LIKUD
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 15,121
- 27,128
Moja kati ya kazi za TCRA ni pamoja na kuregulate na kusimamia huduma za mawasiliano zinazo tolewa na kampuni mbalimbali za mawasiliano nchini Tanzania, ikiwemo kampuni ya TIGO.
Pamoja na hayo, kampuni ya TIGO kupitia huduma ya TIGOPESA wamekuwa wakifanya utapeli na ubabaishaji wa hali ya juu sana kwa watumiaji wa huduma ya tigopesa.
Mfano mzuri ni huu hapa kwangu. Siku ya tarehe 05 mwezi wa SABA , 2017 nilifanya muamala wa pesa kupitia TIGOPESA
Bahati mbaya, wakati natoa pesa, nilikosea namba moja na pesa ikatoka kwa wakala mwingine wa tigo. ( MESEJI ZOTE NINAZO )...
NILIPO WAPIGIA SIMU TIGO, WAKASEMA HIYO PESA WAMEIZUIA NA KWAMBA, ITAREJESHWA NDANI YA MASAA ISHIRINI NA NNE.
Baada ya masaa ishirini na nne kupita nikawapigia simu tena kuwauliza, wakaniambia suala lako linashughulikiwa subiri masaa ishirini na nne.
Yakapita masaa ishirini na nne bila kunirudishia pesa yangu.Nikawapigia tena. Wakaniambia kuwa siku hiyo ilikuwa siku ya Jumamosi na kwamba ( HAWAFANYI KAZI KWA SABABU SIO SIKU YA KAZI )nikaambiwa nisubiri hadi siku ya Jumatatu.
Siku ya Jumatatu nilivyo wapigia simu,.wakaniambia tena nisubiri ndani ya masaa ishirini na nne. Baada ya masaa ishirini na nne hola,hawakunitumia pesa yangu.
Hali hii iliendelea kwa muda wa wiki mbili mfululizo.Ilifikia kipindi baadhi ya wahudumu wakawa wamenikariri, kila nikipiga simu na kujitambulisha, wananikatia simu....
Nilivyo ona watoa huduma ya TIGOPESA wananidanganya, nikaamua kwenda mimi mwenyewe makao makuu ya TIGO pale Kijitonyama..Napo wakaniambia, wanashughulikia tatizo langu niende watanirudishia pesa yangu ndani ya masaa ishirini na nne..
Nikarudi nyumbani , siku tatu zikapita bila kunirudishia pesa yangu...
Nikarudi tena ofisi za TIGO na kuomba kuongea na Meneja.. Wakaniambia Meneja hayupo... Nikawaambia nataka kuongea na msaidizi wake, nikajibiwa na yeye hayupo, wote wameenda kwenye kikao...
Nikiwa ofisini hapo, niligundua kuwa wenye tatizo kama langu wapo wengi sana na wote hela zao wametapeliwa na tigo pesa..
NINAWAOMBA TCRA MTUSAIDIE WANANCHI TULIO IBIWA NA KUTAPELIWA NA TIGO TUWEZE KUPATA HAKI YETU KWA WAKATI...
Pamoja na hayo, kampuni ya TIGO kupitia huduma ya TIGOPESA wamekuwa wakifanya utapeli na ubabaishaji wa hali ya juu sana kwa watumiaji wa huduma ya tigopesa.
Mfano mzuri ni huu hapa kwangu. Siku ya tarehe 05 mwezi wa SABA , 2017 nilifanya muamala wa pesa kupitia TIGOPESA
Bahati mbaya, wakati natoa pesa, nilikosea namba moja na pesa ikatoka kwa wakala mwingine wa tigo. ( MESEJI ZOTE NINAZO )...
NILIPO WAPIGIA SIMU TIGO, WAKASEMA HIYO PESA WAMEIZUIA NA KWAMBA, ITAREJESHWA NDANI YA MASAA ISHIRINI NA NNE.
Baada ya masaa ishirini na nne kupita nikawapigia simu tena kuwauliza, wakaniambia suala lako linashughulikiwa subiri masaa ishirini na nne.
Yakapita masaa ishirini na nne bila kunirudishia pesa yangu.Nikawapigia tena. Wakaniambia kuwa siku hiyo ilikuwa siku ya Jumamosi na kwamba ( HAWAFANYI KAZI KWA SABABU SIO SIKU YA KAZI )nikaambiwa nisubiri hadi siku ya Jumatatu.
Siku ya Jumatatu nilivyo wapigia simu,.wakaniambia tena nisubiri ndani ya masaa ishirini na nne. Baada ya masaa ishirini na nne hola,hawakunitumia pesa yangu.
Hali hii iliendelea kwa muda wa wiki mbili mfululizo.Ilifikia kipindi baadhi ya wahudumu wakawa wamenikariri, kila nikipiga simu na kujitambulisha, wananikatia simu....
Nilivyo ona watoa huduma ya TIGOPESA wananidanganya, nikaamua kwenda mimi mwenyewe makao makuu ya TIGO pale Kijitonyama..Napo wakaniambia, wanashughulikia tatizo langu niende watanirudishia pesa yangu ndani ya masaa ishirini na nne..
Nikarudi nyumbani , siku tatu zikapita bila kunirudishia pesa yangu...
Nikarudi tena ofisi za TIGO na kuomba kuongea na Meneja.. Wakaniambia Meneja hayupo... Nikawaambia nataka kuongea na msaidizi wake, nikajibiwa na yeye hayupo, wote wameenda kwenye kikao...
Nikiwa ofisini hapo, niligundua kuwa wenye tatizo kama langu wapo wengi sana na wote hela zao wametapeliwa na tigo pesa..
NINAWAOMBA TCRA MTUSAIDIE WANANCHI TULIO IBIWA NA KUTAPELIWA NA TIGO TUWEZE KUPATA HAKI YETU KWA WAKATI...