M
Mteja atathibitisha vipi kama mwamba ni mgumu au laini. Ebu tuweke range kuwa visima kuanzia urefu Wa mita mfano 20 had I hamsini mwamba mgumu gharama zote mpaka kupata maji ni sh. Y n.k endelea hivi kwa mwamba laini nk. Suala la usafiri nivema likawa kwenu. Tunahitaji gharama za jumla sio ututajie kitu kimoja kimoja. Mteja atajuaje kama maji yanayochimbwa no ya chumvi au la. Ikitokea mmechimba maji mkakosa itakua hasara ya nani? Je, kabla ya kuanza kujimba mnaweza kubainisha umbali wa kupata maji? Kama sio hivo hamuoni kuwa shughuli hii inafanyika kwa kubahatisha? Hali hii so inaweza kuleta mtafaruku kati yenu na mteja? MAJIBU TAFADHALI!!
Suala la kujuwa kuwa mwamba ni mgumu au laini litajulikana baada ya kufanya ground water survey. Na kisima cha mita hamsini kwa mwamba mgumu itaghatimu shillingi,
Mita 1= 80000 tsh
Mita 50=??
Apply cross multiplication
Mita 50 × 80000 tsh/1mita
Cut mita both side
4000000 tsh
Kwa hyo kisima chenye mwamba mgumu cha mita hamsini kinagharimu shillingi millioni nne kamili hapo wapata kila kita mpaka maji yanatoka
Kisima chenye mwamba laini cha mita hamsini kitagharimu shillingi
Mita 1= tsh 65000
Mita 50=??
Mita 50 × 65000/mita 1
3250000 tsh
Hizo ndio gharama za kisima cha mita 50 for soft rock
Mara zoote kwenye suala la uchimbaji wa kisima na kwenye inshu ya kumobilize machine kuja site usafili huwa juu yetu ni katika kumpunguzia gharama mteja.
Suala la quality ya maji huja mara nyingi baada ya maji kuchimbwa yaani hatuwezi kujuwa kuwa maji haya yapoje mpaka yatakapo kuwa yameshachimbwa tayari.Pia zipo njia ya kupunguza au kuondowa chumvi.
Ikitokea tumechimba tukakosa maji sasa hapo tutaangalia jee eneo hilo limefanyiwa ground water survey? Jibu kama ni ndio limefanyiwa,jee nani kafanya survey? Hapo itabidi aliyefanya survey awe responsible kwenye suala hilo ila kama survey tumefanya sisi wenyewe pia tutakuwa responsible kuyatafuta maji hadi yapatikane.Mara zote huwa tuna chimba kisima kwa kufuata maelezo ya ground water survey report,yenyewe ndio inatuelekeza tuchimbe mita ngapi,tutumie mashine ya aina gani katika kuchimba hapo pia hapo kuna mwamba wa aina gani soft au hard na ni vyema maji yakishachimbwa yapimwe kwanza kujuwa kama yanafaa kwa matumizi ya binaadamu.
Nb:huwezi kubaini umbali wa maji yalipo kabla ya kuchimba kisima kama hujafanya ground water survey
Angalizo: Ni vyema atakaye kufanyia ground water survey ndiye huyo huyo akuchimbye kisima incase yakitokea matatizo yoyote katika uchimbaji yeye mwenyewe ndio awajibike.
Usisahau hii ni biashara maongezi yapo.