Wakati Mh Tindu lisu akishusha nondo kali kwa takwimu kuhusu utata wa hati za Muungano, inaonekana 'dawa iliwaingia ' waheshimiwa wakaamua kuzima matangazo ya Tv yaliyokuwa yanarushwa hewani live na TBC 1 ili kuwapumbaza Watanzania. La kushangaza ambalo kwangu inaonekana matangazo yalizimwa makusudi, badala ya kuomba radhi wananchi wao wakaweka hotuba ya J.K aliyoitoa wakati wa kufungua Bunge la Katiba hususani katika kipengelee kwamba watu wengi wamezaliwa baada 1964 hivyo Tanganyika hawaijui,. Hii inaonyesha kuhangaika na hotuba ya Lissu na ni aibu kwa Taifa. Haya ndiyo yaliyomshinda Tiddo ya kulamba watu nyao kwa kujikomba na kudhalilisha taaluma yako. Baada ya kugundua mbinu hiyo, Freeman Mbowe aliomba mwongozo kwa mwenyekiti Sitta ambaye kwa kweli hakuwa na jinsi zaidi ya kuhailisha bunge. TBC walirudi wakati Sita akisoma dua ya kuhailisha Bunge, na mtangazaji akasema matangazo yamekatika kwa bahati mbaya na "si vinginevyo". SHAME ON YOU TBC. "You can fool all the people one time, but you cant fool all the people all the time"