TCU, sio kila Professor anaweza kuwa VC wa chuo

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,305
12,600
Vyuo vyetu vikuu vina idadi ndogo ya maprofesa, na wale wachache waliopo sio kweli wote wanazo sifa za kushika nafasi ya u vice chancellor, maNaibu Makamu wakuu wa chuo taaluma na mipango na fedha, au kuwa mkuu wa idara au Mkuu wa kitivo. Nafasi hizi zinahitaji maarifa na sifa ambazo ni zaidi ya kuwa na PhD na PROFESSOR tu.

Vyuo vingi vikuu vina rasilimali chache sana kumudu kusomesha, kuajili na kuwalipa wafanyakazi wenye PhD na professors wengi wa kutosha ili kupata wigo mpana wa kuchagua Kati yao wenye sifa za ziada za kuuongoza chuo, na vitengo vya ki utawala vyuoni. Waliopo wanaweza tu kufundisha lakini hawana sifa za kuongoza, ndiyo maana vyuo vingi havisongi mbele, vinategemea Ada za wanafunzi kujiendesha.

Vyuo Sasa ili kuendana na mashariti ya TCU ya kuwa lazima kuwa na viongozi MAPROFESA vinalazimika kuzoazoa yeyote mwenye PhD /professor ili kufunika kombe mwanaharamu apite.

Vyuo vingi hasa binafsi vimejaza maprofesa wazee sana na wasiokuwa na mawazo mapya na kusababisha vyuo kudumaa na Kutegemea Ada kwakuwa wametoka vyuo vya Serikali ambavyo Serikali inalipa kila kitu.

Serikali saidieni vyuo binafsi katika:
1. Kusomesha walimu wao wengi ngazi ya masters na PhD.

2. Saidieni kulipa mishahara ya maprofesa (vijana) vyuoni.

3. Sio lazima nafasi za uongozi vyuoni zishikwe na maprofesa tu, uprofessa uwe ni added advantage baada ya sifa nyingine za uongozi kutimia.

4. Vyuo viwe na idadi maalum ya watumishi waliostaafu, sio idara nzima ni wastaafu tu, wengi wa wastaafu wetu jawawezi kufundisha siku zote na vipindi vyote kwenye wiki, mwezi na mhula kutokana na shida mbalimbali za kiafya na kijamii.
 
Mawazo mazuri Sana ukuzingatia Na umasikini.wa vyuo vyetu havina ubunifu wowote wa kubuni miradi itakayosaidia chuoni kujiendesha
 
Mawazo mazuri Sana ukuzingatia Na umasikini.wa vyuo vyetu havina ubunifu wowote wa kubuni miradi itakayosaidia chuoni kujiendesha
Viongozi watendaji wakuu wazee vyuoni ni chanzo cha kudumaa kwa vyuo, ubunifu kwao unapungua, hawataki ku risk, sïo waumini wa changes, Wanaamini na kulinda kile wanachokijua, present is known and secure. Sio ma entrepreneurs katika industry. Wazee hawa ni muhimu sana kwenye kutoa ujuzi /kufundisha kwa vijana lakini sio kwenye uongozi. Vyuo hivi utavikuta chancellor, vice chancellor, DVC-ARC, DVCPFA, DEAN'S, DIRECTORS, NA WAKUU WA IDARA WOTE ni wazee, muda mwingi ama wanaumwa kwenye clinic za magonjwa ya uzee, safari nyingi, wanasinsia ofisini, ama wanawaza wajukuu zao na miradi yao binafsi. Hakuna ubunifu kwenye hivi vyuo, wanakwenda kwa minimums za TCU tu.
 
Mawazo mazuri Sana ukuzingatia Na umasikini.wa vyuo vyetu havina ubunifu wowote wa kubuni miradi itakayosaidia chuoni kujiendesha
Ni makosa makubwa kudhani kila professor anaweza kuwa kiongozi, waziri, Rais, mkurugenzi, Mkuu wa kitengo, nk. Maprofesa waende kwenye maeneo yao ya ubobezi sio uongozi
 
Point yako n nn hasa? Ngumbaru tumejaa chuki
Pont kuu hapa vyuo vijengewe uwezo wa makusudi wa kusomesha watumishi wao wengi wawe na PhD na kufanya tafiti badala ya kutegemea vikongwe. Kila zama Ina Kitabu chake. Pili, sio kila professor anafaa kuwa kiongozi. Wako maprofesa ambao hawafai kuwa hata wajumbe wa nyumba 10 lakini wanaingoza vitengo kwakuwa Kuna mtu kasema lazima kiongozi wa kitengo lazima awe professor na hakuna professor mwingine pale ila yeye TU.

Umenipata Sasa?
 
Ni makosa makubwa kudhani kila professor anaweza kuwa kiongozi, waziri, Rais, mkurugenzi, Mkuu wa kitengo, nk. Maprofesa waende kwenye maeneo yao ya ubobezi sio uongozi
Sio kweli Prof au Dr. ni mtu mwenye uelewa mkubwa sana ndio maana Yupo katika hiyo nafasi. Wewe kama hutaki kusoma ni bora utulie kwenye nafasi zako hizo hizo tumeelewana. You dont become Prof because you don't qualify come down man. Wewe na kibachelor chako ndio tukupe UVC come on bora utulie tu..
 
Sio kweli Prof au Dr. ni mtu mwenye uelewa mkubwa sana ndio maana Yupo katika hiyo nafasi. Wewe kama hutaki kusoma ni bora utulie kwenye nafasi zako hizo hizo tumeelewana. You dont become Prof because you don't qualify come down man. Wewe na kibachelor chako ndio tukupe UVC come on bora utulie tu..
Anaepaswa kuwa na PhD/Professor ni mwalimu/mkufunzi/mtaaluma wa somo husika, sio kiongozi. Kama ni hivyo Rais na mawaziri wangestahili kuwa maprofessor tu basi. Kiongozi ni yule mtu mwenye maono, PhD haifundishi kuwa na maoni bali utafiti tu basi. wewe ni mfano wa watu ambao hu\awajaelimika bali wamesoma.
 
Anaepaswa kuwa na PhD/Professor ni mwalimu/mkufunzi/mtaaluma wa somo husika, sio kiongozi. Kama ni hivyo Rais na mawaziri wangestahili kuwa maprofessor tu basi. Kiongozi ni yule mtu mwenye maono, PhD haifundishi kuwa na maoni bali utafiti tu basi. wewe ni mfano wa watu ambao hu\awajaelimika bali wamesoma.
Hata ungejipa moyo, sisi tutaendelea kutumia Drs and Professors kwenye mambo yetu.
 
Hata ungejipa moyo, sisi tutaendelea kutumia Drs and Professors kwenye mambo yetu.
Wizara hazitoi matokeo hata chini ya mawaziri maprofesa, wizara zinatoa matokeo hata chini ya mawaziri wenye diploma tu. Uongozi ni zaidi ya kuwa na PhD. Waliotaka kuiuza Kigamboni walikuwa na maprofesa.
 
Wizara hazitoi matokeo hata chini ya mawaziri maprofesa, wizara zinatoa matokeo hata chini ya mawaziri wenye diploma tu. Uongozi ni zaidi ya kuwa na PhD. Waliotaka kuiuza Kigamboni walikuwa na maprofesa.
Kama huna elimu kaongezee tu badala ya kulalamika hiyo ndio faida ya serikali kusomesha watu wake.
 
Kama huna elimu kaongezee tu badala ya kulalamika hiyo ndio faida ya serikali kusomesha watu wake.
Elimu ninayo tele lakini hiyo haitoshi kuacha kusema ukweli kuhusu dhana halisi ya administration na management kwenye taasisi zetu za elimu. Unafahamu kuwa siku hizi hata PhD zinanunuliwa? Hoja hapa ni tuwe na maprofesa wengi vyuoni ili miongoni mwao wenye sifa za kuongoza washike nafasi za uongozi na sio kudhani kila professor au PhD anafaa kuongoza wengine. Mbaya zaidi inatokea kuwa professor hana sifa za kiongozi na ni mzee wa kutupwa/mstaafu. Huyu hata kumpa continuous education kuhusu uongozi haiwezekani, they do not penda mabadiliko, kwake yeye "present is known and secure"
 
Elimu ninayo tele lakini hiyo haitoshi kuacha kusema ukweli kuhusu dhana halisi ya administration na management kwenye taasisi zetu za elimu. Unafahamu kuwa siku hizi hata PhD zinanunuliwa? Hoja hapa ni tuwe na maprofesa wengi vyuoni ili miongoni mwao wenye sifa za kuongoza washike nafasi za uongozi na sio kudhani kila professor au PhD anafaa kuongoza wengine. Mbaya zaidi inatokea kuwa professor hana sifa za kiongozi na ni mzee wa kutupwa/mstaafu. Huyu hata kumpa continuous education kuhusu uongozi haiwezekani, they do not penda mabadiliko, kwake yeye "present is known and secure"
Sasa si wanalipa hela, hata diploma zinanunuliwa hata bachelor, kila kitu bila pesa huwezi Ku kupata. Ile tution fees unayolipia ndio bei yenyewe ya kununulia sasa kama mtu amenunua PhD kwa fedha yake mwache ale vyake. All in all kupata PhD sio kazi nyepesi kama unavyofikiria ndio maana wenye PhD ni wachache Tanzania. Mimi naona uwaache tu.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Sasa si wanalipa hela, hata diploma zinanunuliwa hata bachelor, kila kitu bila pesa huwezi Ku kupata. Ile tution fees unayolipia ndio bei yenyewe ya kununulia sasa kama mtu amenunua PhD kwa fedha yake mwache ale vyake. All in all kupata PhD sio kazi nyepesi kama unavyofikiria ndio maana wenye PhD ni wachache Tanzania. Mimi naona uwaache tu.
Hahaha, kweli elimu imeshuka, your reasoning is too weak to be considered one of the elites we have.
 
Vyuo vyetu vikuu vina idadi ndogo ya maprofesa, na wale wachache waliopo sio kweli wote wanazo sifa za kushika nafasi ya u vice chancellor, maNaibu Makamu wakuu wa chuo taaluma na mipango na fedha, au kuwa mkuu wa idara au Mkuu wa kitivo. Nafasi hizi zinahitaji maarifa na sifa ambazo ni zaidi ya kuwa na PhD na PROFESSOR tu.

Vyuo vingi vikuu vina rasilimali chache sana kumudu kusomesha, kuajili na kuwalipa wafanyakazi wenye PhD na professors wengi wa kutosha ili kupata wigo mpana wa kuchagua Kati yao wenye sifa za ziada za kuuongoza chuo, na vitengo vya ki utawala vyuoni. Waliopo wanaweza tu kufundisha lakini hawana sifa za kuongoza, ndiyo maana vyuo vingi havisongi mbele, vinategemea Ada za wanafunzi kujiendesha.

Vyuo Sasa ili kuendana na mashariti ya TCU ya kuwa lazima kuwa na viongozi MAPROFESA vinalazimika kuzoazoa yeyote mwenye PhD /professor ili kufunika kombe mwanaharamu apite.

Vyuo vingi hasa binafsi vimejaza maprofesa wazee sana na wasiokuwa na mawazo mapya na kusababisha vyuo kudumaa na Kutegemea Ada kwakuwa wametoka vyuo vya Serikali ambavyo Serikali inalipa kila kitu.

Serikali saidieni vyuo binafsi katika:
1. Kusomesha walimu wao wengi ngazi ya masters na PhD.

2. Saidieni kulipa mishahara ya maprofesa (vijana) vyuoni.

3. Sio lazima nafasi za uongozi vyuoni zishikwe na maprofesa tu, uprofessa uwe ni added advantage baada ya sifa nyingine za uongozi kutimia.

4. Vyuo viwe na idadi maalum ya watumishi waliostaafu, sio idara nzima ni wastaafu tu, wengi wa wastaafu wetu jawawezi kufundisha siku zote na vipindi vyote kwenye wiki, mwezi na mhula kutokana na shida mbalimbali za kiafya na kijamii.
University ni taassis ya elimu ya juu kabisa duniani na vyuo vyote duniani Kwa nafasi hizo muhimu viongozi wa juu huwa ni PhD au full Professor. Kwa mawazo yako unataka mtu yeyote Yule anayejua kusoma na kuandika kupewa kuongoza Taasis za elimu ya juu haitawezekana. ungetoa ushauri kwamba vyuo na serikali viweke mikajati ya kuandaa ma Dr na maprofessor wengi . Kwa mfano SUA ilikuepo ni chuo chenye ma Dr na Prof wengi Ila asimilia kubwa sasa ni retired na hawakuwekeza kuandaa replacement lecture hiyo ndio problem ya Tanzania.
 
Vyuo vyetu vikuu vina idadi ndogo ya maprofesa, na wale wachache waliopo sio kweli wote wanazo sifa za kushika nafasi ya u vice chancellor, maNaibu Makamu wakuu wa chuo taaluma na mipango na fedha, au kuwa mkuu wa idara au Mkuu wa kitivo. Nafasi hizi zinahitaji maarifa na sifa ambazo ni zaidi ya kuwa na PhD na PROFESSOR tu.

Vyuo vingi vikuu vina rasilimali chache sana kumudu kusomesha, kuajili na kuwalipa wafanyakazi wenye PhD na professors wengi wa kutosha ili kupata wigo mpana wa kuchagua Kati yao wenye sifa za ziada za kuuongoza chuo, na vitengo vya ki utawala vyuoni. Waliopo wanaweza tu kufundisha lakini hawana sifa za kuongoza, ndiyo maana vyuo vingi havisongi mbele, vinategemea Ada za wanafunzi kujiendesha.

Vyuo Sasa ili kuendana na mashariti ya TCU ya kuwa lazima kuwa na viongozi MAPROFESA vinalazimika kuzoazoa yeyote mwenye PhD /professor ili kufunika kombe mwanaharamu apite.

Vyuo vingi hasa binafsi vimejaza maprofesa wazee sana na wasiokuwa na mawazo mapya na kusababisha vyuo kudumaa na Kutegemea Ada kwakuwa wametoka vyuo vya Serikali ambavyo Serikali inalipa kila kitu.

Serikali saidieni vyuo binafsi katika:
1. Kusomesha walimu wao wengi ngazi ya masters na PhD.

2. Saidieni kulipa mishahara ya maprofesa (vijana) vyuoni.

3. Sio lazima nafasi za uongozi vyuoni zishikwe na maprofesa tu, uprofessa uwe ni added advantage baada ya sifa nyingine za uongozi kutimia.

4. Vyuo viwe na idadi maalum ya watumishi waliostaafu, sio idara nzima ni wastaafu tu, wengi wa wastaafu wetu jawawezi kufundisha siku zote na vipindi vyote kwenye wiki, mwezi na mhula kutokana na shida mbalimbali za kiafya na kijamii.
Saaa kama umeshindwa kufanya tafiti na kuwa prof utaweza kukisogeza chuo mbele?

Nakubaliana na wewe kwamba wazee wapumzike lakini VC au uongozi wowote wa chuo au department lazima mtu awe na PhD!

Huwezi mpa Dr u VC wakati kuna maprofesa! Hiyo haiwezekaniki!
 
Back
Top Bottom