Naskitika sana television ya Taifa TBC kwenye dstv mara mnapotea mara mnarudi nashindwa kuelewa kweli mmejipanga kurusha matangazo yenu kimataifa ama bado mpo kwenye majaribio? Kasheshe ni pale wakati wa usomwaji wa taarifa za habari. Clips mmezirekodi siku hiyohiyo lakini zinagoma kucheza ina maana gani?vyombo vyenu vibovu ama vipi?tena mara mnaongeza sauti ambapo inanilazimu nikae na remote control ya decorder yangu kupunguza na kuongeza sauti mnamatatizo gani? Halafu taarifa zenu hazina mvuto wa kutazama kabisa. Kama kuna siku mlikuwa mnarusha siasa tupu pasipo na habari nyingine iliyokuwa na uzito. Naombeni msitutie aibu maana hata nchi nyingine zinawatazama myatendayo