Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

32



Wanasema hakuna mtu yoyoye aliye suspect ambaye ameshawahi kufanikiwa kutoroka ndani ya Russia akiwa chini ya surveillance ya KGB. Wakuu wa kitengo hususan bwana Victor Grushko akaandaa timu ya kufanya surveillance kwa ajili ya Oleg . Ni kwamba waliamua kumfuatilia Oleg kila mahali alipokwenda. Na Sasa kwa mara ya pili wakasubiri Oleg hayupo nyumbani ,wakaingia kwake kwa Siri na viatu vyote vya Oleg wakapulizia vumbi lenye kemikali za radiation . Hii ni kwamba Oleg akivivaa viatu hivi ,kila atakapokwenda angejulikana. Sababu angekuwa anaacha trail za vumbi lenye radiation kila atakapopita ,na kifaa kitakachotumiwa kumtrack Oleg ni Geiger counter. Kikosi kazi hiki pia waliteua watu special ambao sio rahisi kushtukiwa na Oleg Kwa ajili ya ku keep eyes on him popote aendapo. Na KGB waliamini pia ikiwa familia yake ikirudi Moscow haitakuwa rahisi kwa bwana Oleg kutoroka kwa namna yoyote ile wao wakiendelea kumpeleleza.

Jijini London makachero wa M16 Sasa wakawa full alerted kwamba bwana Oleg yupo kwenye matatizo. Hii ni pale walipopewa taarifa mke wa Oleg naye alipaswa kurejea Moscow. Wakaamini Sasa Oleg Kwa namna yoyote uteuzi wake umekuwa terminated .
Afisa wa M16 alikuwa amedraft plan maalumu ya kumtorosha Oleg nje ya Urusi tokea mwaka 1978 . Hii plan iliitwa PIMLICO na ilikuwa planned na mwanamama Oliver price. Kwa kifupi operation hii ilimtaka Oleg kama atakuwa yupo Moscow na ameingia matatizoni na yupo under surveillance basi ilimpasa Atoe ujumbe kwa njia ya signal kwa afisa wa M16 aliyepaswa kukutana naye . Na signal hiyo ingewajulisha maafisa wote waliopo hapo Moscow na London wawe tayari na timu zilizokuwa zimeandaliwa kwa ajili ya kumtorosha Oleg kupitia nchi ya Finland .
Kwanza hapo kabla Huyu mama alikuwa na options kadhaa ali draft njia za kumtorosha mtu(kama cargo ) kutoka nchi ya Russia kupitia bahari nyeusi Hadi uturuki au bahari ya Caspian Hadi Iran pasipo kushtukiwa. Lakini hii Option ilionekana itakuwa na risk ya kuwa intercepted na maafisa wa Russia wanofanya patrol baharini. Na pia kutoka Jiji la Moscow Hadi mpakani mwa uturuki kulikuwa mbali sana kiasi kwamba barrier zingekuwa nyingi na kukamatwa kutokana na search.
Option ya pili ya mama huyu ilikuwa kumsafirisha mtu kwa Siri kupitia kigezo Cha kidiplomasia. Kwa mfano kwa mujibu wa Vienna convention mizigo kama,silaha,madawa na vilevile watu , haikupaswa kukaguliwa endapo ilikuwa inasafirishwa kama diplomatic luggage inapopita kwenye mipaka ya nchi ,au viwanja vya ndege. Lakini kupitia option hii kulikuwa Kuna risk ya kugundulika . Hii ilitokana pale ambapo mpwa wa rais umaru shagari wa Nigeria aliyepinduliwa 1983 na Obasanjo kugundulika uwanja wa ndege wa Stanstead na maafisa wa ukaguzi. Huyu mpwa wa rais aliitwa umaru dakku na alitekwa akiwa London Kisha akafungiwa kwenye crate kubwa kiasi lililokuwa na lebo ya extra cargo yenye anwani ya wizara ya mambo ya nje ya Lagos kwa ajili ya kusafirishwa Hadi Nigeria. Baada ya maafisa kuhisi mashaka na mzigo huo wakaufungua ndipo wakamkuta huyo dakku akaachiwa free. Tuachane na ya akina Obasanjo......Sasa price aliona akitumia njia hii huenda ikafeli na Oleg akakamatwa. Option nyingine ilikuwa kumsafirisha Oleg kupitia gari lenye diplomatic number linaloendeshwa na maafisa wa ubalozi Kwa maana yalikuwa hayapigwi mkono barabarani kwa ajili ya search kwa mujibu wa Vienna convention. Lakini kumbuka hizo hazikuwa sheria rasmi na Russia wasingesita kupiga search endapo wangetilia shaka gari hata kama ni la diplomatic staff. Hii option nayo ikawa kama haitafanya kazi kutokana na kuwa suspicion.
Option ya mwisho iliyokuwepo na ambayo oliver price aliona kidogo ingefanya kazi ni kumtorosha mtu wao kupitia Finland. Kijiografia nchi ya Finland ndio nchi ya ulaya magharibi iliyopakana na Russia, ingawaje kulikuwa na umbali wa mwendo wa masaa 12 hivi kwa gari kutoka Moscow Hadi mpakani mwa nchi ya Finland. Hivyo price aliona njia hii inaweza kufanya kazi .

ELEWA HAPA
Hii option ya mwisho ilikuwa drafted kama ifuatavyo:
Baada ya Oleg kufanya mawasiliano ya signal na maafisa wa M16 hapo Moscow, nao wawe tayari kwamba mwamba Yuko tayari kusepa . Kisha yeye Oleg mwenyewe asafiri kwa Siri pasipo kugundulika Hadi kwenye rendezvous point (sehemu ya kukutana) iliyo karibu na mpaka wa Russia na Finland . Nao maafisa wa M16 waje kivyao Hadi hiyo rendezvous point wakiwa na magari kadhaa ambazo Zina plate namba za ubalozini wajifanye kama wanaenda vacation. Kisha wambebe Oleg hapo rendezvous point huku akiwa amefichwa kwenye Buti ya gari na kumvusha mpakani Hadi Finland..... Endapo hawatapigwa search hapo mpakani...tuachie hapa kwanza...

Huku Moscow Oleg alifika uwanja wa ndege hapo Moscow kwa ajili ya kuipokea familia yake kutoka London. Na manjagu wa KGB hawakuwa wanacheza mbali naye
Baada ya kukamilisha protocol zote za hapo uwanjani kama mke wa afisa wa kanali wa KGB Leila hatimaye akakutana na mumewe . Kama kawaida mama zetu lawama kwao ni kawaida. Wakiwa wanaelekea nyumbani Kwa gari njiani mama akawa analalamika mara hakupigiwa simu, mara Oleg kaumwa pasipo kumtaarifu n.k. Oleg akampooza mkewe akamwambia tu utakachoambiwa chochote kuhusiana na Mimi usiamini. Kisha akaendelea kumpanga mkewe kwamba Kuna watu wenye roho mbaya kazini wamempondea na majungu Hadi kazi ya ubalozi hapo London ikawa terminated hivyo hawatarudi Tena. Kidogo mkewe akaelewa. Muda wote wakiwa wanaelekea home walikuwa kwenye surveillance ya KGB maana walikuwa wanafuatiliwa na gari kwa nyuma ile ya kuzuga. Baada ya maelezo mengi Hilo likapita. Wakiwa home Sasa bwana Oleg akawa anawaza amchane mkewe kuhusu plan yake ya kutoroka nchini au amezee . Kilichomfanya Oleg kuwaza hivyo ni namna gani ataiacha familia yake nyuma hususan wanawe kipenzi. Mkewe alianza kuona dalili za kwamba mmewe hayuko sawa kabisa kutokana na kuweweseka mara kwa mara Lakini bado Oleg hakutaka kufunguka. Kutokana na Hali ya Oleg ya kisaikolojia kutokuwa katika Hali nzuri ,mama yake Olga alimshauri apumzishe hata akili yake kutokana Hali aliyokuwa nayo (Wao walihisi Oleg ana stress za kutumbuliwa nafasi ya ubalozi ). Laiti wangejua alilokuwa nalo kichwani.

Na kweli Oleg akaomba ruhusa kwa wakubwa wa kitengo kwamba anahitaji kupumzika ku refresh akili na sehemu ya mapumziko alipaswa kwenda kwenye sanatorium Moja yenye majakuzi kwa ajili ya ku refresh akili ambayo ilikuwa exclusive kwa maafisa wa KGB.... Sanatorium hii ilikuwa ipo kwenye mji wa Semyonovskoye uliopo umbali wa maili 60 kusini mwa Moscow. Hivyo Oleg alipewa leave ya wiki mbili kwa ajili ya kupata huduma ya spa kwenye sanatorium hiyo
Sanatorium ni sehemu special iliyotengwa kwa ajili ya kutoa huduma za kitabibu special hususan magonjwa chronic hususan ya kisaikolojia ,na humo Kuna kuwa na huduma za spa n.k.
Lakini kabla ya kuondoka kwenda huko kwenye spa kwaajili ya mapumziko akaona ni Sasa atume signal kwa makachero wa M16 waliopo hapo Moscow kwamba Sasa wajiandae kwa ajili ya kumtorosha . Na sehemu ya signal ilikuwa ni kwenye jengo la katikati ya hapo Moscow la st. Basil sehemu iliyoitwa central market. Hivyo siku ya jumamosi ya tarehe 15 June 1985 akatoka kwake huku akiwa amevaa kofia ya grey ya ngozi akiwa amebeba mfuko wa ulioandikwa Safeway bag.
( Jina la mfuko huu yaani safeway bag ilikuwa ni signal inatumwa kwa afisa wa M16 ambaye angemuona muda huo Oleg hapo kwenye central market basi maana yake ujumbe ungekuwa umetumwa kwamba Yuko tayari kutoroshwa. ... Na huyu afisa ambaye Oleg alipaswa kumpa signal naye alistahili kuwa na mfuko ulioandikwa Harrod bags Ili Oleg akimuona mtu na huo mfuko sehemu hiyo basi aamini ujumbe utakuwa umefika rasmi kwa wahusika.)


Na kweli Oleg akashika njia Hadi kwenye central market lilipo kanisa la mtakatifu Basil hapo Moscow akasimama sehemu ametulia akijizuga kama Kuna mtu anamsubiria hii ni kuepusha kuwasanua maafisa wa KGB waliokuwa wanafuatilia kisiri Siri. Baada ya oleg kusimama kwa muda wa kama dakika kumi hakuona mtu yoyote kati ya wale waliokuwepo hapo aliyebeba mfuko ulioandikwa Harrod bags. Hivyo meseji ikawa haijatumwa au imefeli kuwafikia M16 .. hapo inabidi asubiri zaidi kama wiki 2 Tena mbeleni.
Hilo likapita ..
Oleg akaelekea huko ilipo sanatorium kwa ajili ya ku refresh . Mfuko ule aliuficha kwenye miongoni mwa mizigo aliyoenda nayo huko . Aliamini lazima atapata sehemu nyingine ya kutuma signal kwa M16. Hadi sehemu hiyo aliyofikia Oleg ,bado macho ya KGB yalikuwa nyuma yake . Baada ya kufika alianza kupata huduma za spa na pia jogging za hapa na pale . Na Hadi akiwa jogging kwenye kijipori Cha hapo sanatorium bado alikuwa anafuatiliwa na maafisa wa KGB na alikuwa ikatokea amewaangalia hao maafisa walizuga wanakojoa pembeni. Kwa kifupi haikuwa rahisi kwa oleg kutoroka kukwepa macho ya KGB

Baada ya kurudi kutoka Semyonovskoye akiwa ame relax ,lengo lake lilikuwa ni Moja tu kutuma ujumbe kwa mara ya pili kwa M16 pasipo kugundulika. Lakini kipengele kikawa kwa familia yake . Yeye kama yeye anaweza ku risk maisha yake kwa kutoroka lakini familia yake ? Na aliwaza endapo angetoroka na familia yake kwa pamoja chance ya kukamatwa ilikuwa ni kubwa sana kiasi kwamba wote wangeingia matatizoni .
Safari hii baada ya Oleg kurudi akaamua kumchana plan yake ya kutoroka hapa alitaka kumpima mkewe imani yake . Oleg akamwambia anaonaje wakaenda huko Azerbaijan kutembelea familia ya mkewe Kisha huko watorokee milimani kwa njia ya mkato Hadi uturuki Kisha huko wafanye mpango wa kwenda uingereza? Mkewe alimcheki tu mumewe kwa hizo stori Kisha akamwambia "Don't be idiotic".
Lakini baada ya long discussion na mkewe wakakubaliana yeye Leila na watoto waende Azerbaijan kama mapumziko kumtembelea baba yake ambaye ni mstaafu wa KGB.
Na kweli siku ya mwisho mkewe alienda kufanya shopping za wanawe akiwa na Oleg huku moyo ukimuuma kutokana na kuiacha familia yake Moscow . Alimbusu kwa mara ya mwisho Leila Kisha akaenda kupanda treni kwa ajili ya kwenda huko Azerbaijan kwa baba yake . Oleg akiwa amesimama akiangalia treni ikitokomea aliyopanda mkewe ,alihisi hatia akiamini labda ni mara ya mwisho kuonana na familia yake . Alikuwa broke


Siku ya tarehe 30 June siku ya jumapili Oleg alitaka kutuma Tena ujumbe kwa M16 ,Hivyo aliandika ki memo na kukiweka kwenye bahasha
Ujumbe uliandikwa nanukuu:"AM UNDER STRONG SUSPICION AND IN BAD TROUBLE , NEED EXFILTRARION SOONEST. BEWARE OF RADIOACTIVE DUST AND CAR ACCIDENTS."
Oleg alijua tokea mwanzo alipuliziwa vumbi la mionzi kwenye nguo na pia viatu hivyo ndio maana Sasa alikuwa anafuatiliwa kila mahali .
Sasa ujumbe huu alitaka kuuacha hapo st.basili Lakini kutokana na eneo Hilo kuwa ni sehemu ya ibada hakuruhisiwa kuingia na Kofia. Makachero wa KGB walikuwa wanafuatilia movements zake zote kwa urahisi.Akaona apande Hadi sehemu ya juu ya jengo hilo kwa ajili ya kuweza kumuona afisa wa M16 mwenye mfuko wa Harrod ampe hiyo barua kupitia brush contact.
Brush contact ni pale ambapo unakutana na mtu na kumkabidhi kitu au kupokea kitu pasipo kushtukiwa na mtu aliye pembeni. Mfano mzuri ni kipindi tupo shule ,wakati wa mtihani kile kitendo Cha kupeana kikaratasi chenye majibu baina yako na mwenzako pasipo msimamizi kusanuka.... au kumpa namba ya simu mdada humfahamu Wala hakufahamu kwa Siri Ili muweze kuwasiliana baadaye pasipo kushtukiwa na watu wa pembeni .
Baada ya Oleg kufeli katika kupasisha huu ujumbe akaamua kuchana pasipo kushtukiwa na maafisa wa KGB waliokuwa wanamfuatilia kwa Siri akavitafuna vipande vyote Kisha akavitemea mbali.
Kwa mara nyingine brush contact ikawa imefeli. Signal message sending failed Akarudi kwake kinyonge .
Lakini hakukata tamaa .......
Haya mambo ya signal na code mbona hatari sana
 
Tanga kulikuwa na mama mmoja alikuwa kichaa kwa zaidi ya miaka 30. Mimi nainukia namuona akiwa kichaa na historia yake alikuwa vizuri tu mwanzo na chanzo cha ukichaa wake mauzauza tu.. But mwishoni mwa mwaka 2019 akapona eti ndugu zake walikwenda kwa mganga gani sijui akapona..

Lkn taarifa nyengine inasema mama alikuwa tiss nguli muda wakustaafu umefika ikabidi itengenezwe skendo yakupona kwake..
Kila tukiunganisha doti za ukichaa wake huenda ni kweli alikuwa tiss maana kuna kipindi anaopotea haonekani (sijui alikuwa anapeleka report ).
 
Tanga kulikuwa na mama mmoja alikuwa kichaa kwa zaidi ya miaka 30. Mimi nainukia namuona akiwa kichaa na historia yake alikuwa vizuri tu mwanzo na chanzo cha ukichaa wake mauzauza tu.. But mwishoni mwa mwaka 2019 akapona eti ndugu zake walikwenda kwa mganga gani sijui akapona..

Lkn taarifa nyengine inasema mama alikuwa tiss nguli muda wakustaafu umefika ikabidi itengenezwe skendo yakupona kwake..
Kila tukiunganisha doti za ukichaa wake huenda ni kweli alikuwa tiss maana kuna kipindi anaopotea haonekani (sijui alikuwa anapeleka report ).
Dunia Ina mengi mkuu
 
Tanga kulikuwa na mama mmoja alikuwa kichaa kwa zaidi ya miaka 30. Mimi nainukia namuona akiwa kichaa na historia yake alikuwa vizuri tu mwanzo na chanzo cha ukichaa wake mauzauza tu.. But mwishoni mwa mwaka 2019 akapona eti ndugu zake walikwenda kwa mganga gani sijui akapona..

Lkn taarifa nyengine inasema mama alikuwa tiss nguli muda wakustaafu umefika ikabidi itengenezwe skendo yakupona kwake..
Kila tukiunganisha doti za ukichaa wake huenda ni kweli alikuwa tiss maana kuna kipindi anaopotea haonekani (sijui alikuwa anapeleka report ).
Watu na vitengo vya kazi zao😄😄!!
 
Back
Top Bottom