Tatizo la macho, jicho kutoa kinyama juu

Tatizo la macho, jicho kutoa kinyama juu

Kalaga Baho Nongwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2020
Posts
11,301
Reaction score
25,780
Wakuu kwema?

Kuna changamoto hapa jicho limetoa kijipu kina takriban miezi mitatu hakiponi wala hakipotei kama kilivyoadiriwa.

Ni dawa gan inatibu hili?
20250406_120929.jpg

Cc. DR HAYA LAND
 
Wakuu kwema?

Kuna changamoto hapa jicho limetoa kijipu kina takriban miezi mitatu hakiponi wala hakipotei kama kilivyoadiriwa.

Ni dawa gan inatibu hili?
View attachment 3294721
Cc. DR HAYA LAND

Pole sana.

Hii kitaalamu inaitwa Chalazion (meibomian cyst/eyelid cyst ), ni uvimbe wa kope (sio tafsiri rasmi).

Chalazion ni uvimbe unaotokea kwenye sehemu kope (eyelid ) kutokana kuziba kwa tezi ya mafuta (meibomian gland) iliyoko kwenye kope. Tezi ya meibomian huzalisha mafuta ya kufanya jicho kuwa na unyevunyevu wake, hivyo ikizibwa uvimbe huo hutokea.

Chalazion huwapata watu wenye umri wa miaka 30 hadi 50 japo inaweza pia kutokea kwa watoto.

Chalazion huanza taratibu lakini mara nyingi haiumi lakini inaweza kusababisha muwasho kidogo, uoni hafifu nk.

Matibabu:
-Kanda kwa kitambaa kisafi kilicholowekwa kwa maji ya uvuguuvgu kwa dakika 15 (warm compresses).
-Usafi macho: epuka makeup, epuka kugusa macho mara kwa mara.
-Mara nyingi chalazion hupotea yenyewe: kama haitaisha basi muone daktari ili iweze kutolewa.

Kila la kheri.
 
Back
Top Bottom