Tatizo la ulevi Rombo: Wanawake wakodi wanaume kutoka Kenya kufanya nao ngono

Hii ina maanisha nchi yetu sasa imeanza ku import wanaume.!!!!

Shillingi itapanda kweli.????
 
HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO

TANGAZO LA KAZI

Halmashauri ya wilaya ya Rombo kwa kushirikiana na chama cha wanaume rijali Tanzania (CHAWARITA) inatangaza nafasi elfu saba na miatano (7500) za Maafisa Rijali (AR) watakaofanya kazi katika zoezi la uboreshaji wa ndoa rombo na kuiepusha wilaya kutokana na kizazi cha wakenya.

Muda wa Mkataba wa kazi ni mpaka ambapo kina swai Massawe Mushi na kina Mlacha watakapoacha kupiga kilaji na kuurudia urijali wao.

Sifa za Mwombaji
1. Awe ni Mtanzania mwenye umri usiozidi miaka 45 mwenye uzoefu katika masuala ya ndoa michepuko au fani inayofanana na hiyo.

2. Mwombaji aambatanishe CV akielezea uzoefu wake katika mapenzi na picha mbili (Passport size)

3. Waombaji ambao si wachagga watapewa kipaumbele.

4. Mwombaji asiwe mlevi maana rombo idadi ya bar na nyumba ni sawa.

5. Mwombaji aambatinishe nakala za vyeti vya magonjwa ya zinaa ikiwemo UKIMWI kutoka katika hospitali inayotambiliwa na serikali.


Mwisho wa kupokea Maombi ni tarehe 22/05/2015 saa SITA na NUSU usiku. Maombi yatumwe au kuletwa kwa:-

MKURUGENZI WA WILAYA,
HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO,
S. L. P 3040,
KILIMANJARO.

Ndorrrrobbbo....

Hap Red angalia sana na ujifunze.... sio kila jina la kichagga linapatikana Rombo.... afu hiyo buku kanunue gazeti ujipepee....
 
Nonesense. Wanawake kibao tena walioko kwenye ndoa wana mahusiano nje ya ndoa na wanaume wengine wakati hao wanaume wao wa ndoa hawajui hata harufu ya pombe. Naona Gazeti la Mwananchi linaanza kuwa kama magazeti ya udaku sasa.

Duu! Kuna Watu Vilaza Aisee, Umepiga Viroba Vingapi Mkuu.
 
Maana hapo wamekutana.
Maana haya wanawake wa huko kwenye mapenzi sio kabisaaa tasteless .
Ndio maana wameenda Kenya kuchukua vimeo wenzao.

Kwa hiyo mkuu wewe unazifahamu ladha za wanawake wa rombo na wanaume wa kenya wote?
 
Inaonekana eneo la Kenya mpakani na Rombo wanaume wake hawajaathirika na pombe. Kenya hili tatizo ni kubwa kuliko hata Tanzania. Kumbuka wanawake wa central kenya walipoamua kuwachapa hawa wanaume.Pombe haramu haziuzwi baa. viroba vinauzwa hata kwenye maduka ya kawaida. Hata wilaya ya hai ninakotoka hali ni mbaya. wanaume hasa vijana wa 20-30s wamepotelea kwenye pombe. wanalala nazo na kuamka nazo. kazi hawafanyi wanachukua vijimali vya nyumbani hata chakula cha watoto wanaenda kuuza wapate hela ya pombe. wanawake wakikosea wakaweka hela hovyo zinaibwa ili pombe ikanunuliwe. Viroba vimesambaa na kupata umaarufu kupita kawaida. mzigo wa maisha umewaelemea wanawake. huko hai wanadai sababu ni kuanguka kwa zao la kahawa ambapo kumewafanya wanaume wakose shughuli za kiuchumi za kufanya!?! arusha nako hivyo hivyo....maisha magumu yanafanya wanaume wapunguzie mawazo kwenye viroba, matokeo yake nguvu ya kuzaa na kufanya kazi inapotea.

Ukweli kabisa
 
Huu ndio uzuri wa nji hii. Jambo serious namna hii watu wanafanya mzaha. Tatizo la pombe ni la nchi nzima. Pita Kariakoo biashara inayokesha pale ni ya viroba. Kwetu Maruku kule Bkb ni hivyo hivyo. Inawezekana tunawavumilia maana tumeshindwa kuwasaidia kwa njia mbadala, tunawaacha wenyewe viroba kujisahaulisha masaibu yao. Hiyo ya Uchagani (sio Rombo tu) nimewahi kuisikia eti sasa watoto wa kuanza Shule hakuna. Jambo hili ni vema likaangaliwa critically maana sio suala la Chadema wala CCM. Hebu tuangalie mambo yanayohusu mustakbali wa nchi kwa miwani mikubwa zaidi!!
 
Nimejionea hali ilivyo Rombo kupitia report maalum Itv, Hali ni mbaya akina mama wanalalamika hawapati huduma, uzalishaji mali kwa wanaume ni mdogo sana kwa sababu ya ulevi wa pombe za kienyeji!rai yangu vyombo husika vichukue hatua kali za kisheria dhidi ya hawa watengenezaji. Lasivyo hili ni janga.

ILA NIWAPONGEZE HAWA WACHAGGA!mwonekano wa hayo mazingira haufananii na hao walevi! Najiuliza ni nan wanaojenga huko vizuri namna hyo ilihali wenyeji ni pombe tuu

Wanaojenga huko wako mijini mkuu
 
Niliwahi kuandika hapa kipindi fulani kule rombo shule hazina watoto, tatizo ni wanaume kushindwa kuwazalisha wake zao kutokana na ulevi uliopindukia. Tatizo ni Kubwa something must be done to save this generation
 
Back
Top Bottom