Naomba kujuzwa kuhusu neno sahihi na fasaha la "TENDO LA NDOA" ni lipi??
Naomba kujuzwa kuhusu neno sahihi na fasaha la "TENDO LA NDOA" ni lipi??
kwa mujibu wa kamusi ya kiswahili sanifu TUKI.
'Tia tupu ya kiume kwenye tupu ya kike katika kitendo cha kujamiiana'
tendo la ndoa ni kile kitendo cha kuacha kojoleo la kike kulimeza jienzie la kiume
Naomba kujuzwa kuhusu neno sahihi na fasaha la "TENDO LA NDOA" ni lipi??
Maneno "tendo la ndoa" katika muktadha wa matumizi ya lugha ni tafsida. Hutumika kuelezea dhana ya ashakumu kuingiliana kimwili baina ya watu wawili. Badala ya kutumia maneno makali tunayoyafahamu. Tafsida hii "tendo la ndoa" ilianza kutumika kushadidia ile dhana ya kimsingi kuwa tendo hilo ni mahsusi kwa watu ambao tayari wako kwenye ndoa tu. Nje ya ndoa tendo hilo huchukuliwa kimadili kuwa ni kosa. Kwa hiyo, hata likifanyika nje ya ndoa nadhani bado ni sahihi kuliita tendo la ndoa kama mtumiaji anakusudia kutumia tafsida. Sikubaliani na wale wanaosema kuwa litumike tu andapo kuna ndoa. Hapana, tuangalie muktadha wa chimbuko lake. Asante,