Hiyo hali imenitokea wiki 2 zilizopita nilipata shida kwa mda wa wiki 1, dalili ilianza kama mafua makali, kinywa kilikuwa kichungu, baada ya hapo kooni kunakuwa kama kuna kitu, ukilazimisha kukohoa tunatoka tupande tweupe tugumu tunanuka, kwa sasa mi niko fresh.
Mama watoto nae kabanwa na hali hiyo nae anasema kama kuna kitu kipo kooni akilazimisha kukohoa tunatoka huto tujamaa tweupe tugumu.
Ko nami nimetia kambi hapa kujua hali hiyo inasababishwa na nini na tiba yake ingawa mi nilipona bila kutumia tiba yoyote.