Eee Mungu, mpe mapumziko ya amani mpendwa wetu Hussein Mkiete (Sharo milionea).Kamwe sitomsahau kijana huyu kwa ubunifu wake wa kuchanganya ucheshi na muziki, na misemo yake ya ucheshi 'umebugi meen! nk.na kupangusa bega lake la kulia kama vile kuondoa uchafu. Ndo maana hussein machozi alimtumia kwenye video yake ya Mzimu wa Babu na kufanya video hiyo kushika chati sana.
Baada ya kuona picha za ajali kama zinavyoonekana hapo juu, nashangaa kuona lami. Awali tuliambiwa kwamba ajali ilitokea kwa sababu gar alokuwa akiendesha limekaa chini mno, ilhali barabara za kijijini ni mbaya. Lakini kwenye post na picha tunaambiwa gari ni toyota harrier. Na toyota harrier haiko chini sana kiasi cha kusababisha ajali.
Poleni sana wanafamilia, Poleni sana wanaJF na pole sana mzee King Majuto.