TBC 1: Hivi tatizo ni Mitambo au Kamera hazina uwezo?

nyumbamungu

JF-Expert Member
Mar 3, 2017
997
828
Kinachonisikitisha zaidi ukiwa unaangalia matangazo Mubashara kupitia televisheni ya taifa muonekano wa picha hauna mvuto, tofauti na Azam tv, ITV, Star tv na Clouds tv.

Huwa najiuliza sana tatizo ni mitambo ya kurushia matangazo au Kamera, kama itakuwa Kamera kwanini wasinunue? naambiwa Lens zenye uwezo gharama yake inaanzia 30,000,000.

Tena wanasema hizo hata wanaopiga picha binafsi kwenye shughuli za harusi wanamiliki.

Kitu kingine ninachojiuliza! lile gari la Matangazo ya nje mbona ni mara chache sana huwa linatumika? tena pamoja na kutumika kwake matangazo yake huwa yanakatika au sauti inakosekana, Nakumbuka Mh Rais alipofanya ziara mkoa wa Pwani aliwaagiza TBC 1 warushe matangazo kila atakapokuwa anahutubia mkutano wa hadhara, walirusha matangazo lkn kidogo yalikatika.

Kupitia kampeni ya Uzalendo inayoendelea ingekuwa vizuri wao kama Televisheni ya Taifa wahamasishe kwakufanya matangazo Mubashara maeneo mbalimbali ya nchi (hadi mikoani), sio muda wote wanaendesha vipindi vya kuwa Mzalendo, Tunatekeleza na Tanzania Mpya, ndani ya Studio tu, ikiwezekana wawezeshwe waende mikoani .

Wiki iliyopita nilimuona Mkurugenzi wa TBC alipokuwa kwenye Maonesho ya Sabasaba, akipokea maoni na kujibu maswali ya watazamaji na wasikilizaji wa TBC kuhusu uboreshaji wa vipindi upande wa Redio na Televisheni, hongera kwa hilo lakini tunaomba uyafanyie kazi kwani ulisema yapo yanayojibika na mengine yanahitaji utekelezaji tu.

Mwisho: Hili kama utakuwa na bajeti tunaomba uandae kampeni ya wazi au mjadala kwa Watazamaji, Wasikilizaji na Wadau mbalimbali wanapenda nini toka Televisheni na Redio yao halafu peleka kunakohusika subiri maamuzi yao.

Pia peleka Dokezo kwa Wakuu waunde Tume kupitia Utendaji wa Star Media ikiwezekana hata mkataba wao uangaliwe upya kama kuna manufaa au hakuna kw aTaifa, Je TBC ikiwezeshwa itashindwa kufanya wanavyofanya wao ili iweze kujitegemea? Star Media ibaki kuuza Ving'amuzi tu, na kiundwe Chombo kitakacho simamia Chaneli.
 
TBC kwa ujumla wao ni wameshindwa.
Ukiangalia kwa kutumia flat screen tv ndo TBC1 inaoneka hovyo zaidi bora utumie chogo.

Sasa zama hizi nizakutumia chogo?

Siku hizi siangalii TBC tena ningekua na uwezo ningewambia wamiliki wa king'amuzi changu waiondoe TBC
 
kweli kabisa cheki kitu hiki dijitali toka AZAM TV

AZAM TWO MIZANI YA WIKI JULAI 09. 07. 2017

Source: Azam TV
 
TIDO MHANDO aliweza kuleta mapinduzi mazuri sana katika shirika hili ,SASA SIJUI NINI KILITOKEA AKAONDOKA HUKO NA BAADA YA HAPO NI UBOVU KILA SECTA KATIKA HILI SHIRIKA
 
TBC wanaosikika vzr ni watangazaji tu wakati wa habari. Wengine wanaoriport na habari yenyewe field ni chenga tu. Unajilazimisha kusikia hadi kichwa kinauma.
Wajirekebishe
 
Mi huwa nafikiri wamelazimishwa kuendesha vipindi.yaani hakuna anayependa kazi hapo TBC.

Lakini bado sijaona haja ya kusifia hata hao wengine nao ni upuuzi mtupu,harafu jinsi TV yako inavyozidi kuwa pana ndipo wanavyozidi kuonekana hovyo.
 
Bora shirika libinafsishe umiliki 75% ili liweze kujiendesha kitaalamu

Sent from my TECNO_W4 using JamiiForums mobile app
 
Sijui niliangalia TBC 1 lini mara ya mwisho kwakweli

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
 
Ila una moyo mgumu eti bado unaaangalia hiyo kitu

Sent from my itel it1550 using JamiiForums mobile app
 
Kwa taarifa yako mfano ile gari wanayoiita Obi Van yenye uwezo wa kurusha matangazo mubashara popote pale yako ktk nchi tatu Africa na Hata camera za TBC za kuchukua matukio mbalimbali ni za high quality na gharama sana.

Sasa labda wataalam ndiyo inaweza kuwa shida.
 
Nimeiona michango yenu inaonesha jinsi gn kila mmoja anavyosikitika juu ya TBC, wapo wengine wamesema karibu redio zote kwa afrika mashariki zinalingana. Lkn kupitia mitandao tunaweza mshauri Mkurugenzi wake anachotakiwa akifanye angalau hadi anatoka hapo aweke kumbukumbu kama alivyoweka Tido Mhando, kuonesha ligi ya Uingereza, kuanzisha kauli mbiu "Ukweli na Uhakika"
 
Kwa kweli kwa sasa TBC inasikitisha sana.
yaani ni aibu kuangalia. sasa mbaya zaidi ni hao wafanyakazi wake. yaani utadhani hawalipwi mshahara.. balaa tupu

Sent from my SM-J200F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom