Tatizo ni Upendo kupungua

Daudi1

JF-Expert Member
Dec 14, 2013
8,805
8,716
Habari ndugu zanguni, nawasalimuni wote kila mmoja kwa imani yake

Niende moja kwa moja kwwnye hoja ya leo, kumekuwa na malalamiko mengi juu ya mahusiano mpaka inafikia mahali inaonekana mahusiano hayana maana tena, wengine wamefanya mahusiano kuwa biashara, wengine imekuwa uwanja wa vita kuonyesha uwezo na ujanja maana halisi ya mahusiano haieleweki hasa kwa kizazi cha sasa.

Mwingine ukimwambia suala la mahusiano fikra zinazoingia kwake ni ngono hicho ndo anachokifahamu, mwingine atawaza kupewa zawadi/hela na mambo kadha wa kadha. Tatizo ni upendo wa kwanza kupungua, ule upendo wa kumpenda mpenzi wako kama unavyojipenda haupo tena, saizi upo upendo wa nipe nikupe.

Tatizo hili ni kubwa sana kwa sisi vijana wa sasaivi hasa kwa wanandoa, tumeshindwa kupendana katika uhalisia wake "tumetanguliza sentensi ya nitapata nini" yaani leo unamtongoza binti anakuambia utaniweza? Sasa nisikuweze kwa lipi wewe tembo? Mwingine anakuuliza nikikukubalia utanipa nini?? Aaaggrrr yaani wanajiweka kimtego mtego, tatizo upendo tumetanguliza vitu tumechukulia kama fursa fulani.

Upendo wa kweli hauangalii vitu, ukimpenda mtu sawa sawa,
1. Hautaangalia madhaifu aliyonayo bali utamvumilia

2. Hautamhesabia makosa kwamba jana ulinifanyia hivi, leo tena..

3. Utakuwa mwepesi wa kumsamehe kwa kuwa unampenda

4. Hautapenda awe katika msongo wa mawazo kwani ndiye furaha yako hivyo utamsaidia

5. Hautamtangaza vibaya kwa marafki hata kama kuna mahali hakutendei haki au hakuridhishi

6. Utaridhika na hali aliyonayo, iwe kiuchumi, kimaumbile au kwa namna alivyo

7. Utamthamini na kumheshimu kama wewe unavyopenda kufanyiwa.

Na upendo wa mtu kwa mwenzi wake unapungua kutokana na yafuatayo:

1. Dharau kwa mwanamke au mwanaume, yaani kuona kama bila wewe yeye hana maisha, au kuona kama wewe ndo umemfanya vile alivyo

2. Kutomsikiliza hasa wanawake wanapenda sana kusikilizwa hata kama jambo la kipuuzi msikilize tuu usipofanya hivyo ataona unampuuza hana maana kwako

3. Kukosa utii hasa kwa wanawake wamekosa utii kwa waume zao,hakuna mwanaume asiyependa mwanamke amtii, na wanawake wengi wanaona kumtii mwanaume ni utumwa hilo ni tatizo.

4. Kusema madhaifu ya mwenzi wako kwa mashost au masela, labda nikuambie kitu cha uhakika si kila mtu anapenda mahusiano yako na mwenzako hivyo ukianza kusimulia ya ndani unampa point ya kukuumiza tumeona na kushuhudia wengi wakipoteza mahusiano yao.

Mwisho kabisa rudisha upendo ule wa mwanzo kwa mpenzi wako na mahusiano yako yatakuwa salama, achana na habari za kuomba omba ushauri juu ya mahusiano yako inapotokea mmetofautiana tafuta suluhu mwenyewe, muwe na siku njema
 
Ngoja kwanza nimtumie huu ujumbe ausome ndio tuamue wote kwa pamoja kurudisha upendo,maana naweza kuurudisha peke yangu mwenzangu akagoma.Yani haya mapenzi ya siku hizi kweli ni majanga,nipe nikupe usipotoa hupewi...
 
Asubuhi yote hii tunaongelea Upendo na Mapenzi , Kwa Style hii mabadiliko tutayona kwenye tv tu.

Kila kitu kina muda wake Mkuu ndio maana auwezi kukuta kipindi cha Mapenzi Asubuhi wala mchana kwenye Radio station yoyote.

Vichwa vimeamka na Stress za matope ya Jangwani, Kuvuka kwenda kazi kwa Shida na Bado jioni.
 
Ngoja kwanza nimtumie huu ujumbe ausome ndio tuamue wote kwa pamoja kurudisha upendo,maana naweza kuurudisha peke yangu mwenzangu akagoma.Yani haya mapenzi ya siku hizi kweli ni majanga,nipe nikupe usipotoa hupewi...
Mapenzi halafu hayana pande mbili, na hayajawahi kubalance katika wawili lazima awepo mmoja anayeyabeba hayo mapenz bila hivyo itakuwa ni yale ya nipe nikupe
 
Asubuhi yote hii tunaongelea Upendo na Mapenzi , Kwa Style hii mabadiliko tutayona kwenye tv tu.

Kila kitu kina muda wake Mkuu ndio maana auwezi kukuta kipindi cha Mapenzi Asubuhi wala mchana kwenye Radio station yoyote.

Vichwa vimeamka na Stress za matope ya Jangwani, Kuvuka kwenda kazi kwa Shida na Bado jioni.
Poleni watoto wa mjini,kama nawaona mlivyovurugwa na matope ya Jangwani,ila mkipandisha tu hapo Fire utafikiri mmeshushwa mnavyojua kunawa fasta...
 
Asubuhi yote hii tunaongelea Upendo na Mapenzi , Kwa Style hii mabadiliko tutayona kwenye tv tu.

Kila kitu kina muda wake Mkuu ndio maana auwezi kukuta kipindi cha Mapenzi Asubuhi wala mchana kwenye Radio station yoyote.

Vichwa vimeamka na Stress za matope ya Jangwani, Kuvuka kwenda kazi kwa Shida na Bado jioni.

Ukikoment ndio mabadiliko?
Ni asubuhi kwa huko ulipo kuna sehemu nyngne ndio jua linazama, usikariri.
 
Asubuhi yote hii tunaongelea Upendo na Mapenzi , Kwa Style hii mabadiliko tutayona kwenye tv tu.

Kila kitu kina muda wake Mkuu ndio maana auwezi kukuta kipindi cha Mapenzi Asubuhi wala mchana kwenye Radio station yoyote.

Vichwa vimeamka na Stress za matope ya Jangwani, Kuvuka kwenda kazi kwa Shida na Bado jioni.
Ikiwa kichwa kinaamka na stress asubuh hii kuna shida mahali kichwa asubh kinatakiwa kiwe fresh, pole sana kwa stress kapambane mkuu na uwe na kazi njema
 
Ukikoment ndio mabadiliko?
Ni asubuhi kwa huko ulipo kuna sehemu nyngne ndio jua linazama, usikariri.
Mabadiliko ni dhana pana au yeye mabadiliko kwake ni kuona maghorofa tu na furahi ova huku watoto wasio mfahamu Baba wakiongezeka mtaani? Taasisi bora ya familia itatoa viongozi bora wenye maono bora kwa ajili ya vizazi vijavyo, lakini ukikomaa kwenye kubeba zege mwisho wa siku utakachojua ni kumwaga mbegu na kulala bila kuwaza kupalilia, kuvuna na kutunza ulichovuna
 
Habari ndugu zanguni, nawasalimuni wote kila mmoja kwa imani yake

Niende moja kwa moja kwwnye hoja ya leo, kumekuwa na malalamiko mengi juu ya mahusiano mpaka inafikia mahali inaonekana mahusiano hayana maana tena, wengine wamefanya mahusiano kuwa biashara, wengine imekuwa uwanja wa vita kuonyesha uwezo na ujanja maana halisi ya mahusiano haieleweki hasa kwa kizazi cha sasa.

Mwingine ukimwambia suala la mahusiano fikra zinazoingia kwake ni ngono hicho ndo anachokifahamu, mwingine atawaza kupewa zawadi/hela na mambo kadha wa kadha. Tatizo ni upendo wa kwanza kupungua, ule upendo wa kumpenda mpenzi wako kama unavyojipenda haupo tena, saizi upo upendo wa nipe nikupe.

Tatizo hili ni kubwa sana kwa sisi vijana wa sasaivi hasa kwa wanandoa, tumeshindwa kupendana katika uhalisia wake "tumetanguliza sentensi ya nitapata nini" yaani leo unamtongoza binti anakuambia utaniweza? Sasa nisikuweze kwa lipi wewe tembo? Mwingine anakuuliza nikikukubalia utanipa nini?? Aaaggrrr yaani wanajiweka kimtego mtego, tatizo upendo tumetanguliza vitu tumechukulia kama fursa fulani.

Upendo wa kweli hauangalii vitu, ukimpenda mtu sawa sawa,
1. Hautaangalia madhaifu aliyonayo bali utamvumilia

2. Hautamhesabia makosa kwamba jana ulinifanyia hivi, leo tena..

3. Utakuwa mwepesi wa kumsamehe kwa kuwa unampenda

4. Hautapenda awe katika msongo wa mawazo kwani ndiye furaha yako hivyo utamsaidia

5. Hautamtangaza vibaya kwa marafki hata kama kuna mahali hakutendei haki au hakuridhishi

6. Utaridhika na hali aliyonayo, iwe kiuchumi, kimaumbile au kwa namna alivyo

7. Utamthamini na kumheshimu kama wewe unavyopenda kufanyiwa.

Na upendo wa mtu kwa mwenzi wake unapungua kutokana na yafuatayo:

1. Dharau kwa mwanamke au mwanaume, yaani kuona kama bila wewe yeye hana maisha, au kuona kama wewe ndo umemfanya vile alivyo

2. Kutomsikiliza hasa wanawake wanapenda sana kusikilizwa hata kama jambo la kipuuzi msikilize tuu usipofanya hivyo ataona unampuuza hana maana kwako

3. Kukosa utii hasa kwa wanawake wamekosa utii kwa waume zao,hakuna mwanaume asiyependa mwanamke amtii, na wanawake wengi wanaona kumtii mwanaume ni utumwa hilo ni tatizo.

4. Kusema madhaifu ya mwenzi wako kwa mashost au masela, labda nikuambie kitu cha uhakika si kila mtu anapenda mahusiano yako na mwenzako hivyo ukianza kusimulia ya ndani unampa point ya kukuumiza tumeona na kushuhudia wengi wakipoteza mahusiano yao.

Mwisho kabisa rudisha upendo ule wa mwanzo kwa mpenzi wako na mahusiano yako yatakuwa salama, achana na habari za kuomba omba ushauri juu ya mahusiano yako inapotokea mmetofautiana tafuta suluhu mwenyewe, muwe na siku njema

BILA SHAKA WEWE UNATUMIA VPN YA BURE WEWE!!!

UONGO/KWELI?
 
Back
Top Bottom