Tb Joshua alivyonipa utajiri

Tb Joshua alivyonipa utajiri

"Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2" umeona amefanya mangapi ndani ya miezi 3 kwa mil 180 ....ngoma yataka matao jamani ....
 
Heading yako iko vizuri kuwa
TB Joshua amekupa utajiri. Umekosea hapo mwishoni ulipomtaja Yesu kwani
hakuna uhusiano wa anointing water na Neema ya Bure iliyotolewa na
Yesu Kristo wala haiuzwi kwa bei yeyote
. Hiyo anointing water ni
ibada ya sanamu na ushirikina ambayo chanzo chake ni shetani. Shetani
anasema ukinisusujudia na kunitumikia nitakupa milki yote ya dunia. Yesu
anasema tafuteni kwanza ufalme wa mbinguni na haki yake na hayo yote
mtazidishiwa...hapo usimmsingizie Yesu.

Pokea LIKE mkuu ukiona kanisa linahubiri utajri na miujiza ya uponyaji jua YESU wa kweli hayupo
 
Sikiliza wewe mwanamahesabu. Kama jamaa kanunua fuso ya kwanza mwezi wa kwanza. mwezi wa pili kafungua mgahawa mwingine, mwazi wa tatu kanunua fuso na kufungua mgahawa wa tatu. Je mwezi wa nne atakuwa na uwezo kiasi gani? Utabakia Tshs 2M kama mahesabu yako yalivyo sema. Kweli hesabu ni tatizo kwa watanzania wengi

Huyu jamaa amesema, hivi sasa yupo mbioni kufungua restraunt zngine 2, kwahyo vyote alivfanya kwa ku2mia mgahawa mmoja ule ule. Pia alidai kipato chake kilpanda toka lak 2 hadi 2 milioni (ambayo ndo maxmum amount mana hajasema kama kiliongezeka zaidi).
 
Ivi watu, lini tutaacha upuuzi? Lini tutajielewa?

Ivi wachungaji wangekua na uwezo huo kungeanzishwa hospitali kweli???????

Huyo Yesu ameshakufa, aliebaki ni Mungu, kwanini mnadai nguvu za mfu na kuzitukuza kuliko hata alivyokuwa hai?

Kama yeye muokozi kwanini alishindwa kujiokoa mwenyewe msalabani pale?????
:think: :think: :think:

Wewe sasa unataka kuharibu thread
 
Ngoja T.B joshou afe utarudi kama zaman na hali yako ya kawaida
 
milion 2 ndani ya miezi 3 ni milioni 180 (2 mara 90 = 180)! Inawezekana vipi kwa milion 180 uweze kununua fuso 2, coasta 3 pia ujenge nyumba 2, restraurant 3? Innocent chacha hebu fafanua vizuri.

Labda nyumba ya maboks na magari ya mabox niliona lusekelo nae anawaombea watu wanapata magarii aiseeeee
 
Last edited by a moderator:
Mungu kakupa utajiri au TB JOSHUA? Mwanadamu akikupa utajiri lazima uulipie
 
du, wacha niendelee kumuamini Mungu wa ibarahimu, isiaka,na yakobo, maana aya yote yalitabiliwa kabla. Amein. uwa nikionaga na wa hapa bongo wakiwapokelesha kitu watu, ila hakuna kikubwa zaidi ya imani, na imani bila matendo ni bure. endelea kuamini hiko unachoamini.
 
Alifufuka mkuu ndio maana tunaamini la sivyo ukristo usingekuwepo, na kuhusu kufa msalabani ilikuwa lazima afe ili alipe deni la dhambi zetu ndio maana hakujiokoa. Ila kuna wajanja wachache wanatumia vibaya neema
tuliyopewa bure.

hongera mkuu Gamaha! Kwa jibu zuri na la kistaarabu kwa huyu mpuuzi anaejiitaa mashaxizo, maana amenitia hasira na nikawa najiandaa nimlipuwe. Anyway nishamsamehe kwa ujinga wake!!
 
Tb Joshua si atumie hayo maji awarudishe wale waliotekwa na boko haram?
 
milion 2 ndani ya miezi 3 ni milioni 180 (2 mara 90 = 180)! Inawezekana vipi kwa milion 180 uweze kununua fuso 2, coasta 3 pia ujenge nyumba 2, restraurant 3? Innocent chacha hebu fafanua vizuri.

hata mi baso najiuliza maswali mkuu hapo naangalia sana TB Joshua na pia naamini uponyaji wake.
_mleta mada katia chumvi hadi mboga imekuwa chungu
 
Last edited by a moderator:
.
.
.
Huwezi kuamini, mauzo yalibadilika kutoka shs laki 2 kwa siku hadi milioni 2.

Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2.

ASANTE YESU. ASANTE TB JOSHUA

mauzo mil 2, mtaji matumizi mengine ~ 1m = faida ~1m/day x miezi 3(siku90) = faida kwa miezi 3, 90m.

Fusso >40m x 2 = >80m
coaster >30m x 3 >90m
nyumba> 25m x 2 = >50m.
Jumla >220m.
Jumla kuu (>130m)

Mkuu unadaiwa si chini ya 130m
 
Hayo maji yanatofauti gani na zile dawa tunazopewa na waganga tuweke kwenye biashara...

Huo ni ushetani tu..
 
Kama utakumbuka, miezi miwili iliyopita nilikuja na post juu ya kutoa shukrani kwa Yesu kwa kumtumia mtumishi wa Mungu TB Joshua kuniponya tatizo langu la uvimbe sehemu za siri ambalo lilikuwa likinifanya kushindwa kusimamisha uume wangu kwa miaka zaidi ya 4. Uponyaji wa tatizo langu ulifanyika kupitia maji maarufu ya ANOINTING WATER yanayoandaliwa na kutolewa na TB JOSHUA MINISTRIES.

Leo nataka nikushirikishe juu ya jinsi maji hayo yalivyonipa FUSSO 2, COASTER 3, NYUMBA 2, na RESTAURANT 3.

Nilianza biashara yangu miezi 4 iliyopita. Kalikuwa ni kamgahawa kadogo tu lakini kwasababu niliamini kwenye nguvu iliyomo ndani ya Yesu, sikuwa na hofu yoyote kuwa mafanikio yanakuja.

Kabla ya hapo, nilisikia shuhuda za watu mbaimbali ambao walitajirika baada yakutumia ANOINTING WATER kwa imani. Nikaamua kuyatumia haya maji kwenye biashara yangu kwa imani kubwa. Nilichokifanya ni kupuliza haya maji kwenye milango na makabati ya chakula huku nikiamrisha wateja wafurike kwenye biashara yangu kwa jina la Yesu.

Huwezi kuamini, mauzo yalibadilika kutoka shs laki 2 kwa siku hadi milioni 2. Watu wanajaa kwenye restaurant hadi nikaamua kuweka viti na meza eneo la jikoni na bafuni. Wateja wako radhi hata kula huku wamesimama au wamechuchumaa. Inapofika muda wakufunga huwa inabidi niwafukuze wateja vinginevyo tunaweza kukesha.

Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2.

ASANTE YESU. ASANTE TB JOSHUA

Biashara ni matangazo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom