Tapeli anayesimulia mambo ya Fre Mason

Tapeli anayesimulia mambo ya Fre Mason

Huyo jamaa alionekana maeneo ya Pamba Road Mwanza akauza cd kwa sh 5,000. Watu walivyokataa kununua akashusha bei mpaka sh.1000
 
Safi sana, jitu lolote jinga ni halali kutapeliwa maana mnapenda vitu vyepesi badala ya kuwaza mambo ya maana, hongera zake huyo muuza CD kwa kutafuna pesa ya mjinga.

Si hivo mkuu, ni kwamba anajitia kama mtu wa mungu na kuonya mtendo maovu kwa hivo kama hupendi uovu ni rahisi kunaswa. huwa sinaswi hovyo lakini saari hii nimekuwa ndege mjanja nikanaswa kwenye tundu bovu. nimeaandika haya kuwafanya wengine wasinaswe kama mimi. watu kama hawa wanawafanya watu wazuri wanaosema maneno ya mungu wasisikilizwe.
 
Dah nami yalishanikuta, kuna jamaa wanauza CD mpya za bongo movie mtaa wa msimbazi kwa sh 500 kila moja, nikamchukulia wife 4 maana ndio ugonjwa wake. Alipoanza kutazama ni matangazo matupu mwanzo mpaka mwisho wa CD.
 
Kiingiacho mjini si haramu na pia katika dunia hii, wajinga ndio waliwao.

si swala la wajinga tu mkuu kwamba ndio waliwao. watu kama hawa wanaathiri kazi za wahubiriw engine wenye nia njema. nasitikitika tu kuwa watu wanatapeli kupitia neno la mungu. hii ni kupiga vita imani. ina maana hata katika nyumba za ibada kuna matapeli sasa ndo kusema huko kuna wajinga wanaoliwa?
 
Kwani mkuu hukujiuliza kwa nini asiuze hizo CD huko kwao Kenya? Kwa sababu kila taifa linajua ukitaka faida ya haraka nenda kwa watu wa Tanzania utafanikiwa wao ni rahisi kudanganyika ni sawa na kushuka kwenye mlima kwa baiskeli hakuna kunyonga pedal....

Umenena mkuu, yuko mwingine anaitwa Mbugua kama sikosei. pia yeye ni mkenya anaedai kuwa alikuwa mlokole lakini sasa ni mhubiri wa kiislmu. nilikuwa mahali natenenza simu yangu siku moja fundi alikuwa ameweka Cd ya huyu mhubiri nae alikuwa asimulia mambo hayo ya mafree mason. watu wengi katika nyumba za ibada huzngumzia mambo hayo. kama mtafiti unaweza kutaka kujua zaidi je, hii ni myth au kuna uhalisia? waamini wengi wanapenda kuhusisha mali na umaarufu na mambo haya. kama mwelimishaji napenda kujua zaidi kama hayo yasemwayo yana ukweli. katika harakati hizo nimetapeliwa. sasa naanza kuona haya mambo yanafanana pia na myth!
 
Si hivo mkuu, ni kwamba anajitia kama mtu wa mungu na kuonya mtendo maovu kwa hivo kama hupendi uovu ni rahisi kunaswa. huwa sinaswi hovyo lakini saari hii nimekuwa ndege mjanja nikanaswa kwenye tundu bovu. nimeaandika haya kuwafanya wengine wasinaswe kama mimi. watu kama hawa wanawafanya watu wazuri wanaosema maneno ya mungu wasisikilizwe.
Mkuu toka lini umeanza kufuatilia mambo ya imani? Unabii umenifunulia kuwa una miaka mingi sana hujakanyaga kanisani. Kama si mke na wanao hata jumuiya ingekuwa imeshakutenga.

Unabisha?
 
mzamifu yani umelenga....

mimi na ujanja wangu wote nimetapeliwa na huyu baba, nilinunua cd 2 kufika home kuweka hamna kitu, nikabadilisha hata deki wapi..
kuna baba mwingine jirani yangu ni mstaarabu sana na mtu wa Mungu tulikuwa tunaongelea mambo ya imani akagusia hizo cd alizonunua kumbe na yeye hazikucheza.

kwa kweli ni taadhali watu muwe makini na huyu mbaba mkenya, yuko na wadada wawili na mbaba mwingine..

haya mambo ya freemason yatatupeleka pabaya, kuna watu wamegeuza story za freemason kuwa ndo njia ya kujipatia kipato.
 
Last edited by a moderator:
Pole mkuu siku hizi wajasiriatumbo wako wa kila sampuli
 
mzamifu yani umelenga....

mimi na ujanja wangu wote nimetapeliwa na huyu baba, nilinunua cd 2 kufika home kuweka hamna kitu, nikabadilisha hata deki wapi..
kuna baba mwingine jirani yangu ni mstaarabu sana na mtu wa Mungu tulikuwa tunaongelea mambo ya imani akagusia hizo cd alizonunua kumbe na yeye hazikucheza.

kwa kweli ni taadhali watu muwe makini na huyu mbaba mkenya, yuko na wadada wawili na mbaba mwingine..

haya mambo ya freemason yatatupeleka pabaya, kuna watu wamegeuza story za freemason kuwa ndo njia ya kujipatia kipato.

asante Queeny kwa ushuhuda
 
Mkuu toka lini umeanza kufuatilia mambo ya imani? Unabii umenifunulia kuwa una miaka mingi sana hujakanyaga kanisani. Kama si mke na wanao hata jumuiya ingekuwa imeshakutenga.

Unabisha?

Aspirini una hakika? ungeekuwa unahuduria ungeniona au tunapishana session. au unabii wako ni kama huo wa mkenya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom