Uchaguzi 2020 TEF yamaliza Mgogoro wa TBC na CHADEMA, wapeana Mkono

TBC Waache tabia yao mbovu. Wakiwa kwenye mikutano ya wapinzani hawaonyeshi uwepo wa watu wanaosikiliza hizo hotuba tofauti na mikutano ya CCM
 
Daah yaani hii tume ya uchaguzi imeona hili la TBC na CDM ni la muhimu sanaaaaa kuliko issue ya msingi ya kukatwa kwa wagombea na wagombea wa chama kimoja tuu kupita bila kupingwa???
 
Huko ni kupoteza muda. Hao wajinga wa tbc wao waendelee tu na kutangaza kampeni za ccm maana ccm ndio inawalipa mishahara.
 
Naona TBCCM wanataka umaarufu kduniani kwa kurusha habari za Chadema. Chadema haibabaishwi kibwege, wamehangaika kuiua na kuitabiria kifo imeshindikana. Sasa wanataka suluhu mezani hata hivyo hatuwahitaji. Wameona I.T.V. ilipo rusha mahojiano na Tundu Lissu Dunia nzima imeangalia wamepata kiwewe ghafla.
 
Salaam Wakuu,

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limemaliza Mgogoro kati ya Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.

Hivi Karibuni CHADEMA iliwafukuza TBC kwenye Mkutano wao baada ya kuwa wanawakatia sauti kwenye Ufunguzi wao wa Kampeni.

Baadaye TBC wakatoa tamko kusitisha kuonesha habari za CHADEMA hadi watakapojirekebisha na kuwahakikishia usalama wa Wafanyakazi wao.

=====

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) leo Ijumaa Septemba 4, 2020 limefanikiwa kumaliza mgogoro uliokuwapo kati ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Shirika la Habari la Utangazaji Tanzania (TBC), baada ya kuwakutanisha viongozi wakuu wa taasisi hizo jijini Dar es Salaam, leo Ijumaaa Septemba 4, 2020. TEF kupitia kwa Kaimu Mwenyekiti wake, Deodatus Balile ilifanya mawasiliano na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayubu Ryoba, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Willison Mahera Charles, ambao wamekutana leo katika ofisi za NEC jijini Dar es Salaam kumaliza mgogoro huo.

Mkurugenzi wa Uchaguzi Dk. Mahera, wakati anafungua kikao hicho cha usuluhishi, amesema vyombo vya habari vya umma vinawajibika kutoa fursa sawa kwa vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha 53 (2) cha Sheria ya Uchaguzi ya Mwaka 2010, sambamba na Maadili ya Uchaguzi, Katiba ya Tanzania, Sheria mbalimbali na maelekezo ya Tume. Pia amesema vyama vya siasa na wafuasi wao wanawajibika kutii sheria za nchini kwa kuhakikisha wanalinda amani na utulivu. Amevitaka vyama vya siasa kuepuka kutoa tuhuma zisizo na uthibitisho kwenye mikutano ya kampeni.

Katika mkutano huo Mwenyekiti wa TEF, Balile ameeleza umuhimu wa vyombo vya habari kushirikiana na vyama vya siasa kwa kutimiza wajibu wake wa kitaaluma, lakini pia akafafanua umuhimu wa vyama vya siasa kushirikiana na vyombo vya habari hasa kipindi hiki cha kampeni kupata fursa ya kuhabarisha na kuelimisha jamii juu ya sera za vyama vyao katika majukwaa ya siasa. Amevitaka vyama kukosoana bila kutumia lugha ngumu au kuingia katika ugomvi binafsi na watu au matusi hali inayovipa wakati mgumu vyombo vinavyorusha matangazo ‘live’.

Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ryoba amelishukuru Jukwaa la Wahariri kwa juhudi za kuikutanisha TBC na Chadema, ila akaeleza masikitiko yake kuwa uamuzi wa Chadema kufukuza waandishi wao katika mkutano wa ufunguzi wa Kampeni, Mbagala wiki iliyopita ulikuwa unahatarisha maisha ya waandishi na mali za shirika. Pia amesema hatua ya Chadema ililenga kubomoa kiwango cha TBC kuaminika mbele ya jamii, suala ambalo ni gharama kubwa kwa chombo cha habari. Hata hivyo amekiri upungufu uliofanywa na watangazaji siku hiyo kwa jinsi matangazo yaliyokatwa na mjadala ulioendelea studio, hivyo akasema shirika litajitahidi kutorudia makosa yaliyojitokeza.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameeleza historia ya uhusiano wa TBC na Chadema kwamba kwa muda mrefu umekuwa si mzuri na akasema hata baadhi ya vyombo vya habari binafsi vinakataa kurusha matangazo ya shughuli za chama chao hata kama kinalipia kwa maelezo kuwa vimepewa maelekezo. Mbowe ameviomba vyombo vya habari kufanya kazi kwa weledi na kwa mujibu wa sheria, hasa katika kipindi hiki cha kampeni.

Baada ya mjadala mrefu, Dk. Ryoba na Mbowe walikubaliana kumaliza tofauti zao kwa kupeana mikono na kuahidi kurejesha ushirikiano. Mbowe amesema atawatangazia wanachama wa Chadema kuwa wako tayari kufanya kazi na TBC kuanzia sasa. Dk. Ryoba amesema Chadema wawapatie TBC ratiba ya mikutano yao watashiriki kikamilifu kuitangaza. Pia, amemwabia Mbowe kuwa TBC ina kipindi cha nusu saa kila wiki kwa wagombea kunadi sera zao kinachorushwa bila malipo, hivyo akawaalika Chadema kuitumia fursa hiyo, ambapo Mbowe amekubali kuitumia.

Akifunga kikao, Mkurugenzi wa Uchaguzi Dk. Mahera aliyekuwa Mwenyekiti wa kikao hicho, ameishukuru TEF kwa juhudi ilizofanya kuwakutanisha TBC na Chadema na akaviomba vyama vya siasa nchini kufanya kampeni za kistaarabu kwa kutambua kuwa kuna maisha baada ya uchaguzi. Dk. Ryoba, Mbowe, Dk. Mahera na Balile wamepeana mikono kuashiria kufungua ukurasa mpya na wakaahidi kumaliza migogoro kati ya vyombo vya habari na vyama vya siasa au wanasiasa nchini kwa njia ya mazungumzo badala ya kutegemea sheria pekee katika kipindi hiki cha uchaguzi.

IMETOLEWA NA JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA (TEF) DAR ES SALAAM, SEPTEMBA 4, 2020

NEVILLE MEENA

KATIBU


View attachment 1558585View attachment 1558604View attachment 1558605View attachment 1558607View attachment 1558608
Heri ya mpatanishi. Ila TBC wajirekebishe.
 
kwani bila tbc siasa hazifanyiki? hakuna haja ya suluhu wao wafanye kazi za Ccm..chadema wameanza udhaifu sasa
 
Muda aliopoteza Mbowe kwenda kupatana na TBC bora angeutumia kwa kufanya jambo jingine, kama Mimi ni muongo basi mtasubiri sana.

Mmoja wa wagombea wa chama kimojawapo ndiye aliyewatuma TBC wawahujumu CHADEMA kwa makombora yanayorushwa na mzee baba sidhani kama yataruhusiwa kupaa angani.

Mfano kwa waliofuatilia kampeni za CHADEMA jana sidhani kama zilirushwa hewani na TBC.
 
Jana kwenye Mkutano wa uzinduzi wa kampeni za NCCR-Mageuzi, kila Mbatia na Maganja walipokuwa wanatema cheche kuhusu upendeleo wa Tume ya uchaguzi na uharamia unaofanywa na serikali hususani kipindi hiki cha uchaguzi hao TBC wakawa wanafanya ile mnaita censoring, na kucheza nyimbo za uchaguzi. Kweli naunga mkono hoja, hayo mapatano hayatadumu hata kidogo
 
Jana kwenye Mkutano wa uzinduzi wa kampeni za NCCR-Mageuzi, kila Mbatia na Maganja walipokuwa wanatema cheche kuhusu upendeleo wa Tume ya uchaguzi na uharamia unaofanywa na serikali hususani kipindi hiki cha uchaguzi hao TBC wakawa wanafanya ile mnaita censoring, na kucheza nyimbo za uchaguzi. Kweli naunga mkono hoja, hayo mapatano hayatadumu hata kidogo
Hao ni ccm b.
 
Muda aliopoteza Mbowe kwenda kupatana na TBC bora angeutumia kwa kufanya jambo jingine, kama Mimi ni muongo basi mtasubiri sana.

Mmoja wa wagombea wa chama kimojawapo ndiye aliyewatuma TBC wawahujumu CHADEMA kwa makombora yanayorushwa na mzee baba sidhani kama yataruhusiwa kupaa angani.

Mfano kwa waliofuatilia kampeni za CHADEMA jana sidhani kama zilirushwa hewani na TBC.
Kiukweki nafasi ya Mbowe angeipata Heche..unajipendekeza kwa bwanyenye Hilo ili iweje? Aisee
 
Back
Top Bottom