Tathmini: Lowassa amemfunika Dr. Slaa

Tathmini: Lowassa amemfunika Dr. Slaa

Wakati ule haukuwa muungano kama sasa, na wakati ule wapiga kura hawakuwa wengi kama mara hii, mara hii wamekuwa mara 2 ya 2010, kama unatazama hivyo Hata magufuli kapata kura nyingi zaid ya kikwete 2010

Usiropoke bila ya kuelewa. Angalia zaidi asilimia ya kukubalika. Si kila mwana-UKAWA amempigia kura Lowassa

Mzee Tupatupa
 
Usiropoke bila ya kuelewa. Angalia zaidi asilimia ya kukubalika. Si kila mwana-UKAWA amempigia kura Lowassa

Mzee Tupatupa

Nadhani wewe ndio unaropoka, hebu chukua kura za lipumba 2010 add za Slaa 2010 , Halafu chukua za wale washirika pia,add kwa Slaa,Halafu chukua wapiga kura wa 2010 na wa sasa utapata jibu, sijaona ongezeko lolote la kura za lowassa, hata kama ukawa wangekuwa lema hizi hizi kura zingefika
 
Slaa ni bora mara 200 kuliko Lowassa.Lowassa ni nguvu ya FEDHA na kumbuka kaanza kitambo 2008.Halafu Lowassa amekuwa "backed up" na UKAWA ambayo ni vyama vinne.Kwa vyama 4 plus Lowassa mwenye nguvu ya fedha 39% ni ndogo sana.SILAA WA 2010 WATU WALIMPENDA KUTOKA MOYONI KABISA NIKIWEMO MIMI SEMA CCM WALITUMIA UZOEZI WA MIAKA 50 NA NILIUMIA ALIVYOSHINDWA INGAWA ALINITOKA AKILINI ALIVYOANZA KUTUMIWA NA MBOWE-SAKATA LA ZZK.Lowassa kaua vyama 4 kwa mpigo.SUBIRI MTAFUTANO UANZE MAANA KUNA (TeamLowassa,4U Movement,CDM Asilia,NCCR Mageuzi,NLD na CUF).

We Wacha tu hizo pesa za ruzuku watatafutana kwa tochi. khe khe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Last edited by a moderator:
Licha ya mimi kuwa mwanaccm lakini ninakili haya matokeo sikuyategemea..rsilimali ccm ilizotumia,wasanii,kuchonganisha ukawa hadi dr silaa na prof libpumba wakaondoka..kujumlisha na record ya magufuri..bado tumepata kula 58% na kupoteza ngome muhimu kama mbeya,iringa,tanga,arusha na huenda jiji la dar+mtwara....hii inaonyesha ccm kama ingemusimamisha asharose migiro au yule mama wa zanzibar basi ccm tungeshindwa vidaya.ingebidi tume ifute uchaguzi ili kutunyenyua.haya matokeo kwa ccm siyo ya kushangilia sana

Umeongea ukweli kabisa nadhani pombe magufuli ana kazi ya ziada kuaminisha wananchi kuwa hawakukosea kumchagua
 
Usiangalia kipimo kimoja kama vile kura peke yake. Angalia pia muda. Je Lowasa angegombea 2010 angepata kura alizopata Dr. Slaa? Tafiti zote zinazingatia pia muda. Wakati wa sasa wapiga kura wengi wameongeza uwelewa wao. Mafanikio ya Lowasa ya sasa yamelala juu ya juhudi binafsi za Dr. Slaa kuwaamsha kuwaelimisha watanzania na kuujenga upinzani. Lowasa ni mwizi wa matunda aliyoivisha Dr. Slaa. Huwezi kumpambanisha anayetaka vya bwerere na mtafutaji. Lowasa ni mwizi wa pesa mwizi wa juhudi za watu na mwizi wa sifa za wengine
Pamoja na kutoshinda kwa Ndugu Edward Ngoyai Lowassa, bado kuna haja ya kufahamu kuwa Lowassa amemzidi na kumfunika Dr. Slaa aliyegombea mwaka 2010 kupitia CHADEMA. Mwaka 2010, kura zilizopigwa zilikuwa 8,398,394 na Dr. Slaa alipata kura milioni 2.2 ambazo ni sawa na asilimia 26.34 ya kura zote. Mwaka huu, zilipigwa kura 15,193,863 na Lowassa kupata kura milioni 6 na ushee sawa na asilimia 39.97.

Mshindi wa mwaka 2010,Rais Kikwete alipata asilimia 61 na wa mwaka huu amepata asilimia 58.46. Ukitazama kwa jicho kali, utaona na kujua kuwa Lowassa amemzidi kwa mbali sana Dr. Slaa. Pia, CCM imeendelea kupungua kwa asilimia za kura zake. Ni wazi sasa kuwa, Lowassa ameongeza hta majimbo ya uchaguzi kwa CHADEMA na CUF pamoja na vyama hivyo kupoteza baadhi ya majimbo yao.

Lowassa amesaidia kupoka ngome mbalimbali za CCM na kuzikabidhi CHADEMA na CUF. Mwaka huu, kwa uwiano wa kura za wagombea wa Urais wa Tanzania, CHADEMA itapata nafasi za viti maalum kwa wingi zaidi na kutoachwa mbali na CCM kama ilivyokuwa mwaka 2010. Haya pia ni mafanikio yaliyoletwa na Lowassa huko CHADEMA na kumzidi kwa mbali Dr. Slaa wa mwaka 2010. CHADEMA ilicheza karata zake vyema.

Kila la kheri watanzania!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Kwa back up ya Sumaye,Kingunge na makapi kibao pamoja na bajeti aliyoitumia Edo sioni unafuu wowote labda kama ujio wake ulilenga kumfunika Slaa.
 
Pamoja na kutoshinda kwa Ndugu Edward Ngoyai Lowassa, bado kuna haja ya kufahamu kuwa Lowassa amemzidi na kumfunika Dr. Slaa aliyegombea mwaka 2010 kupitia CHADEMA. Mwaka 2010, kura zilizopigwa zilikuwa 8,398,394 na Dr. Slaa alipata kura milioni 2.2 ambazo ni sawa na asilimia 26.34 ya kura zote. Mwaka huu, zilipigwa kura 15,193,863 na Lowassa kupata kura milioni 6 na ushee sawa na asilimia 39.97.

Mshindi wa mwaka 2010,Rais Kikwete alipata asilimia 61 na wa mwaka huu amepata asilimia 58.46. Ukitazama kwa jicho kali, utaona na kujua kuwa Lowassa amemzidi kwa mbali sana Dr. Slaa. Pia, CCM imeendelea kupungua kwa asilimia za kura zake. Ni wazi sasa kuwa, Lowassa ameongeza hta majimbo ya uchaguzi kwa CHADEMA na CUF pamoja na vyama hivyo kupoteza baadhi ya majimbo yao.

Lowassa amesaidia kupoka ngome mbalimbali za CCM na kuzikabidhi CHADEMA na CUF. Mwaka huu, kwa uwiano wa kura za wagombea wa Urais wa Tanzania, CHADEMA itapata nafasi za viti maalum kwa wingi zaidi na kutoachwa mbali na CCM kama ilivyokuwa mwaka 2010. Haya pia ni mafanikio yaliyoletwa na Lowassa huko CHADEMA na kumzidi kwa mbali Dr. Slaa wa mwaka 2010. CHADEMA ilicheza karata zake vyema.

Kila la kheri watanzania!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Sawa ameongeza ushindi kumbuka 2010 Dr. Slaa alikuwa na kura za chadema tuu, wakati sasa hivi Lowasa ana kura wa apiga kura wa CUF pia. Ushindi wa sasa hivi umechangiwa na mambo mengi likiwepo la vyama kuunganisha nguvu, mbona lenyewe hamlisemi?
 
Kwanza kama ulifuatilia vizuri uchaguzi wa 2010, uchaguzi wa sasa hivi hata kama Lowasa asingesimamishwa na chadema ungekuwa na ushindani mkali tuu, hususan baada ya vyama vya upinzani kuunganisha nguvu. Hilo halipingiki kabisa kama unabisha wewe ni mbishi tuu.
 
Hujaelezea hapo katikati ya 2010 na 2015 effort aliyoweka Dr Slaa kuimarisha na kupanua chama..
Ukweli ni huu, siku Lowassa amepitishwa na UKAWA kugombea, CCM ilifanya sherehe maana walijua hiyo move ingekuwa mwanzo wa mwisho wa agenda ya ufisadi (agenda pekee iliyoipandisha chadema chati)...In short, watu wenye akili (wanajiita Chadema Halisia) walishtukia sanaa za Mbowe na wakakaa pembeni...
Sasa tumeshuhudia Lowassa akisimama majukwaani pamoja na rejects- Kingunge, Lau Masha, Sumaye and the likes...
Imagine hayo majukwaa yangekuwa replaced na Dr Slaa na Lipumba!
#MboweMustGo


CCM wanajitenga na ajenda ya ufisadi kwenye majukwaa ya kisiasa wakati Chadema wana nafasi ya uthibitsja kiuhalisia ktk maisha ya kawaida. Baada ya siasa za jukwaani CCM sasa hivi watalazimika kutenda matendo yanayopinga rushwa. Sasa hivi wasipokuwa makini hakuna mtu yeyote atakayewaelewa 2020 maana kiutendaji bado watu wanaamini CCM bila rushwa ni kama haiwezekani.
 
Kwanza kama ulifuatilia vizuri uchaguzi wa 2010, uchaguzi wa sasa hivi hata kama Lowasa asingesimamishwa na chadema ungekuwa na ushindani mkali tuu, hususan baada ya vyama vya upinzani kuunganisha nguvu. Hilo halipingiki kabisa kama unabisha wewe ni mbishi tuu.


Siyo kweli, CCM walipiga bao upinzani baada ya kumsimamisha magufuli ambaye anakubalika hata na wapinzani, lkn UKAWA pia walipinga bao walipomsimamisha Lowassa ambaye anakubalika pia na wananchi wengi licha ya kuandamwa na kashfa ya Richmond ambayo wengi wanaamini ina ajenda ya kisiasa ndani yake.
 
Wakati ule haukuwa muungano kama sasa, na wakati ule wapiga kura hawakuwa wengi kama mara hii, mara hii wamekuwa mara 2 ya 2010, kama unatazama hivyo Hata magufuli kapata kura nyingi zaid ya kikwete 2010

Thread inataja idadi na aslimia. Wewe unaongelea idadi tu..... Umegundua ulipokosea? % n number
 
Huwezi kumlinganisha Dr slaa na lowassa. Hasa kwenye upande wa kiuchumi ambayo ni sifa muhimu ya kujitafutia umaarufu.
 
Pamoja na kutoshinda kwa Ndugu Edward Ngoyai Lowassa, bado kuna haja ya kufahamu kuwa Lowassa amemzidi na kumfunika Dr. Slaa aliyegombea mwaka 2010 kupitia CHADEMA. Mwaka 2010, kura zilizopigwa zilikuwa 8,398,394 na Dr. Slaa alipata kura milioni 2.2 ambazo ni sawa na asilimia 26.34 ya kura zote. Mwaka huu, zilipigwa kura 15,193,863 na Lowassa kupata kura milioni 6 na ushee sawa na asilimia 39.97.

Mshindi wa mwaka 2010,Rais Kikwete alipata asilimia 61 na wa mwaka huu amepata asilimia 58.46. Ukitazama kwa jicho kali, utaona na kujua kuwa Lowassa amemzidi kwa mbali sana Dr. Slaa. Pia, CCM imeendelea kupungua kwa asilimia za kura zake. Ni wazi sasa kuwa, Lowassa ameongeza hta majimbo ya uchaguzi kwa CHADEMA na CUF pamoja na vyama hivyo kupoteza baadhi ya majimbo yao.

Lowassa amesaidia kupoka ngome mbalimbali za CCM na kuzikabidhi CHADEMA na CUF. Mwaka huu, kwa uwiano wa kura za wagombea wa Urais wa Tanzania, CHADEMA itapata nafasi za viti maalum kwa wingi zaidi na kutoachwa mbali na CCM kama ilivyokuwa mwaka 2010. Haya pia ni mafanikio yaliyoletwa na Lowassa huko CHADEMA na kumzidi kwa mbali Dr. Slaa wa mwaka 2010. CHADEMA ilicheza karata zake vyema.

Kila la kheri watanzania!


Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam


Zaidi ya hayo imeonekana pia kuwa Lowassa amepata kura nyingi zaidi (zaidi ya milioni 6 kuliko aliyechaguliwa mwaka 2010 Rais Kikwete aliyeshinda kwa kura milioni tano na ushee. Teh teh
 
Pamoja na kutoshinda kwa Ndugu Edward Ngoyai Lowassa, bado kuna haja ya kufahamu kuwa Lowassa amemzidi na kumfunika Dr. Slaa aliyegombea mwaka 2010 kupitia CHADEMA. Mwaka 2010, kura zilizopigwa zilikuwa 8,398,394 na Dr. Slaa alipata kura milioni 2.2 ambazo ni sawa na asilimia 26.34 ya kura zote. Mwaka huu, zilipigwa kura 15,193,863 na Lowassa kupata kura milioni 6 na ushee sawa na asilimia 39.97.

Mshindi wa mwaka 2010,Rais Kikwete alipata asilimia 61 na wa mwaka huu amepata asilimia 58.46. Ukitazama kwa jicho kali, utaona na kujua kuwa Lowassa amemzidi kwa mbali sana Dr. Slaa. Pia, CCM imeendelea kupungua kwa asilimia za kura zake. Ni wazi sasa kuwa, Lowassa ameongeza hta majimbo ya uchaguzi kwa CHADEMA na CUF pamoja na vyama hivyo kupoteza baadhi ya majimbo yao.

Lowassa amesaidia kupoka ngome mbalimbali za CCM na kuzikabidhi CHADEMA na CUF. Mwaka huu, kwa uwiano wa kura za wagombea wa Urais wa Tanzania, CHADEMA itapata nafasi za viti maalum kwa wingi zaidi na kutoachwa mbali na CCM kama ilivyokuwa mwaka 2010. Haya pia ni mafanikio yaliyoletwa na Lowassa huko CHADEMA na kumzidi kwa mbali Dr. Slaa wa mwaka 2010. CHADEMA ilicheza karata zake vyema.

Kila la kheri watanzania!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

[TD="class: xl65, width: 35"] [/TD]
[TD="class: xl65, width: 44"]CCM %[/TD]
[TD="class: xl65, width: 75"]CHADEMA %[/TD]
[TD="class: xl65, width: 175"]VYAMA VYOTE VILIVYOBAKI %[/TD]
[TD="class: xl65, width: 62"]UKAWA %[/TD]
[TD="class: xl65, width: 135"]VYAMA VILIVYOBAKI %[/TD]
[TD="class: xl66, width: 45"]100%[/TD]

[TD="class: xl65"]2010[/TD]
[TD="class: xl65"]61[/TD]
[TD="class: xl65"]26[/TD]
[TD="class: xl65"]13[/TD]
[TD="class: xl65"]NIL[/TD]
[TD="class: xl65"]NIL[/TD]
[TD="class: xl65"]100[/TD]

[TD="class: xl65"]2015[/TD]
[TD="class: xl65"]58[/TD]
[TD="class: xl65"]NIL[/TD]
[TD="class: xl65"]NIL[/TD]
[TD="class: xl65"]38[/TD]
[TD="class: xl65"]4[/TD]
[TD="class: xl65"]100[/TD]

Siyo kweli : 2010 (Vyama vya upinzani vilipata jumla ya 39% (26 % + 13% =39% ambavyo mwaka huu 2015 wanaita Ukawa 38% +4%) unaona tofauti ni ndogo sana, pia ukiangalia pesa ambazo Lowasa alishawekeza havilingani kabisa na na uo ushindi, wakati huo huo Dr. Slaa hakuwekeza pesa nyingi.
 
Hujaelezea hapo katikati ya 2010 na 2015 effort aliyoweka Dr Slaa kuimarisha na kupanua chama..

#MboweMustGo

Kwa bahati mbaya hili linaweza lisionekane, vijana wengi waliandaliwa kugombea mwaka huu na hii inajionyesha katika majimbo ambayo CHADEMA imeshinda ubunge lakini kura za Urais CCM wanaongoza.

Lowassa kasaidia sana kupunguza kura za CCM na si kuimarisha CDM, hatujui kama hawa watu wake watabaki upinzani au watarudi kwao
 
Hujaelezea hapo katikati ya 2010 na 2015 effort aliyoweka Dr Slaa kuimarisha na kupanua chama..
Ukweli ni huu, siku Lowassa amepitishwa na UKAWA kugombea, CCM ilifanya sherehe maana walijua hiyo move ingekuwa mwanzo wa mwisho wa agenda ya ufisadi (agenda pekee iliyoipandisha chadema chati)...In short, watu wenye akili (wanajiita Chadema Halisia) walishtukia sanaa za Mbowe na wakakaa pembeni...
Sasa tumeshuhudia Lowassa akisimama majukwaani pamoja na rejects- Kingunge, Lau Masha, Sumaye and the likes...
Imagine hayo majukwaa yangekuwa replaced na Dr Slaa na Lipumba!
#MboweMustGo

Ni hivi mi ntakuwa wa kwanza kuandamana kupinga hilo lako unalolisema... Mbowe Must stay.... he is there to stay!!! Wewe si ulikuwa ccm sasa ya CDM yanakuhusu nini???
 
Slaa ni bora mara 200 kuliko Lowassa.Lowassa ni nguvu ya FEDHA na kumbuka kaanza kitambo 2008.Halafu Lowassa amekuwa "backed up" na UKAWA ambayo ni vyama vinne.Kwa vyama 4 plus Lowassa mwenye nguvu ya fedha 39% ni ndogo sana.SILAA WA 2010 WATU WALIMPENDA KUTOKA MOYONI KABISA NIKIWEMO MIMI SEMA CCM WALITUMIA UZOEZI WA MIAKA 50 NA NILIUMIA ALIVYOSHINDWA INGAWA ALINITOKA AKILINI ALIVYOANZA KUTUMIWA NA MBOWE-SAKATA LA ZZK.Lowassa kaua vyama 4 kwa mpigo.SUBIRI MTAFUTANO UANZE MAANA KUNA (TeamLowassa,4U Movement,CDM Asilia,NCCR Mageuzi,NLD na CUF).

Umesema kweli ndugu yangu! Dr.Slaa alipata 26% akipambana na Rais aliye mamlakani tena aliekuwa ana kibindoni na 80%, Chadema ilikuwa na Mgogoro wa ndani na Zitto, haikuwa na Backup wala fedha za kampeni leo baada ya kazi kubwa ya uhamasishaji 2010-2015, sapoti ya umoja wa Ukawa, ukwasi wa fedha zilizotumika, mpasuko uliotokea ccm watu kuhama, ccm kuleta mgombea mpya n.k Wamepunguza kura za urais ccm kutoka 61% ya Rais Kikwete mpaka 58% za Rais Mteule Dr.Magufuli i.e only 3% tena baada ya wazee na kina mama wengi kuogopa fujo kupiga kura, Dr.Slaa alisema Siasa ni Science Mbatia akapinga akasema ni Sanaa saaa kaona matokeo ya sanaa za mgombea wake!
 
Back
Top Bottom