Tathmini ya robo ya kwanza ya Mwaka, CHADEMA yaongoza

Tathmini ya robo ya kwanza ya Mwaka, CHADEMA yaongoza

Taarifa zako tutasoma hatuna namna kwasababu chadema Chama kikubwa nchini japokua ccm inarobotatu ya ukubwa inaowazini ,mkilimudu hilo mliloliazisha ,katiba ,tume huru ya uchaguzi 2025 octoba ccm tutapoteana ....ila mkiingia uchaguzi mambo mawili hayo Yako hivohivo .....mmekwisha
 
....cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kama chama cha siasa Maarufu zaidi Nchini....
Kuna muda Hata Al-qaeda ilikuwa maarufu sana.

Kikubwa ni tija ipi watanzania wanajivunia umaarufu huo wa Chama Hiki cha Siasa katika kujikwamua kikweli kweli kutoka minyororo ya utumwa kiuchumi iliyofungwa na kufuli la "mabeberu uchwara" walio nje ya mipaka ya nchi yetu?
 
Wadau wa Siasa Duniani wanakitaja Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kama chama cha siasa Maarufu zaidi Nchini Tanzania katika robo ya Kwanza ya mwaka, Chadema inatajwa Dunia nzima kama chama cha siasa kinachoongoza harakati zote nchini Tanzania, ikiwemo harakati "Tukufu" ya Mapambano ya Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, ambacho ndio kilio kikuu cha Watanzania.

Taarifa zingine zinadai kwamba Ujio wa Tundu Lissu na Godbless Lema, pamoja na kishindo cha Mikutano Kabambe ya hadhara iliyopangwa Kisomi na kuvurumishwa kwenye kanda kadhaa imekifanya chama hicho kujizolea umaarufu mkubwa, si tu Tanzania bali Dunia nzima.

Hata hivyo Taarifa kutoka ndani ya Chama hicho inaeleza kwamba kuanzia mwisho wa mwezi huu ndio kinaanza rasmi kufanya mikutano ya hadhara Nchi nzima na kwamba ile mliokuwa mnaiona huko Kanda ya Nyasa ilikuwa "FAGIA UWANJA TU" Mliokuwa mnaangalia sinema zamani mtanielewa kwamba kabla ya picha yenyewe kuanza , mlionyeshwa vipande fulani vilivyoitwa "Trela" ili kuwashawishi mlipe kiingilio kabla ya picha lenyewe kuanza .

Mungu Ibariki Chadema.

Mwisho, lakini si kwa Umuhimu, Nawashukuru Wana JF wote wa Jukwaa hili kwa kuniamini .
Kulamba asali
 
Pamoja na ushindi lakini baadhi ya Wadau wamenishambulia mno kwamba sikustahili na kwamba nimependelewa , lakini nawashukuru wote kwa ujumla wao.

Hata hivyo naahidi taarifa kemkem za kweli sana na za haraka sana kwenye Jukwaa hili kwa mwaka huu.
_ubarikiwe sana kamanda
 
Back
Top Bottom