CRDB, fanyieni kazi tatizo la business transactions, nmeshindwa kupata huduma

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
15,106
27,090
Siamini kama crdb wamekuwa wababaishaji kiasi hiki...

Miezi miwili iliyo pita nilijaza fomu ya kujiunga na online purchasing...

Nikaambiwa nitatumiwa Temporary Access code ndani ya masaa 24. Zikapita siku mbili sijatumiwa hiyo namba, nikamwambia kuulizia kulikoni. Kama kawaida Yao wakaomba namba ya akaunti, namba SITA za Mwanzo za kwenye card number yangu na namba nne za Mwisho. Nikafanya kama walivyo agiza then nikaaambiwa after 24 hours nitatumiwa namba..

Two days later number bado haijatumwa. Nikaamua kwenda makao makuu.
.
wakachukua details zangu nikaaambiwa nitatumiwa namba baada ya masaa 24.

siku tatu zikapita bila majibu. Nikapiga simu.. nikaambiwa Tena ntatumiwa namba baada ya masaa 24..

seven hours later nikatumiwa temporary access code...

Kwenda kwenye website Yao nikafanya kama walivyo elekeza..

Sehemu ya majina yangu nikajaza jina la Mwanzo na la mwisho Kwa herufi kubwa then nikaweka na hiyo temporary access code Yao..

Baada ya Ku click, ikaleta majibu Password and names do not match.

Nikajaribu mara ya pili, password and names do not match.


mara ya tatu nikaambiwa the service has been suspended.

nikapiga simu nikaambiwa ntatumiwa access code nyingine after two hours.

after two hours HAKUNA namba iliyo tumwa, kupiga simu nikaambiwa after twenty four hours natumiwa namba..

toka mwezi wa tatu mwishoni mpaka WA huu WA SITA majibu NI Yale Yale..

Watu wengi wanawalalamikia crdb kuhusu huduma hii.

crdb badilikeni SASA... Vunjeni kitengo chenu cha IT ni wababaishaji mno..

watu tunashindwa kufanya business transactions Kwa sababu ya uzembe na ubabaishaji wa IT experts wenu.


personally nimevunja account yangu ya crdb.

hela zote nimehamishia Standard Chartered Bank..

sijui NI wateja wenu wangapi watakuwa wamefanya hivi.

yani watu wenu wa it wanafanya mambo kienyeji Sana. Like seriously!!! Yani hawawezi kufanya majukumu Yao mpaka uwapigie kuwakumbusha?

This is too unprofessional. Enzi za Kimei hakukuwaga na ubabaishaji kama huu.

IT EXPERTS wa Standard Chartered Wana kitu gani ambacho IT experts WA Crdb hawana?

how comes nimeenda Standard Chartered nimefungua account, Kadi ilivyo kuwa activated nikaenda kujiunga na huduma ya online purchasing na imekuwa activated ndani ya siku moja?


Nitamshauri vp MTU anaetaka kujiunga na huduma ya online purchasing akafungue akaunti Crdb wakati Standard Chartered wapo?

Hata ngombe Hawezi kuyapeleka Makinda yake kunywa maji kwenye kisima chenye maji machafu wakati anajua mahali kilipo kisima chenye maji masafi.

Dunia ya sasa karibu kila kitu kinafanyika online..Taasisi kubwa kama crdb inakuwa na experts wanao fanya ubabaishaji kwenye kitengo muhimu kama hicho inakuwa haimake sense..

Kwa usumbufu mlio nifanyia mngeufanya Kwa mtu kama Mtikila am sure as hell huko mahakamani kungekua na jalada linalosomeka MTIKILA Vs CRBD.

Angewashtaki for the breach of contract

crdb lifanyieni kazi Tatizo haraka iwezekanavyo.

asanteni na kwaherini
 
Charles Kimei wa CRDB, Nehemia Mchechu wa NHC na Ramadhan Dau wa NSSF ni mapacha watatu wa awamu ya Nne ambao ndio walikuwa think tank ya JK

Hakuna Siku Ndege ya JK iliruka kwenda Nje ya Nchi kwa ziara ya Kikazi ikakosa mmoja kati yao

Kweli Mzee Mwinyi alisema ''…Kila zama na kitabu chake…'
 
Unahangaika nini na hao tumia Mpesa au airtel mastercard ukiona haitoshi nenda chukua card ya bank ABC isiyokuwa na akaunti pesa unaweka via simu
PayPal wakakubali MPesa Master Card?
 
CRDB is a local bank,full of people from nothern part of tanzania.Hata mikopo yao ni ovyo kabisa wanakwapua nssf za watu as if hiyo mikopo haina bima.Kimbia haraka kutoka kwenye hii local bank,wanaoperate chini ya kiwango cha kibubu.
 
Crdb Nmb Tpb - Usithubutu kutumia hizi bank kwenye online purchasing. Utajuta

Benki za kutumia kwenye online purchasing ni ABC na Exim ndo wako vizuri. Equity wako vizuri kwenye payment (one way payment) ila usiitumie ku receive hela wana usumbufu kwenye kupata hela kutoka online.

~ Experienced user
 
CRDB haijaanza huo ushamba leo. Toka Kimei yupo hapo wamekuwa wanafanya mambo ya kishamba vilevile.

Nakumbuka 2013, niliwaomba wa-activate card yangu kufanya online transaction. Wakanijazisha forms.

Nilifuatilia ile form mwezi mzima wananipiga kalenda. Nikahamia Standard Chartered Bank. Toka siku hiyo sijajutia.

Leo hii unaweza fungua account kwa App ya SC bila kwenda bank. Na kila kitu ukaattach hapohapo. Haya mambo Crdb hawawezi.

Crdb na Nmb ni benki local, zina wafanyakazi wanaowaza kilocal zaidi.
 
Kimei kutengeneza ukabila crdb hana legacy ya kumkumbuka.

Crdb caribu heads wote wa idara, sections and branches utakuta ni ndugu zake/wakaskazini wenzake.

A country with over 50m people kupendelea watu wa kanda yako pekee ni ujinga ambao hauna mfano.
 
Nahitaji hii huduma nami nifungue akaunti yangu nipe procedure kiongozi
CRDB haijaanza huo ushamba leo. Toka Kimei yupo hapo wamekuwa wanafanya mambo ya kishamba vilevile.

Nakumbuka 2013, niliwaomba wa-activate card yangu kufanya online transaction. Wakanijazisha forms.

Nilifuatilia ile form mwezi mzima wananipiga kalenda. Nikahamia Standard Chartered Bank. Toka siku hiyo sijajutia.

Leo hii unaweza fungua account kwa App ya SC bila kwenda bank. Na kila kitu ukaattach hapohapo. Haya mambo Crdb hawawezi.

Crdb na Nmb ni benki local, zina wafanyakazi wanaowaza kilocal zaidi.
 
kuna jambo ambalo Serikali inatakiwa kuliangalia katika Taasisi zake. Taasisi inapokuwa na watu wa jamii moja tu ni tatizo kiutawala. sababu ni nini ? sababu ni kwamba watu hao kuingia kwao katika hiyo taasisi mara nyingi ni 'undugunization' sasa mtumishi wa hivyo anakuwa na ''network'' ndani ya Taasisi kiasi kwamba hata kumtawala inkuwa shida. watu wamekuwa wanalalamikia sana CRDB , lakini watumishi hawajali, unafikiri tatizo nini ? si mtu anakuwa anakiburi cha undugu uliopo kwenye Taasisi, utamfanya nini !!
 
kuna jambo ambalo Serikali inatakiwa kuliangalia katika Taasisi zake. Taasisi inapokuwa na watu wa jamii moja tu ni tatizo kiutawala. sababu ni nini ? sababu ni kwamba watu hao kuingia kwao katika hiyo taasisi mara nyingi ni 'undugunization' sasa mtumishi wa hivyo anakuwa na ''network'' ndani ya Taasisi kiasi kwamba hata kumtawala inkuwa shida. watu wamekuwa wanalalamikia sana CRDB , lakini watumishi hawajali, unafikiri tatizo nini ? si mtu anakuwa anakiburi cha undugu uliopo kwenye Taasisi, utamfanya nini !!
CRDB ni taasis binafsi siyo yaserikali, serikali ina hisa ndogo pale.
 
Back
Top Bottom