Tatizo la umeme Tanzania siyo Bodi ya TANESCO, tatizo ni kukosekana kwa political will na kujaza academicians wasio business plan wala commitments

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
879
4,116
Tatizo kubwa la umeme Tanzania linaanza na msimamo wa wanasiasa. Magufuli alisema hakuna kukatika kwa umeme na akaweza kwa sababu aliweka nadhiri yakutokula matapishi yake. Akakata mirija yote ya wauza majenereta na mafuta waliokuwa wananufaika na mgawo wa umeme.

Sasa hivi kila mtu anafungua kituo cha mafuta kwa sababu anaamini kabisa usipoyanunua kwa ajili ya chombo cha usafiri utanunua kwa ajili ya mifumo ya umeme nyumbani. Viwanda vingi vinatumia sana mafuta kuwasha majenerator na baadhi mitambo inaweza ikachakaa kabla ya muda

BODI ya TANESCO hata tungeshusha viumbe kutoka nchi gani bado haitaweza kuvuka Kiunzi hiki kwa sababu haina nguvu yoyote kisheria kupinga wishes za mwanasiasa. Wakipinga wanatoka na wasipopinga watatoka. Lakini pia sometimes bodi hizi nyeti tuzitenge na watumishi wa dola kwa sababu inapotoka press bodi imevunjwa inaleta tafsiri ya kutumbuliwa kwa mwenyekiti wa bodi au kufeli kwake......huyu mtu ni mtumishi ambaye kwa cheo alichokuwa nacho kwenye dola kinatia doa viongozi waandamizi wa dola.

Nadhani ni wakati sasa wa kuchukua tahadhari kabla ya kuteua na baada ya kuteua ili ikiwezekana hawa wazee wetu waliojenga heshima yao muda mrefu wasitiliwe shaka kuhusu uwezo wao wa kuleta matokeo chanya.

Political will ikiwa strong hata kama hakuna bodi mambo yatakwenda kwa sababu kila ukiamka utawaza umeme...kila ukisali kama mtumishi wa TANESCO utasali ukame usitokee kwasababu ndio umepoteza kazi ...kila ukisikia transfoma imeibiwa utaunda mikakati ipatikane na kuweka sheria kali.......kila ukisikia Luku inasumbua utawalipa vijana wakae standby kushughulika na mfumo.

Sasa hivi TANESCO unashindwa kujua tatizo ni maji au nini? Maana mvua zimenyesha ila mgao upo palepale na hakuna kauli yakueleweka kuhusu chanzo cha tatizo. Tuwalinde wazee wetu hawa wamefanya mengi kwa nchi yetu
 
Mleta mada umechanganya mambo sana. Kama unazungumzia political will kwa Tanzania ni mtu mmoja tu ndiye anayemiliki political will ya nchi nzima. Ndiye pekee ambaye anachotaka au anachoruhusu ndicho hufanyika.

Wazee wa heshima? Huo ni mzaha. Nchi haina haja ya watu wa aina hiyo. Hao huishia kupiga magoti kwa mteuzi wao. Kinachohitajika ni mipango sahihi ya kitaifa, taaluma sahihi, matumizi sahihi ya rasilimali na udhibiti makini wa rasilimali za umeme. Muamuzi wa yote hayo ni mmoja tu.

Kwa kiwango cha ufisadi na hujuma kinachofanyika kwenye sekta ya umeme ni hakikisho kuwa hali ya kusua sua itaendelea kuwa suala la kudumu hadi siku wananchi watakapokuwa na uwezo wa kudhibiti political will nchini. TANESCO haina kauli kwenye hilo. Inaamrishwa tu.
 
Binafsi sijui kwanini kumekuwa na ulazimu wa kuitengenezea TANESCO mapungufu ya kila aina na kuitafutia sababu za kila aina ya kumernyoko kwamba haiendesheki na inakosa ufanisi.

Yaani wanataka(wahujumu) kuifanya TANESCO kama mgonjwa asietibika halafu mwisho wa siku waje waseme Euthanasia itumike.

Euthenasia ni mauaji yasiyo na uchungu(painless killing) ya mgonjwa anayeugua ugonjwa usiotibika au aliye kwenye Coma. Tatizo ambalo naona wengi wanaliona ni kwamba TANESCO sio mgonjwa na hana ugonjwa usiotibika au coma na hivyo basi kukosekana sababu ya kufanya Euthanasia au mauaji haya. Sijui kuna Kansa aina gani huko lakini ni lazima ishughulikiwe.

Hatahivyo nachelea kuafiki hakuna utashi wa Kisiasa(political will if I may) bali Ufisadi wa hali ya Juu. Kuna sehemu nilishwahi kushauri wale wanaopenda kutafuta taarifa za "uhujumu uchumi" waangalie yaliyojiri kwenye Kampuni kama TANESCO ya Puerto Rico PREPA
Vilevile pitia hapa
Ripoti ya IEEFA: Athari za kashfa ya ununuzi wa mafuta ya muda mrefu

...utaona madudu ni yale yale utafikiri wame copy na kupaste.

Niseme tu, wahujumu wote watakao bainika wakamatwe wanyongwe na wakifa warudishwe kwenye gridi ya TANESCO wapigwe shoti za umeme halafu wanyongwe tena. aarrrrgh
 
..muda si mrefu Tanesco itauzwa.
Ndicho wanachotaka kufanya, itoshe TANESCO imo kwenye makubaliano ya awali kati ya Tanzania na Dubai...kulikozaliwa scandal la DPW na naamini wazi kwamba kama isingekuwa makelele ya DPW TANESCO ingekuwa bye bye. Kwani walishakubaliana kuimega mega.

...wacha ninywe uji kwanza duh
 
1. Hapo kwenye kukosekana political will umepatia kabisa.
2. Cha pili ni ubabaishaji. Watanzania tumekuwa wababaishaji kwa kila kitu tunachofanya. Hakuna accountability, hakuna ufanisi wowote kwa kila tunachofanya, and nobody cares!
3. Ufisadi, uzembe, rushwa, nk.
Hao academicians hata kama wangekuwa na business plan nzuri namna gani, kama culture na mazingira ya kufanyia kazi yamejaa hayo niliyoyataja hapo juu, lazima watamezwa na kuwa sehemu ya huo uozo uliojaa kwenye society yetu.
 
Tatizo ni dogo sana lakini Watanzania tunakosa akili.

Tanesco ikatwe ki mikoa tu, hapo hata serikali kusimamia itakuwa wepesi, kila mkuu wa mkoa atadili direct na watu wake umeme unapokosekana.

Yanesco imekuwa kubwa kuliko uwezo wa Mtanzania kuiendsha, hata serikali nzima ikihamia Tanesco bado tutakosa umeme mara kwa mara.

Uendeshaji mbovu na hatuna uwezo wa kurekebisha, tanesco kuanzia mfagiaji anataka ale mpaka juu huko, utawadhibiti wangapi?


Kuna mitaa umeme unazimwa makusudi ili watu wajipatie pesa. Fikiri mtu anaeendesha kiwanda unafikiri ataona tabu kumpa fundi wa tanesco laki mbili ili amuwashie umeme? Transfoma lazima ziunguwe, waya lazima zikatike, matatizo hayataisha eneo hilo.
 
Nina mashaka na gesi na mauziano...kama vile pumzi ya serikali imekata.
 
Mama SSH sio mfatiliaji wa mambo, anaendesha nchi kwa kurelax sana. Rais inatakiwa uwe mfatiliaji wa kila kitu sio kutegemea tu ushauri kutoka kwa wasaidizi wako, yaani katika kipindi ambacho pesa inapigwa serikalini basi kipindi hiki upigaji umezidi maradufu na hiyo yote ni kwa sababu mama sio mfatiliaji wa mambo katika serikali yake. Tutegemee madudu na baadae Tanesco nayo kuuzwa kama ilivyouzwa bandari.
 
Tatizo kubwa la umeme Tanzania linaanza na msimamo wa wanasiasa. Magufuli alisema hakuna kukatika kwa umeme na akaweza kwa sababu aliweka nadhiri yakutokula matapishi yake. Akakata mirija yote ya wauza majenereta na mafuta waliokuwa wananufaika na mgawo wa umeme.

Sasa hivi kila mtu anafungua kituo cha mafuta kwa sababu anaamini kabisa usipoyanunua kwa ajili ya chombo cha usafiri utanunua kwa ajili ya mifumo ya umeme nyumbani. Viwanda vingi vinatumia sana mafuta kuwasha majenerator na baadhi mitambo inaweza ikachakaa kabla ya muda

BODI ya TANESCO hata tungeshusha viumbe kutoka nchi gani bado haitaweza kuvuka Kiunzi hiki kwa sababu haina nguvu yoyote kisheria kupinga wishes za mwanasiasa. Wakipinga wanatoka na wasipopinga watatoka. Lakini pia sometimes bodi hizi nyeti tuzitenge na watumishi wa dola kwa sababu inapotoka press bodi imevunjwa inaleta tafsiri ya kutumbuliwa kwa mwenyekiti wa bodi au kufeli kwake......huyu mtu ni mtumishi ambaye kwa cheo alichokuwa nacho kwenye dola kinatia doa viongozi waandamizi wa dola.

Nadhani ni wakati sasa wa kuchukua tahadhari kabla ya kuteua na baada ya kuteua ili ikiwezekana hawa wazee wetu waliojenga heshima yao muda mrefu wasitiliwe shaka kuhusu uwezo wao wa kuleta matokeo chanya.

Political will ikiwa strong hata kama hakuna bodi mambo yatakwenda kwa sababu kila ukiamka utawaza umeme...kila ukisali kama mtumishi wa TANESCO utasali ukame usitokee kwasababu ndio umepoteza kazi ...kila ukisikia transfoma imeibiwa utaunda mikakati ipatikane na kuweka sheria kali.......kila ukisikia Luku inasumbua utawalipa vijana wakae standby kushughulika na mfumo.

Sasa hivi TANESCO unashindwa kujua tatizo ni maji au nini? Maana mvua zimenyesha ila mgao upo palepale na hakuna kauli yakueleweka kuhusu chanzo cha tatizo. Tuwalinde wazee wetu hawa wamefanya mengi kwa nchi yetu
Hakuna cha political will wala ushuzi.

Toka lini serikali ikaweza kuendesha shirika la kibiashara? Siyo Tanzania tu, popote duniani?

Ni ujinga tu uliyotujaa.

Utatuzi: tanesco ismbaratishwe, kila mkoa ujitegemee kwa umeme, mkoa unaoshindwa, linawekwa shirika binafsi mkoa huo.

Hiyo ni permenent solution. Kwa kuwa mashirika yote yatayoendeshwa kiserikali yataishia njiani na kampuni binafsi zinazoweza zitaendesha umeme kifaida.
 
Tatizo ni dogo sana lakini Watanzania tunakosa akili.

Tanesco ikatwe ki mikoa tu, hapo hata serikali kusimamia itakuwa wepesi, kila mkuu wa mkoa atadili direct na watu wake umeme unapokosekana.

Yanesco imekuwa kubwa kuliko uwezo wa Mtanzania kuiendsha, hata serikali nzima ikihamia Tanesco bado tutakosa umeme mara kwa mara.

Uendeshaji mbovu na hatuna uwezo wa kurekebisha, tanesco kuanzia mfagiaji anataka ale mpaka juu huko, utawadhibiti wangapi?


Kuna mitaa umeme unazimwa makusudi ili watu wajipatie pesa. Fikiri mtu anaeendesha kiwanda unafikiri ataona tabu kumpa fundi wa tanesco laki mbili ili amuwashie umeme? Transfoma lazima ziunguwe, waya lazima zikatike, matatizo hayataisha eneo hilo.
Lakini si kuna uongozi wa tanesco kila mkoa hadi mawilayani huko au? Vyeo kama meneja wa mkoa. Meneja wa kanda wa tanesco si vipo? Tatizo la Tanesco ni wanasiasa wala sio menejimenti ya Tanesco. Tanesco ndo shirika linaloongozwa kwa kufanyiwa hujuma na ufisadi na wanasiasi, kumbuka kashfa ya Escrow na nyinginezo.
 
Lakini si kuna uongozi wa tanesco kila mkoa hadi mawilayani huko au? Vyeo kama meneja wa mkoa. Meneja wa kanda wa tanesco si vipo? Tatizo la Tanesco ni wanasiasa wala sio menejimenti ya Tanesco. Tanesco ndo shirika linaloongozwa kwa kufanyiwa hujuma na ufisadi na wanasiasi, kumbuka kashfa ya Escrow na nyinginezo.
Hilo ndiyo Tatizo, kwa kuwa uongozi wote mpaka wa kijijini unachukuwa maagizo kutokea makao makuu, sasa fikiri ukiritimba uliopo njiani hapo mpaka ufike makao makuu.

Solution ni kubomoa tu, iwe kama mashirika ya maji, kila mkoa unajitegemea.
 
Tatizo kubwa la umeme Tanzania linaanza na msimamo wa wanasiasa. Magufuli alisema hakuna kukatika kwa umeme na akaweza kwa sababu aliweka nadhiri yakutokula matapishi yake. Akakata mirija yote ya wauza majenereta na mafuta waliokuwa wananufaika na mgawo wa umeme.

Sasa hivi kila mtu anafungua kituo cha mafuta kwa sababu anaamini kabisa usipoyanunua kwa ajili ya chombo cha usafiri utanunua kwa ajili ya mifumo ya umeme nyumbani. Viwanda vingi vinatumia sana mafuta kuwasha majenerator na baadhi mitambo inaweza ikachakaa kabla ya muda

BODI ya TANESCO hata tungeshusha viumbe kutoka nchi gani bado haitaweza kuvuka Kiunzi hiki kwa sababu haina nguvu yoyote kisheria kupinga wishes za mwanasiasa. Wakipinga wanatoka na wasipopinga watatoka. Lakini pia sometimes bodi hizi nyeti tuzitenge na watumishi wa dola kwa sababu inapotoka press bodi imevunjwa inaleta tafsiri ya kutumbuliwa kwa mwenyekiti wa bodi au kufeli kwake......huyu mtu ni mtumishi ambaye kwa cheo alichokuwa nacho kwenye dola kinatia doa viongozi waandamizi wa dola.

Nadhani ni wakati sasa wa kuchukua tahadhari kabla ya kuteua na baada ya kuteua ili ikiwezekana hawa wazee wetu waliojenga heshima yao muda mrefu wasitiliwe shaka kuhusu uwezo wao wa kuleta matokeo chanya.

Political will ikiwa strong hata kama hakuna bodi mambo yatakwenda kwa sababu kila ukiamka utawaza umeme...kila ukisali kama mtumishi wa TANESCO utasali ukame usitokee kwasababu ndio umepoteza kazi ...kila ukisikia transfoma imeibiwa utaunda mikakati ipatikane na kuweka sheria kali.......kila ukisikia Luku inasumbua utawalipa vijana wakae standby kushughulika na mfumo.

Sasa hivi TANESCO unashindwa kujua tatizo ni maji au nini? Maana mvua zimenyesha ila mgao upo palepale na hakuna kauli yakueleweka kuhusu chanzo cha tatizo. Tuwalinde wazee wetu hawa wamefanya mengi kwa nchi yetu
Toa siasa za kipuuzi wewe,Kauli hazizuii kukatika Kwa umeme.

Umeme sio Kauli ulikatika kama kawaida ila nyie mapunda wake naona mnatumia Nguvu sana kulazimisha uongo.
 
Hilo ndiyo Tatizo, kwa kuwa uongozi wote mpaka wa kijijini unachukuwa maagizo kutokea makao makuu, sasa fikiri ukiritimba uliopo njiani hapo mpaka ufike makao makuu.

Solution ni kubomoa tu, iwe kama mashirika ya maji, kila mkoa unajitegemea.
Solution ni kuruhusu washindani wengine, TTCL inashindana na VODA/TIGO n.k na hiyo imesaidia sn
 
Hata waje malaika kwenye bodi kuiongoza bado mgawo utakuwepo

Ova
 
Back
Top Bottom