Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
NINAOMBA UFAFANUZI WA KINA KUTOKA KWA WATAALAM WA ICT PAMOJA NA TELECOMMUNICATION ENGINEERS.
Shikamooni wakubwa zangu wote wa humu jamiiforums. Mimi mdogo wenu Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty. Leo swali langu lipo kama ifuatavyo?
Kwanini "fingerprint scanners/censors" zilizopo nyuma ya "smartphones" zetu hazitumiki katika zoezi linaloendelea la kusajili upya wa simcards?
Kwanini mtu afunge safari kutoka point A kwenda point B kisha akawasilisha number ya NIDA pekee kisha alama ya kidole chake ikawa matched na ile alama ya kwenye computers servers za NIDA kisha akaambiwa kuwa umekamilisha zoezi?
Kwanini hakuna uwezekana wa kuwa na Android App ambayo itakuwa linked ikawa ina communicate na severs za NIDA, Service Provider husika pamoja na Fingerprint sensor ya kwenye smartphone kisha mtu akajifanyia usajili yeye mwenyewe akiwa sehemu yenye network coverage nzuri?
Au Kwanini "fingerprint censors" zilizopo nyuma ya hizi "smartphones" zetu haziwezeshwi kutumika katika kutengeneza accounts pamoja na ku-login katika mitandao ya kijamii (Twitter, Facebook, Jamiiforums) ili sasa tuachane na masuala ya mtu kusahau passwords pamoja na emails?
Unaweza ukakuta mtu anamiliki accounts kadhaa katika mitandao tofauti ya kijamii pamoja na emails pia, ila kila account ina password yake hivyo inakuwa ni rahisi sana kwa mtu kuweza kusahau moja kati ya credentials hizo.
OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.