Tanzia: Shekh Nassor Bachu amefariki!

Tanzia: Shekh Nassor Bachu amefariki!

Status
Not open for further replies.
Nilikuwa namsikiliza Sheikh Bachu miaka 20 iliyopita. Bado namsikiliza leo. Nitasikiliza mawaidha yake mpaka mwisho wa maisha yangu. Inna lillah wainna ilaih raajiuun
 
Mungu ailaze roho ya marehem mahala pema, naona kama mwaka jana ulikuwa ni wa watu maarufu wa kidunia na mwaka huu ni wa watu maarufu katika ibada zetu. Mara maaskofu mara wachungaji mara Shekhe. Mungu atuepushie visiendelee hivi
 
as usual to muslims

wewe una mke mmoja sawa una vimada wangapi?
ni bora yeye mwenye wake wa tatu akaishi nao kwa uadilifu kuliko wewe mwenye mke mmoja lakini unanuka zinaa una wanawake kila sehemu.
 
Wasifu wa marehemu ameacha wake watatu na watoto15, Mungu amrehemu!!


Ndugu zetu msiokuwa wa-Islam, naona mnachukia na kuogopa sana hili jambo, ila mnatoka nje ya ndoa na mnatarajia malipo siku ya mwisho! Tumehalalishiwa mke zaidi ya mmoja, katika kitabu chenu mnachokiamini sijaona sehemu mlipoharamishiwa mke zaidi ya mmoja, kama ipo naombeni, mitume wengi na watu wema mnaowaamini walioa zaidi ya mke mmoja, sasa mmekatazwa na kitabu kipi wenzetu? Kuoa mke zaidi ya mmoja siyo sheria/lazima, ila kuepuka zinaa ni ruksa kuoa tena kwa sharti la kama utaweza kuishi nao kwa uadilifu. Na Mwenyez Mungu anajua zaidi.
 
Mwenyez mungu akulaze mahala pema pepon ameen, 2takukumbuka kwa kaz kubwa uliyoifanya
 
Kwa hakika jami itamkosa mtu muhimu,ambaye alipenda kusimamia haki na kuifundisha jamii kuishi maisha yanayozingatia upendo.amni na ushirikiano,MUNGU AMUHIFADHI MAHALA PEMA PEPONI AMIIN
 
Shukrani za dhati kwa wana JF wote ambao wamehuzinika na sisi, hasa wasiokua waislamu, lakini wameonyesha respect kwa kiongozi wetu ambae Mawaidha yake huamsha na kuongeza imani ya anae sikiliza.

Innalilahi waina illaihi rajiuni.
 
Ndugu zetu msiokuwa wa-Islam, naona mnachukia na kuogopa sana hili jambo, ila mnatoka nje ya ndoa na mnatarajia malipo siku ya mwisho! Tumehalalishiwa mke zaidi ya mmoja, katika kitabu chenu mnachokiamini sijaona sehemu mlipoharamishiwa mke zaidi ya mmoja, kama ipo naombeni, mitume wengi na watu wema mnaowaamini walioa zaidi ya mke mmoja, sasa mmekatazwa na kitabu kipi wenzetu? Kuoa mke zaidi ya mmoja siyo sheria/lazima, ila kuepuka zinaa ni ruksa kuoa tena kwa sharti la kama utaweza kuishi nao kwa uadilifu. Na Mwenyez Mungu anajua zaidi.

well said brother......salute!!!
 
anasikia,hata kinyantuzi.

Ni "KinyantuzU"

Sasa mbona huwa naona lazima watu wamu-address kwa "ile" lugha? Sijawahi ona watu wakimu-address kwa kinyantuzu, kizaramo, kingoni, etc? prove me wrong. Hasikii lugha zaidi ya "ile"!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom