba baada ya kupata taarifa kuwa wanataka kuandamana, aliamua kuwapa taarifa kuwa yupo tayari kukutana katika maeneo mbalimbali ya wazi ikiwa ni pamoja na eneo la Mnazi Mmoja, Kidongo chekundu pamoja na Jangwani lakini hakupata majibu yoyote.
"Tatizo la CUF ni kuwa namba wanazoziweka katika paper (nakala za machapisho) yao ukizipiga huwapati, mpaka umpigie mtu binafsi," alisema.
Wakati hayo yakiendelea, CUF kwa upande wake ilikuwa ikiendelea na maandalizi ya maandamano na Profesa Lipumba alipoulizwa msimamo wa Tendwa alisema hakuwa na taarifa nao lakini kijana wake alikuwa polisi akizungumzia suala hilo.
Imeandikwa na Prosper Mosha, Yusuph Katimba na Husna Ridhiwan