Tb Joshua alivyonipa utajiri

Tb Joshua alivyonipa utajiri

Huwezi kuamini, mauzo yalibadilika kutoka shs laki 2 kwa siku hadi milioni 2. Watu wanajaa kwenye restaurant hadi nikaamua kuweka viti na meza eneo la jikoni na bafuni. Wateja wako radhi hata kula huku wamesimama au wamechuchumaa. Inapofika muda wakufunga huwa inabidi niwafukuze wateja vinginevyo tunaweza kukesha.

Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2.

ASANTE YESU. ASANTE TB JOSHUA

Haiingii akilini hii makitu! Tumeambiwa tukiwa na IMANI kiasi cha punje ya haradali, twaweza hamisha milima. Lakini kwa biashara ya mauzo ya Shs. milioni mbili kwa siku (siyo FAIDA), kupata hayo yote kwenye RED, basi imani yako mpendwa ni kubwa kama fenesi. Hujatuambia gharama zako ni zipi kwani biashara ina mapato na matumizi. Lakini hongera kwa mafanikio yako through anointing water. Tena nimeona juzi kwenye re-broadcast ya 15 July 2014 kuna new product ya anointing water - ukiipata hiyo, kwa imani utajenga 5 star hotel.
 
Shauri zako,
Kutoka laki mbili kwenda milion mbili kwa siku ni maajabu; hata zingekuwa zile hotel za kimataifa siyo hivyo.

Hizo hela ndugu yangu jiangalie mara mbili mbili, kuna siku watakuambia tunataka sadaka, kaa vizuri na mkeo/mume na watoto wako.

Usifurahie pesa za mapepo, hayo maji yangekuwa na huo uwezo akina martha kaaya wanaoyauza si wangekuwa mbali sana kimaendeleo?
 
Wewe ni wakala wa TB joshua unatangaza biashara yenu tu hapa!

Mimi ni mkristo safi na kwenye Biblia inasema umepewa bure utoe bure sasa hawa wachungaji wa jua kali wanaouza maji , sabuni, sijui nini hivyo wanavyouza wanajua wenyewe vinapotoka lakini huyu MUNGU muumba wa Mbingu na ardhi alisha sema amewapa watu uwezo wa kuponya kuombea na kama alivyotoa bure bila garama basi na waliopewa hiyo karama waitoe bure hao wanaofanya kinyume na hayo ni mawakala wa shetani sio wale tunaowasoma ndani ya Biblia .
 
ushuhuda wako umeukosea au inawezekana umeuongezea chumvi maana huwezi kujenga nyumba mbili kwa miezi mitatu......the rest yanawezekana.
 
Ivi watu, lini tutaacha upuuzi? Lini tutajielewa?

Ivi wachungaji wangekua na uwezo huo kungeanzishwa hospitali kweli???????

Huyo Yesu ameshakufa, aliebaki ni Mungu, kwanini mnadai nguvu za mfu na kuzitukuza kuliko hata alivyokuwa hai?

Kama yeye muokozi kwanini alishindwa kujiokoa mwenyewe msalabani pale?????
:think: :think: :think:

Sasa na wewe ni uharo gani huu umeandika....?
 
Ivi watu, lini tutaacha upuuzi? Lini tutajielewa?

Ivi wachungaji wangekua na uwezo huo kungeanzishwa hospitali kweli???????

Huyo Yesu ameshakufa, aliebaki ni Mungu, kwanini mnadai nguvu za mfu na kuzitukuza kuliko hata alivyokuwa hai?

Kama yeye muokozi kwanini alishindwa kujiokoa mwenyewe msalabani pale?????
:think: :think: :think:

yesu alisurubiwa akafa akazikwa akafikia kuzimu siku ya tatu akafufuka katika wafu kama ilivyoandikwa, akapaa mbinguni amekaa mkono wa kuume wa baba toka huko atakuja tena duniani kuwahukumu wazima na wafu na ufalme wake hautakuwa na mwisho.

wafu ni pamoja na mtume mwamedi ambaye yuko jehenamu anayesubiri hukumu yake.
 
Ivi watu, lini tutaacha upuuzi? Lini tutajielewa?

Ivi wachungaji wangekua na uwezo huo kungeanzishwa hospitali kweli???????

Huyo Yesu ameshakufa, aliebaki ni Mungu, kwanini mnadai nguvu za mfu na kuzitukuza kuliko hata alivyokuwa hai?

Kama yeye muokozi kwanini alishindwa kujiokoa mwenyewe msalabani pale?????
:think: :think: :think:

Povu loote hili lakutoka baada ya kuvimbiwa uji! Mudi ndiye mfu! Yesu yu hai ...... alikaa siku 2 kaburini ya tatu akafufuka!
So ukome kumwita Mungu mfu!
Kama yule wenu alishindwa kufufuka siyo Yesu Kristo wa Nazareth aliye hai!
 
na mashaka na ushuhuda wako aiwezekani mafanikio kama hayo yaje kwa miezi 4 tena zaidi ya kipato chako ulichopata kama ni kweli na Mungu akusaidie na alaaniwe amtegemeaye mwanadamu kama wewe unavyomtegemea tb joshua
 
quote_icon.png
By sembo
milion 2 ndani ya miezi 3 ni milioni 180 (2 mara 90 = 180)! Inawezekana vipi kwa milion 180 uweze kununua fuso 2, coasta 3 pia ujenge nyumba 2, restraurant 3? Innocent chacha hebu fafanua vizuri.
:llama:
Mhh hivyo ndani ya miezi 12 atakua ni bilionea, kaka mie sijaelewa vizuri mafanikio ya muda mfupi na makubwa hivyo huwa tuna mashaka sana, Ila Mungu ni mkubwa saana inawezekana ni kwa Neema za Mungu ndo ukapata yote hayo, ila mimi binafsi nina walakini kutokana na maelezo yako Ingawa namwamini Yesu kristo na Damu yake ni kuu mno
 
Nimegeuka TB JOSHUA? Mimi ni mnunuaji wa hayo maji si muuzaji

Inaonekana unaongea vitu usivyojua ndugu yaani useme ni damu halisi ya yesu mara wewe hujui bali ni mnunuzi tu wa hayo maji,, are you serious ??? unatoleaje ushuhuda kitu usichojua??
 
yesu alisurubiwa akafa akazikwa akafikia kuzimu siku ya tatu akafufuka katika wafu kama ilivyoandikwa, akapaa mbinguni amekaa mkono wa kuume wa baba toka huko atakuja tena duniani kuwahukumu wazima na wafu na ufalme wake hautakuwa na mwisho.

wafu ni pamoja na mtume mwamedi ambaye yuko jehenamu anayesubiri hukumu yake.

Thank you! Glory to the Lord! Na kila jicho litamwona, na kila goti litapigwa..... Haleluya!
 
Povu loote hili lakutoka baada ya kuvimbiwa uji! Mudi ndiye mfu! Yesu yu hai ...... alikaa siku 2 kaburini ya tatu akafufuka!
So ukome kumwita Mungu mfu!
Kama yule wenu alishindwa kufufuka siyo Yesu Kristo wa Nazareth aliye hai!

Hahahahahaaaaaaa!
:tape: :tape: :tape:
 
tukiachana na mambo ya maji na damu na yesu
turudi kwenye financial accounting au financial management au investment analysis au hisabati rahisi tu,
kwanza nakunukuu "Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2" jambo hilo haliwezekani.

tuchukulie hio milioni mbili unayopata yote ni faida tupu kwa miezi mitatu (90 x 2 = 180) milioni. hivyo vyote umefanya kwa mil 180? haiwezekani. tafuta uongo mwingine.
 
Huyu jamaa, inatakiwa akajpange upya ndo aje atudanganye tena.

Kuna watu Wa aina mbili wanakera sana
Hawa Wa netwoking marketing na hawa wanaolazimisha watu waabudu binadamu wakat hawaelew hata what is real behind the scene
 
tukiachana na mambo ya maji na damu na yesu
turudi kwenye financial accounting au financial management au investment analysis au hisabati rahisi tu,
kwanza nakunukuu "Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2" jambo hilo haliwezekani.

tuchukulie hio milioni mbili unayopata yote ni faida tupu kwa miezi mitatu (90 x 2 = 180) milioni. hivyo vyote umefanya kwa mil 180? haiwezekani. tafuta uongo mwingine.


Sikiliza wewe mwanamahesabu. Kama jamaa kanunua fuso ya kwanza mwezi wa kwanza. mwezi wa pili kafungua mgahawa mwingine, mwazi wa tatu kanunua fuso na kufungua mgahawa wa tatu. Je mwezi wa nne atakuwa na uwezo kiasi gani? Utabakia Tshs 2M kama mahesabu yako yalivyo sema. Kweli hesabu ni tatizo kwa watanzania wengi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom