Tatizo la CRDB Simbanking

Tatizo la CRDB Simbanking

Mkuu nadhani si vyema kuiita ya kifala bali tuseme tu ni huduma nzuri lakini itumie tu pale ambapo huna suruhisho lingine,mfano binafsi huwa inanisaidia sana nikiwa vijiji vya mbali kusiko na ATMs bali kuna MPESA na TigoPesa.

Kila kizuri hakikosi kasoro.


Narudia tena...

Simbanking ni Huduma ya Kifala sana, hasa kwa sisi tulio mjini hapa...
Kwanza ni expensive, na bado Double Makato...

Nikitaka kutoa laki tano :
Yaani nihamishe pesa kutoka Simbanking kwenda Mpesa/Tigopesa nakatwa 6000.

Bado kuitoa Mpesa/Tigopesa kuiweka mkononi nakatwa 6000.
Jumla nakatwa 12,000. Si upimbi huo???

Kwa jinsi ATM zilivo tapakaa hapa Dar ningekatwa 1800 tu kwa ajili ya transaction fee.
Kwa Lugha ya kiuchumi nakua nimeokoa 10,000.

Habari za Simbanking pelekeni huko Vijijini...
 
Kitu chochote duniani kinachotumia computer system kweny emergency ujue umeliwa ...... DUNIANI............. Shateseka Las Vegas balaa na CC then wakati narudi LA - LAX ikakubali....
Sio kweli unachosema! Sehemu nyingine hata kama kuna issue huwa wanaweka solution mbadala.
 
Sio kweli unachosema! Sehemu nyingine hata kama kuna issue huwa wanaweka solution mbadala.

Kila kitu kina emergency, mimi nimetumia VISA yangu USA na hapakuwa na mbadala zaidi ya cash niliyokuwa nayo mkoloni. Mbadala ni wako sio wa Bank!
 
Kwa uzoefu wangu, jitahidi usifanye transaction kati ya 12 jioni mpaka SAA 2 usiku. Mara nyingi hata ATM zinakuwa offline
 
Mimi nilishamtumia mtu pesa mara tatu, yaani nimemtumia mara ya kwanza CRDB hawatoi feedback yoyote, mtu analalamika hajapata salio, naangalia salio linaonyesha halijatoka, nikatuma mara ya pili napo vilevele, mbaya zaidi CRDB hawa inform hata kwamba ombi lako linashughulikiwa, wanapiga kimya. Nikaamua kuweka cash ili nitume pesa, nikatuma kwa tigo pesa, sasa baada ya masaa kama sita zile transaction zote zilizogoma zikaenda kwa mpigo, ikabidi niingie kwenye zoezi lingine la kumwomba jamaa anitudishie na kwa bahati nzuri alikuwa mwaminifu, ila hii huduma sio ya kuaminika sana
 
Natumia Crdb sim banking mwaka wa nne huu na sijawahi pata tatizo lolote.. Bank naingia kama Nina shida ya hela kubwa tu 1m+
 
Sikilizeni mazee...

Simbanking ni Huduma expensive sana, inakutia umasikini kama hujui...

Mfano :
Kuhamisha tuu 10,000 kutoka Simbanking kwenda Mpesa /Tigopesa unakatwa 2130.
Wakat kama unngeenda ATM makato ni 944.

Twende :
Kuhamisha 500,000 kutoka Simbanking kwenda Mpesa/Tigopesa unakatwa 6000.
Wakati kama ungeenda ATM makato ni 1888.

Conclusion:
Tuache tabia za Uvivu, kupenda shortcut.
Kama unaweza kwenda ATM ni bora mara 100% kuliko kutumia Simbanking.
Simbanking ni gharama sana, unganisha na changamoto kama hizo juu za Wadau wanatoa hela, hawazioni mpaka wasubiri masaa 24.

Kama hiyo haitoshi:
Kumbuka kuna gharama za kutoka Simbanking kwenda Mpesa/Tigopesa, jumlisha na gharama za kutoa hela Mpesa/Tigopesa kwenda mkononi.

Simbanking ni Huduma ya kifala, japo inaokoa safari za kwenda ATM.
Safari ya kuwasha Gari kutafuta ATM naunguza mafuta ya shilingi ngapi? What about time etc?
24 hours not 25 sorry
 
Mzee mm naona Simbanking Ni huduma nzuri Na inarahisisha sana utumaji wa hela, ilisha wahi kunitokea Mara moja sikupata ela Ila baada ya muda niliipata mm nachukulia hamna kitu kizuri kisichokuwa Na challenge zake tujivunie vya kwetu Na tuwape muda wa kuiboresha zaidi Na zaidi huduma hiyo SImbanking ndo mpango mzima Crdb Benki yangu SIBANDUKI!
 
Ukweli ni kwamba hii ni moja ya changamoto zilizopo, lakini ukweli unabaki kuwa simbanking ni huduma muhimu sana na inasaidia kiasi kikubwa
 
Safari ya kuwasha Gari kutafuta ATM naunguza mafuta ya shilingi ngapi? What about time etc?


Kuwasha Gari kutafuta ATM???
Ndio nasikia kwako....

Kwa jinsi atm zilivotapakaa hapa Dar...

Bila shaka wewe utakua upo mikoani
 
Kila kitu kina emergency, mimi nimetumia VISA yangu USA na hapakuwa na mbadala zaidi ya cash niliyokuwa nayo mkoloni. Mbadala ni wako sio wa Bank!
Bila shaka kama uliwahi kukumbwa kadhia ya VISA card kutofanya kazi kwa muda (kitu ambacho hakitokei sana) basi kulikuwa na ATM karibu.... ndio mbadala huyo! Ama!
 
Kuwasha Gari kutafuta ATM???
Ndio nasikia kwako....

Kwa jinsi atm zilivotapakaa hapa Dar...

Bila shaka wewe utakua upo mikoani
M'bongo kwa ubishi htamweza mkuu. Hii simcard banking ni zaidi ya kero. Naona pengine unajaribu kuelewesha watu waliozea shida na tabu (ambazo nyingi husababishwa uzembe kama part and parcel of life! Hawatakuelewa kamwe!
 
Yaani, huduma kama ya wacheza kamari. Unapewa maagizo bonyeza 1, bonyeza... mwisho, hakuna pesa wala habari hadi uwapigie. Mara waseme baada ya masaa 4 mara, baada ya masaa 24.

Sasa hii kweli si usumbufu mkubwa?.

Ni tahadhari kwa wote, msiamini sana huduma hii. Imenikasirisha sana.
mwenzagu, nilitaka kununua hisa za voda kupitia *150*36# basi tukaanza bonyeza bonyeza bonyeza mwishowe nikaambulia sms disconnected! kutizama salio kweupe.
 
Leo wamenirudishia. Ila inakasirisha. Tunaomba waongeze customer care. Mbona walianza vizuri tu?.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom