TCRA kujenga kiwanda cha kutengeneza simu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,875
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA, ina mpango wa kujenga kiwanda cha kutengeneza simu nchini ili kuweza kurahisisha upatikanaji wa ajira kwa wahitimu kwa ngazi ya Ufundi stadi nchini pamoja na kufanya usalama wa mawasiliano.

Hayo yamesemwa leo na Mwakilikishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA ambaye Mkurugenzi wa Leseni na Ufuatiliaji kutoka John Daffa Wakati wa mahafali ya Tisa ya Chuo cha Teknolojia ya Habari na Mawasilino TEHAMA VETA, kilichopo Kipawa Jijini Dar es salaam ambapo zaidi ya wanafunzi 200 wamehitimu kutoka kwenye Taaluma mbalimbali yenye mchepuo wa TEHAMA .

Amesema kuwa katika Chuo hicho wameweza kudhamini mafundi simu kupata ujuzi Pamoja na kuwapa Leseni ili kazi hiyo iweze kutambuliwa kwa mfumo rasmi.

"Ujenzi wa kiwanda hicho unatazamiwa kuanza mwakani ikiwa lengo ni kusaidia kupunguza ajira na kuchochea maendeleo ya nchi ambayo ajenda ya serikali kwenda katika uchumi wa viwanda ambapo wanufaika wakuu wakiwa ni wahitimu kutoka VETA". Amesema .Daffa.

Aidha amesema TCRA inampango wa kuondoa mafundi vishoka wa kutengeneza simu kwani wameshaanza kutoa leseni kwa wategenezaji wa simu kwa ambao wamekidhi vigezo kutoka vyuo husika ambavyo ni VETA na Taasisi ya Teknolojia (DIT) ndio watatambulika.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha VETA Kipawa Mhandisi Dickson Mkasanga, amesema kuwa ujio wa kiwanda cha kutengeneza simu kwao utaongeza wigo mkubwa wa kutoa elimu huku akidai kuongeza idadi ya wanafunzi kwa mwaka ujao wa masomo katika Chuo hicho.

Aidha Mhandisi Mkasanga amesema Chuo hicho kilifanikiwa kudahili wanafunzi 125 katika mafunzo ya muda mrefu kwenye fani mbalimbali kama vile umeme, Tehama na Elektroniki wahitimu 121 (wanawake 27 na wanaume 94).

Pamoja na hayo ameiomba TCRA kuhamasisha makampuni ya simu kama vile Samsung,Nokia Tecno, Huawei kutumia chuo hicho kwa kupeleka vifaa vya simu, tehama na elektroniki kwaajili ya mafunzo kwa vitendo ambapo itakuwa ni msaada kwa mafundi na wanachuo kwa ujumla.

Hata hivyo katika changamoto amesema gharama kubwa ya upatikanaji wa vifaa vya kiteknolojia kunapunguza kasi ya chuo hicho kuweza kutoa mafunzo yanayohitajika kwenye soko kwa wakati.

Vifaa vipo lakini tunatakiwa kutumia mashine za kisasa kutokana na teknolojia zinabadilika kila kukicha hivyo kutumia vifaa vilivyopitwa na wakati kufundishia kunaathiri ubora wa ujuzi anaoupata mwanafunzi ukilinganisha na mahitaji ya soko". Amesema Mhandisi Mkasanga.

Awali wakisoma Risala wahitimu wa chuo hicho wamiomba TCRA kuwasidia kuwatatulia baadhi ya changamoto zinazokikabili chuo hicho ikiwemo mabadiliko ya mitaala kuendana na kasi ya sayansi na Teknolojia,Muendelezo wa kozi ndefu,Upungufu wa vitabu kwenye Library ya chuo,Ukosefu wa vimbweta na Kukosekana kwa maeneo ya kufanyia mafunzo ya vitendo.

Nae Bw.Nelson Rutter akiongea kwa niaba ya wazazi amewataka wahitimu kuwa na nidhamu kazini ama kwa wateja wao ili kuweza kuunda uwaminifu kwani b aadhi ya mafundi wamekuwa si waaminfu kwa wateja wao.

Chuo cha TEHAMA cha VETA –kipawa ni moja kati ya vyuo vilivyopo nchini vinavyomilikiwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), ambacho ni chuo cha mfano kinachotoa mafunzo mbalimbali yenye mchepuo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
 
swala la kuanzisha kiwanda cha simu sio swala la kitoto.
Kwanza kupata jina ambalo linaweza kushindana na na tekno infnix itel kwa afrika masharik. Na pili je unaweza kushindana vip kidunia na samasung iphone huawei sony lg nk.

Pili je ni kitu gani ambacho kimekosekana sokoni ambacho wataenda kutatua kiwada cha simu kutoka Tanzania ikiwa blackberry walishindwa hadi saizi blackberry na viwanda vingi tu vya simu vimeacha kutengeneza simu.

Tatu serikali hiyo biashara itaweiza vip ikiwa hakuna biashara ambayo imewahi kufanya serikali na ikawafanikiwa. Kwa mfano tanesco shilika la ndege nk
Kila siku wanapata hasara mabilion ya shililingi.
 
ooh....kumbe ni kurekebisha na sio kutengeneza maana naona wanahitaji msaada wa kina tecno na nduguze.
 
swala la kuanzisha kiwanda cha simu sio swala la kitoto.
Kwanza kupata jina ambalo linaweza kushindana na na tekno infnix itel kwa afrika masharik. Na pili je unaweza kushindana vip kidunia na samasung iphone huawei sony lg nk.

Pili je ni kitu gani ambacho kimekosekana sokoni ambacho wataenda kutatua kiwada cha simu kutoka Tanzania ikiwa blackberry walishindwa hadi saizi blackberry na viwanda vingi tu vya simu vimeacha kutengeneza simu.

Tatu serikali hiyo biashara itaweiza vip ikiwa hakuna biashara ambayo imewahi kufanya serikali na ikawafanikiwa. Kwa mfano tanesco shilika la ndege nk
Kila siku wanapata hasara mabilion ya shililingi.
ni kutengeneza yaan kama simu ni mbovu unaipeleka wanatengeneza
 
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA, ina mpango wa kujenga kiwanda cha kutengeneza simu nchini ili kuweza kurahisisha upatikanaji wa ajira kwa wahitimu kwa ngazi ya Ufundi stadi nchini pamoja na kufanya usalama wa mawasiliano.

Hayo yamesemwa leo na Mwakilikishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA ambaye Mkurugenzi wa Leseni na Ufuatiliaji kutoka John Daffa Wakati wa mahafali ya Tisa ya Chuo cha Teknolojia ya Habari na Mawasilino TEHAMA VETA, kilichopo Kipawa Jijini Dar es salaam ambapo zaidi ya wanafunzi 200 wamehitimu kutoka kwenye Taaluma mbalimbali yenye mchepuo wa TEHAMA .

Amesema kuwa katika Chuo hicho wameweza kudhamini mafundi simu kupata ujuzi Pamoja na kuwapa Leseni ili kazi hiyo iweze kutambuliwa kwa mfumo rasmi.

"Ujenzi wa kiwanda hicho unatazamiwa kuanza mwakani ikiwa lengo ni kusaidia kupunguza ajira na kuchochea maendeleo ya nchi ambayo ajenda ya serikali kwenda katika uchumi wa viwanda ambapo wanufaika wakuu wakiwa ni wahitimu kutoka VETA". Amesema .Daffa.

Aidha amesema TCRA inampango wa kuondoa mafundi vishoka wa kutengeneza simu kwani wameshaanza kutoa leseni kwa wategenezaji wa simu kwa ambao wamekidhi vigezo kutoka vyuo husika ambavyo ni VETA na Taasisi ya Teknolojia (DIT) ndio watatambulika.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha VETA Kipawa Mhandisi Dickson Mkasanga, amesema kuwa ujio wa kiwanda cha kutengeneza simu kwao utaongeza wigo mkubwa wa kutoa elimu huku akidai kuongeza idadi ya wanafunzi kwa mwaka ujao wa masomo katika Chuo hicho.

Aidha Mhandisi Mkasanga amesema Chuo hicho kilifanikiwa kudahili wanafunzi 125 katika mafunzo ya muda mrefu kwenye fani mbalimbali kama vile umeme, Tehama na Elektroniki wahitimu 121 (wanawake 27 na wanaume 94).

Pamoja na hayo ameiomba TCRA kuhamasisha makampuni ya simu kama vile Samsung,Nokia Tecno, Huawei kutumia chuo hicho kwa kupeleka vifaa vya simu, tehama na elektroniki kwaajili ya mafunzo kwa vitendo ambapo itakuwa ni msaada kwa mafundi na wanachuo kwa ujumla.

Hata hivyo katika changamoto amesema gharama kubwa ya upatikanaji wa vifaa vya kiteknolojia kunapunguza kasi ya chuo hicho kuweza kutoa mafunzo yanayohitajika kwenye soko kwa wakati.

Vifaa vipo lakini tunatakiwa kutumia mashine za kisasa kutokana na teknolojia zinabadilika kila kukicha hivyo kutumia vifaa vilivyopitwa na wakati kufundishia kunaathiri ubora wa ujuzi anaoupata mwanafunzi ukilinganisha na mahitaji ya soko". Amesema Mhandisi Mkasanga.

Awali wakisoma Risala wahitimu wa chuo hicho wamiomba TCRA kuwasidia kuwatatulia baadhi ya changamoto zinazokikabili chuo hicho ikiwemo mabadiliko ya mitaala kuendana na kasi ya sayansi na Teknolojia,Muendelezo wa kozi ndefu,Upungufu wa vitabu kwenye Library ya chuo,Ukosefu wa vimbweta na Kukosekana kwa maeneo ya kufanyia mafunzo ya vitendo.

Nae Bw.Nelson Rutter akiongea kwa niaba ya wazazi amewataka wahitimu kuwa na nidhamu kazini ama kwa wateja wao ili kuweza kuunda uwaminifu kwani b aadhi ya mafundi wamekuwa si waaminfu kwa wateja wao.

Chuo cha TEHAMA cha VETA –kipawa ni moja kati ya vyuo vilivyopo nchini vinavyomilikiwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), ambacho ni chuo cha mfano kinachotoa mafunzo mbalimbali yenye mchepuo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Sasa hiki ndio kituko cha mwaka
 
swala la kuanzisha kiwanda cha simu sio swala la kitoto.
Kwanza kupata jina ambalo linaweza kushindana na na tekno infnix itel kwa afrika masharik. Na pili je unaweza kushindana vip kidunia na samasung iphone huawei sony lg nk.

Pili je ni kitu gani ambacho kimekosekana sokoni ambacho wataenda kutatua kiwada cha simu kutoka Tanzania ikiwa blackberry walishindwa hadi saizi blackberry na viwanda vingi tu vya simu vimeacha kutengeneza simu.

Tatu serikali hiyo biashara itaweiza vip ikiwa hakuna biashara ambayo imewahi kufanya serikali na ikawafanikiwa. Kwa mfano tanesco shilika la ndege nk
Kila siku wanapata hasara mabilion ya shililingi.
Nahisi itakuwa ni mahali pa kuwaweka mafundi wa kurekebisha simu sehemu moja, sio kuunda.
 
Back
Top Bottom