TBC yadanganya, hatua stahiki zichukuliwe

TBC yadanganya, hatua stahiki zichukuliwe

Things Fall Apart

Senior Member
Joined
Jun 26, 2012
Posts
178
Reaction score
146
Habari wana JF,

Naanza na swali: Je, ni halali kwa televisheni ya taifa (TBC) kutangaza habari kwa kupotosha?

Hii imetokea leo katika uchambuzi wa magazeti kwani mtangazaji aliyekuwa akisoma habari za magazeti anashika gazeti na kusema "habari iliyopewa uzito wa kipekee..." lakini cha kustaajabisha anasoma habari ambayo siyo iliyopewa uzito wa kipekee na kuiacha kabisa habari iliyopewa uzito wa juu kisa tu kwamba inamzungumzia Edward Lowassa mgombea urais wa Ukawa kwa tiketi ya CHADEMA. Tizama mwenyewe hapa:


Hii ni wazi kabisa kuwa kanuni za huduma ya utangazaji (maudhui) ya mwaka 2005 zimekiukwa hadharani. Kanuni ya 6(2) inasomeka hivi:

"Kila mwenye leseni ni lazima ahakikishe anatoa taarifa kwa usahihi na uhakika; anaripoti habari bila upendeleo na kuzingatia mizani, bila kukusudia au kuondoka katika ukweli, ama kwa kuvuruga au kwa kutoa taarifa zisizo sahihi".

Ikumbukwe kuwa, ni majuzi tu Mamlaka ya Mawasiliano TCRA imekichukulia hatua za kinidhamu kituo cha ITV kwa kuripoti habari zisizo za kweli.

Hivyo basi; kwa kuwa sharia ni msumeno, basi na TBC nayo iadhibiwe vilevile kwa upotoshaji huu. La sivyo tutakuwa tuna "double standards". Kitendo hiki sio tu kinadhalilisha taaluma ya utangazaji bali pia kinalitia aibu shirika la utangazaji la Tanzania (TBC) ndani na nje ya nchi ikizingatiwa kuwa serikali imekuwa ikijinasibu kuwa inafuata misingi ya uwazi na uwajibikaji.

Naomba kuwasilisha.


TCRA ni taasisi inayoongozwa kwa mujibu wa Sheria ya EPOCA 2010, Kanuni za Utangazaji pamoja na masharti ya leseni za Utangazaji.

Upo utaratibu unaofuatwa katika kushughulikia ukiukwaji wa Kanuni au Masharti ya leseni ikiwa ni pamoja na kumtaka mwenye leseni kujibu tuhuma na kuitwa kwenye Kamati ya Maudhui.

Hatuwezi kutoa hukumu bila kumsikiliza mwenye leseni na shauri kufikishwa katika Kamati ya Maudhui.

Tunawasihi wananchi kuwa Na subira suala hili linafanyiwa kazi na taarifa kwa umma itatolewa juu ya maamuzi yatakayotolewa.

Asante

Update:

TCRA imeipa onyo TBC1. Habari zaidi, Soma=>
TCRA yaipa onyo kali TBC1 kwa kosa la Ubaguzi wa kusoma habari Magazetini
 
Last edited by a moderator:
Ni aibu sana aisee. Ni bora wangefuta tu hiki kipindi kuliko kujidhalilisha kwa kiasi hicho.yani wanashindwa hadi na gazeti la uhuru ambalo ni la chama na kujulikana hivyo wazi
 
Hahaha TBC ni noma!! Hivi kweli hawaoni hata aibu jinsi walivyokuwa wakisoma kwamba watizamaji wanaweza kuona ni nini kinasomwa toka kwenye gazeti na kwamba wanapotosha? Sasa wanafanya hivyo kwa maslahi ya nani kama si kujivua nguo wao wenyewe. Kwani wamelazimishwa kusoma hayo magazeti? Si afadhali ahata wangesema hayajatufikia hayo magazeti wasiyopenda kusoma habari zake? This is too low for Media organ like TBC kwa kweli. Ngoja tuone Msomaji wa magazeti wa kipindi cha magazeti siku ya Jpili atasemaje juu ya kitakachokuwa kimeandikwa na magazeti juu ya uwepo wa huyu jamaa huko Arusha!
 
Hii ni aibu kubwa... JK chek na hawa jamaa... wanaaibisha kabisa mfumo wa demokrasia nchini nawe una dhamana..... yako mengi yanafanywa hehind the curtains ila hili limeonekana na ni aibu kwako na kila mpenda demokrasia nchini na nje ya Tz... Mungu ibariki Tz...
 
Wana JF,

Ni kwa kawaida ya serikali kufanya mabadiliko au kuwafukuza wafanyazi wake wenye weledi pindi wakionyesha weledi wao katika kazi kwa ubora wao, lakini huku wanakumbana na shinikizo nyingi kutoka serikalini, kama vile kupindisha habari, kukuza habari zisizo habari na kudanganya ikitokea , watangazaji, wanahabari waratibu wa habari huwa wana wakati mgumu wa kufukuzwa kazi kipindi cha uchaguzi ikiwa wataenda tofauti na maelekezo ya kutoka kitengo.

My Take.
Hatujui safari hii watamfukuza nani maana lowasa ndio katawala media, huku nyuma yake wakuu wa nchi wakisema huo ni moto wa mabua utazima, tu, hayo ni makapi yatakauka tu.
 
Ccm awajajuwa kuwa vitu kama hivi vitawamaliza kabisa!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom