Tathimini: Wamefanikiwa kutisha na kudhibiti Vyombo vya Habari kwa asilimia kubwa ila pia wameshindwa kudhibiti habari kwa asilimia kubwa zaidi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,022
144,380
Ukweli ni kwamba, hawa Bwana wakubwa wamefanikiwa sana katika kupandikiza hofu na uoga katika jamii yetu na hata katika vyombo vyetu vya habari lakini wamefeli sana katika azima yao ya kutaka umma usipate habari wanazotaka zisifike kwa umma.

Kwanini nasema hivi?

Kuna mambo/matukio ambayo yakitokea, vyombo vyetu vya habari havithubutu kuandika, kuhoji wa kujadili kwa hofu ya kushughulikiwa lakini mwisho wa siku wao wenyewe wanachukua nafasi ya media kutangaza jambo husika kupitia media hizo hizo wanazozidhibiti

Kwa namna gani hali hii inatotokea?

Panapotokea jambo kubwa na zito ambalo wao hawataki wananchi walijue, watu kupitia mitandao ya kijamii, huanza kuliibua na kulijadili jambo husika usiku na mchana kiasi kwamba huwalazimu wao kama wenye mamlaka kujitokeza kulitolea ufafanuzi jambo husika.

Nini hutokea baada ya hapo?

Kitendo cha wao kujitokeza hadharani na kujibu au kutolea ufafanuzi jambo husika,hutoa nafasi kwa vyombo vya habari kuripoti jambo husika kwa umma na hivyo kuibua mijada zaidi.

Kwahiyo, kinachotokea au kinachofuata baada ya hapo, hua ni kufungua mijadala kuhusu jambo hilo katika vyombo vya habari , na matokeo yake ni kuwafanya hata wale wanaoishi gizani kujua nini kinaendelea na hapo kunakuwa hakuna tena siri/kuficha habari kwa umma.

Kwahiyo, katika hili, utagundua work done ni zero or almost equal to zero.

Wanaangamia kwa kukosa maarifa!
 
Inaitwa vicious cycle, utazunguka weeeh lkn mwisho wa siku utarudi palepale.

IMG_20210311_211226.jpg
 
What a load load of rubbish! These are scurrilous insinuations, halftruths, completely devoid of merit. Unaowaita "Vyombo vya Habari" ni watu sawa na wewe au mimi, Watanzania wenzetu, wengi wao ex-TANU Youth League, yaani ni sawa tu na Maaskofu. Usishangae ukiona wanachagua mchele wanaacha chuya. Hivi kweli Mtanzania kawaida, awe ni Askofu au Editor wa Daily News au Majira, atakubali atumike kumsaidia tundulissu au fatmakarume kusambaza matusi yao? Au aombe madhabahuni? Subutu!

If the Press don't report the dirt and scum ya Mabeberu na vikaragosi vyao wale wanaotusaliti, ni uzalendo si woga. Mbowe aliwatukana TBC hazalani siku ile, akawafokea akawafukuza Uwanja wa Taifa, unakumbuka? Kesho yake Vyombo vyako vya habari, VYOTE (kupitia Jukwaa la Wahariri), wakaja juu, vikagoma, walimwita wakamuonya, kesho yake (akiwa Mbeya na Sugu kama sikosei) ikabidi ang'ate matapishi yake in pubric. Uliona kura za Sugu?

Hayo ndiyo mazao ya mgombeaxwenu tundulissu, elewa kuwa people arevtotall6 fed up, y amewafikavhapa. Umemsikia tundulissu anamuombea kifo rais? Walishindwa kura vibaya, ndiyo maana huwasikii wakilalama, au kwenda mahakamani. They knew ut! They expected it. Dr Slaa got 40% bila matusi wala majigambo ya Amsterdam? TANU Youth League iko hadi Kipalapala na Makumira mpaka leo hii.

Wacha habari hizi ni ngojera za watoto hazina mshiko.
 
What a load load of rubbish! These are scurrilous insinuations, halftruths, completely devoid of merit. Unaowaita "Vyombo vya Habari" ni watu sawa na wewe au mimi, Watanzania wenzetu, wengi wao ex-TANU Youth League, yaani ni sawa tu na Maaskofu. Usishangae ukiona wanachagua mchele wanaacha chuya. Hivi kweli Mtanzania kawaida, awe ni Askofu au Editor wa Daily News au Majira, atakubali atumike kumsaidia tundulissu au fatmakarume kusambaza matusi yao? Au aombe madhabahuni? Subutu!

If the Press don't report the dirt and scum ya Mabeberu na vikaragosi vyao wale wanaotusaliti, ni uzalendo si woga. Mbowe aliwatukana TBC hazalani siku ile, akawafokea akawafukuza Uwanja wa Taifa, unakumbuka? Kesho yake Vyombo vyako vya habari, VYOTE (kupitia Jukwaa la Wahariri), wakaja juu, vikagoma, walimwita wakamuonya, kesho yake (akiwa Mbeya na Sugu kama sikosei) ikabidi ang'ate matapishi yake in pubric. Uliona kura za Sugu?

Hayo ndiyo mazao ya mgombeaxwenu tundulissu, elewa kuwa people arevtotall6 fed up, y amewafikavhapa. Umemsikia tundulissu anamuombea kifo rais? Walishindwa kura vibaya, ndiyo maana huwasikii wakilalama, au kwenda mahakamani. They knew ut! They expected it. Dr Slaa got 40% bila matusi wala majigambo ya Amsterdam? TANU Youth League iko hadi Kipalapala na Makumira mpaka leo hii.

Wacha habari hizi ni ngojera za watoto hazina mshiko.
Wakati unatoa povu hapa JF, jamaa kule Twitter keshaa ashiriia kuwa jambo fulani limetimia. Sasa, kwa habari hiyo, sijui usiku wa leo mtakuwa katika hali gani!!
 
Back
Top Bottom