Tbc 1, wanachefua

Daaaaaaaaaaaa bado mnaangalia TBC 1 hadi leoooooooo,mi nilisha acha kuangalia hiyooooooooooooooooooooooooooooo
 
Mi nafikiri ni ujinga tu wa hivi vitangazaji!Kwani ukisoma gazeti maana yake umeandika wewe hiyo habari?Ukiacha kusoma mtaani halitakwenda?Mtawala anayempa nafasi mtu huyu mjinga kwa sababu hii ya kijinga basi naye ni mjinga.
 
Suala la TBC1 kutokuwa independent,litupe fundisho.Sidhani kama serikali ina mkono katika suala hilo,inawezekana ni waandishi wenyewe hawajiamini.Nimewahi kusema katika jamvi hili kuwa elimu zetu tuliowengi ni za mashaka.Elimu sharti impe mtu ujasiri wa kutenda,elimu ya woga hatuihitaji katika kipindi hiki cha mageuzi.Wantangazi wa TBC kwa kujua au kutojua wamejikuta mazezeta na walamba miguu ya wakuu wa serikali wakati sisi wananchi ndio tunaowaweka mjini kwa kuwalipia mishahara na malupulupu mbalimbali.

Hatuandiki haya kwa sababu tunachuki nao,ni kwa sababu kile ni chombo chetu,hivyo lazima kifanye kazi ya kutusaidia sisi.We angalia katika kipindi cha uchaguzi jinsi BBC walivyofanya kazi as if ni shirika letu.Binafsi namshangaa sana TIDO,mtu mwenye exposure ya kutosha anashindwa kufanya mabadiliko kama alivyoahidi,kazi aliyokuwa anafanya akiwa BBC ni tofauti na kazi anayoifanya sasa,huu ni usaliti mkubwa sana na ambao hatuwezi kuuvumilia any more.Kupitia post hizi TBC wachukue hatua mapema iwezekanavyo,kabla wananchi hawajachukua hatua.asanteni wote kwa michango yenu,ujumbe umefika.
 
tbc1 ni tawi la ccm kama ilivyo uvccm...usitegemee uwe na mawazo ya-kipinzani ukapata nafasi ya kuyatoa..
 
Kwa wapenda mabadiliko kama bado mnaangalia Tbc1 ,mnasikiliza Tbc Taifa/FM,Radio Uhuru na kusoma Magazeti ya Uhuru,Mzalendo,Habari Leo,Daily News,Rai,Mtanzania.Mjiandae kumiza mioyo yenu na kuongea peke yenu,kusonya,kutuka kama mmechanganyikiwa.Uchaguzi umeisha ila kampeni zinaendele kama kawa.
 
Juzi pia gazeti la mwananchi lilioandika habari za masha kung'oa Vitasa jamaa alitaka kulisoma lakini akaichunia hiyo habari muhimu kabisa iliyokuwa ukurasa wa mbele kwa herufi KUUBWAAAA!
Halafu wanajamvi naona imepitishwa rasmi sasa vituo vyote vya TV kwamba ni marufuku kusoma magazeti ya Raia Mwema na Mwanahalisi siku ya Jumatano yanapotoka.

TBC wanachefua: mimi huwa siangalii hiyo tv yenu haina jambo la muhimu.
 
Huyo Tido hana lolote na TBC yao katoka TBC kaja kutuharibia huku kwa kuendesha kwa malengo ya kisiasa. Nadhani sasa sina mpango tena na tbc
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom